Sababu 3 Zinazozuia Usifanikishe Malengo Yako.

Sababu 3  Zinazozuia Usifanikishe Malengo Yako.

Katika maisha, kuna sababu nyingi sana ambazo huwa zinasababisha watu washindwe kutimiza malengo yao. Lakini kuna sababu tatu kubwa ambazo zimesababisha watu wengi washindwe kufikia mafanikio kwenye malengo yao. Kimsingi sababu hizi ukiweza kuzikabili, utaweza kutimiza malengo yako kwa haraka sana. Katika makala ya leo nitakushirikisha sababu 3 Zinazozuia usifanikishe malengo yako.

Sababu 3 Zinazozuia usifanikishe malengo yako.

1.Kushindwa kufanya maamuzi.
Watu wengi wameshindwa kufanikiwa kwenye malengo yao na katika maisha yao kwa ujumla kwa sababu walishindwa kufanya maamuzi. Hata wewe inawezekana bado hujafanikiwa kutimiza malengo yako kwa sababu umeshindwa kufanya maamuzi ambayo yangebadilisha maisha yako. Sababu kubwa zinazofanya watu washindwe kufanya maamuzi ni pamoja na hizi zifuatazo:

i. Wanaogopa kujihatarisha (taking risk)
Watu wanaogopa kufanya maamuzi kwa kuogopa kujihatarisha. Wanaogopa kuwa itakuwaje. Hata wewe inawezekana ulitakiwa ufanye maamuzi fulani ambayo yangebadilisha maisha yako, lakini umekuwa ukiogopa itakuwaje ukishindwa kufanikiwa. Kumbuka kuwa, hata usipofanya maamuzi, bado utakuwa unajihatarisha. Unajihatarisha kwa sababu hautafanikiwa.

ii. Wanaogopa watu watawaonaje.
Watu wengi huwa wanashindwa kufanya maamuzi sahihi yakayotimiza malengo yao kwa kuogopa watu watawaonaje. Hata wewe inawezekana unahitajika kufanya kazi fulani, biashara fulani au unahitaji kujiendeleza kielimu, lakini unahofia watu watakusemaje. Kumbuka kuwa, hata usipofanya maamuzi, bado utasemwa tu. Hivyo, ni bora ufanye maamuzi kwani hatma ya maisha yako ipo mkononi mwako.

iii. Wanaamini maisha ni majaaliwa.
Watu wengi ambao huwa wanashindwa kufanya maamuzi wanaamini ipo siku watafanikiwa kwani mafanikio ni majaaliwa. Hivyo hawako tayari kupambania maisha. Hivyo, kama unataka kufanikiwa katika maisha yako, hakikisha unafanya maamuzi bila kuchelewa.

2.Kutokukamilisha mambo.
Hili ni tatizo kubwa sana linalozuia usifanikishe malengo yako. Watu wengi wamekuwa na tabia ya kuanzisha mambo lakini wanashindwa kuyakamilisha. Hata wewe inawezekana ulianza biashara fulani au kazi fulani lakini ukaishia njiani. Inawezekana ulianza kusoma kitabu lakini umeishia njiani na kadhalika. Kumbuka kuwa hauwezi kufanikiwa kwa kuanzisha mambo, bali utafanikiwa kama utakuwa unakamilisha mambo uliyoyaanzisha. Hivyo ninakukumbusha kuwa, ili uweze kufanikisha malengo yako, hakikisha mambo unayoyaanzisha unayakamilisha.

3.Kufanya mambo na kuacha.
Hili ni tatizo kubwa sana linalozuia mafanikio ya watu wengi. Unakuta mtu leo anaanzisha biashara hii baada ya muda mfupi anaona haimlipi anahamia kwenye biashara nyingine. Baadaye anaona nayo haimlipi anahamia kufanya kitu kingine. Unakuta kila kitu anachokifanya kinakuwa hakina mwendelezo. Kumbuka kuwa, ili uweze kufanikiwa, ni lazima ufanye kitu kimoja kwa muda mrefu. Hata kama utakiona hakikulipi lakini baada ya muda kitakuletea mafanikio makubwa.

Swali la leo:
Ni kitu gani ambacho ulianza kukifanya halafu ukaishia njiani?

Ninatamani sana unishirikishe kwa kuandika hapa chini kwenye sanduku la maoni nami nitakurudia ili tupeane ushauri zaidi. Pia kama una swali lolote usisite kuandika swali lako au kwa kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

2 Replies to “Sababu 3 Zinazozuia Usifanikishe Malengo Yako.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp