Rasilimali 3 Unazohitaji Kutimiza Malengo Yako

Rasilimali 3 Muhimu Unazohitaji Uweze Kutimiza Malengo Yako

Watu wengi huwa wanaweka malengo makubwa katika maisha yao lakini wanaofanikiwa kutimiza malengo yao ni wachache sana. Hata wewe unaweza kujiuliza, mwaka uliopita ulikuwa umeweka malengo, je umeweza kutimiza malengo yako kwa kiwango gani? Jibu unalo. Lakini pia mwaka huu inawezekana una malengo ambayo tayari umeyaweka. Ili uweze kutimiza malengo yako, kuna rasilimali ambazo lazima uwekeze. Kila lengo unalopanga litahitaji rasilimali hizi. Katika Makala ya leo nitakushirikisha rasilimali tatu muhimu unazohitajika kuwa nazo ili uweze kutimiza malengo yako.
Rasilimali 3 muhimu unazohitaji uweze kutimiza malengo yako
1. Muda

Muda ndio rasilimali ya kwanza na muhimu sana katika maisha ambayo unahitaji kuweza kufikia malengo yako. Ni rasilimali ambayo inapaswa kulindwa na kutumika kwa uangalifu mkubwa sana. Hii ni kwa sababu muda ukipotea hauwezi kurudishwa (non-renewable resource). Hivyo ili uweze kutimiza malengo yako unapaswa kutumia vizuri muda wako kwenye kile tu ulichojiwekea malengo. Usiruhusu muda wako kupote ovyo. Kumbuka kuwa unaweza kupotesa pesa na ukatafuta nyingine ukaipata. Lakini hauwezi kuurudisha muda uliopotea. Mara nyingi huwa ninaona watu wapo kijiweni, na ukiwasalimia wanasema tupo hapa tunapoteza muda! Wanapoteza rasilimali ya thamani ambayo hawawezi kuirudisha. Hivyo, muda ni rasilimali ya thamani sana kwenye mafanikio yako.
2. Watu
Rasilimali nyingine ambayo utahitaji kuweza kufanikisha malengo yako ni watu. Utahitaji watu wa kukushika mkono, utahitaji watu wa kukusaidia kwenye kazi yako na utahitaji watu kwenye kila unachokifanya.
3. Fedha
Fedha pia ni rasilimali nyingine ambayo ni ya muhimu ili uweze kutimiza malengo yako. Fedha inahitajika katika kuendesha mradi au biashara uliyoianzisha.
Swali la msingi ni hili, kwa nini watu wengi huwa wanashindwa kutimiza malengo yao?
Jibu ni kuwa, watu wengi wanashindwa kutimiza malengo yao kwa sababu huwa wanatapanya rasilimali zao kwenye malengo mengi. Unakuta mtu ameanza biashara ya duka, mara akasikia kilimo cha matikiti kinalipa akaamua kulima matikiti, baadaye akasikia kuwa biashara ya mtandao inalipa akaamua pia kufanya biashara hiyo. Kumbuka kuwa kila lengo linahitaji rasilimali hizi muhimu tatu kama nilivyozielezea hapo juu yaani muda, watu na fedha. Hivyo ukiwa na malengo mengi utashindwa kufanikiwa kwa sababu utakuwa unarashia kwenye kila lengo. Hivyo, ili uweze kufanikiwa kutimiza malengo yako, ni lazima uwekeze nguvu kwenye lengo moja. Nguvu zako zote na rasilimali zako zote ni sharti uziwekeze kwenye lengo moja, hapo mafanikio utayaona. Kumbuka kuwa mafanikio hayaji kwa kufanya vitu vingi, bali yanakuja kwa kufanya kitu kimoja kwa weredi wa hali ya juu. Weredi huu unapatikana pale tu ambapo utakuwa umewekeza rasilimali zako zote kwenye lengo lako yaani pesa zako zote, muda wako wote na watu wa kukusaidia kufikia lengo lako.
Kuna neno la kingereza linalosema FOCUS. Maana ya neno focus ni kuzingatia na kufanya kile ulichokipanga na kukataa kila vishawishi ambavyo vitakuhamisha kwenye kile unachokifanya. Hivyo ili uweze kutimiza malengo yako ni lazima uwe na Focus, fanya kitu kimoja na usiruhusu upepo wowote ambao unaweza kuja kutaka kukuhamisha kwenye kile unachokifanya.
Kwa leo niishie hapo. Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kuweza kufanikisha malengo yako. Kama una maoni au swali, usisite kuandika hapo chini. Pia kwa ushauri wowote, usisite kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye Makala zinazofuata.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

2 Replies to “Rasilimali 3 Unazohitaji Kutimiza Malengo Yako”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp