
Katika maisha ili uweze kufanikiwa, unahitaji rasilimali. Kati ya rasilimali zote ambazo Mungu ametubariki, Muda ndiyo rasilimali ya muhimu sana kuliko rasilimali zote na inapaswa kutunzwa kwa umakini wa hali ya juu. Hii ni kwa sababu, muda ukipotea hauwezi kuurudishwa (non- renewable resource). Muda ni wa thamani kuliko pesa kwani ukipoteza pesa, unaweza kutafuta nyingine ukapata na maisha yakaendelea. Lakini ukipoteza muda hauwezi kuurudisha. Hivyo, ili uweze kufanikiwa ni lazima uweze kufahamu jinsi ya kutunza muda wako. Katika Makala ya leo, nitakushirikisha mbinu mbili ambazo zitakusaidia kutunza muda wako ili uweze kufanikiwa.
Mbinu 2 za kukusaidia kutunza muda wako uweze kufanikiwa.
1. Panga vitu vyako katika mpangilio maalumu (systematic arrangement).
Jambo la kwanza kabisa ambalo litakusaidia kutunza muda wako ni kupanga vitu vyako katika mpangilio maalumu. Kama ni nyumbani weka mpangilio maalumu unaoonesha vitu vyako vitakaaje. Kwa mfano, nguo za kazini mahali zinapokaa, funguo za nyumba, ufunguo wa gari, vitabu na kadhalika. Mpangilio huu utakusaidia kufahamu kila kitu mahali kinapokuwa na hivyo kukusaidia kuokoa muda ambao ungeweza kuupoteza kwa kutafuta vitu. Kama ni ofisini, fanya mpangilio mzuri wa aina za faili. Mfano weka sections mbalimbali zinazotofautisha aina ya faili zilizopo ofisini kwako. Mfano unaweza kutofautisha aina za faili kama vile: Faili za barua, faili za nyaraka, faili za mikataba, faili za mambo ya fedha na kadhalika. Hii itakusaidia kutumia muda mfupi sana kutafuta faili zako. Pia unaweza kuweka mpangilio wa vitu vingine vilivyopo ofisini kwako kama vile vitabu, daftari, peni, mihuri na kadhalika. Kwa kufanya hivyo, utaonkoa muda mwingi sana ambao utautumia kufanya shughuli zingine.
2. Panga vitu vyako siku moja kabla.
Jambo la pili ambalo unaweza kulitumia kutunza muda wako ni kupanga vitu vyako siku moja kabla. Hapa kama unaenda kazini, unaweza kupanga nguo ambazo utavaa na unazitenga kabisa. Pia unatenga vitu vingine ambavyo utakwenda navyo kazini, kama vile vitabu, notebook, laptop na kadhalika. Hii itakusaidia unapoamka kesho, usipoteze muda muda kuanza kutafuta vitu ambavyo unapaswa kuenda navyo kazini. Kwa kufanya hivyo, utaokoa muda mwingi sana ambao utautumia kwa kuwahi kwenye eneo lako la kazi na hivyo kuongeza ubora wa kazi yako.
Kwa leo niishie hapo, nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kutunza muda wako vizuri ili uweze kufanikiwa kwenye maisha yako. Kumbuka kuwa muda ndio rasilimali ambayo ikipotea hauwezi kuirudisha. Kama una maoni au swali lolote, usisite kuandika hapo chini. Pia kama una swali lolote kuhusiana na mada ya leo, usisite kuwasiliana name moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu kwenye Makala zinazokuja.
- Mbinu Tatu Rahisi Za Mafanikio Zinazopuuzwa. - August 9, 2024
- Jinsi Ya Kugundua Kusudi La Maisha Yako - August 7, 2024
- Kanuni za Kujiwekea Malengo - August 5, 2024
One Reply to “Mbinu 2 Za Kukusaidia Kutunza Muda Wako.”