Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

Katika kipindi hiki, maudhui yaliyoandaliwa kwa mfumo wa video ndiyo yanayochukua sehemu kubwa ya maudhui yote mtandaoni. Utafiti unaonyesha kuwa mpaka sasa, video inachukua asilimia 82 ya watu wanaotafuta maudhui mtandaoni. Ikiwa unapenda kufaidika na idadi ya watu wanaotafuta maudhui mtandaoni kwa wingi, basi unahitajika kuanzisha Chaneli ya YouTube. Katika makala ya leo nitakushirikisha mambo 5 ya kuzingatia ili kuwa na chaneli bora ya YouTube.

Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

1.Wekeza katika kupata mada bora zinazoelimisha, Sio Vifaa.
Kifaa pekee unachohitaji kuanzisha chaneli ya YouTube ni simu yenye kamera nzuri. Unachoweza kukosa ni mada bora zinazoelimisha kwa ajili ya video zako. Ikiwa unataka kuwa na chaneli ya YouTube iliyofanikiwa, basi unahitaji kutumia muda kutafakari mada yako. Unaweza kuanza kwa kuandika mawazo 25 hadi 50 kwa ajili ya video zako. Fikiri kuhusu mada za video na utafute YouTube ili kuona mada ulizochagua zina ushindani gani na hivyo kujua unahitaji juhudi kiasi gani ili kushinda ushindani wa chaneli zingine zinazotoa video zenye mada kama za kwako.

2.Andaa video fupi
Watazamaji leo wanatumia muda mfupi sana kusoma au kuangalia habari mtandaoni. Kama ndio unaanza, jitahidi uwe unaweka video fupi. Hii ni kwa sababu Unapoanza, watazamaji wanakuwa hawakujui. Kitu pekee watakachokifanya ni kuangalia maudhui ya video zako kama yanatatua changamoto zao. Hivyo weka video fupi na zenye ujumbe ili kuwafanya watazamaji wako wafurahie na bila kuchoka kuangalia.

3.Weka picha nzuri (thumbnail) kwenye video zako.
Kitu pekee kinachooneka kwenye video zako kabla watu hawajazifungua ni picha (thumbnail). Hivyo, unapoweka thumbnail zinazovutia na zinazoendana na maudhui ya video zako, basi utaweza kuvutia watazamaji wengi kuangalia video zako.

4.Weka vichwa vya habari vinavyovutia.
Jambo jingine la kuzingatia ni kuwa, Unahitajika kuhakikisha kuwa mada za video zako zinavutia watazamaji wako. Pia hakikisha kuwa unaweka vichwa vya habari vinavyovutia na vinavyojumuisha maneno muhimu yanayoendana na maudhui ya video zako ili kuvutia umakini wa injini za utafutaji.


5.Shirikisha Watazamaji Wako Kupitia Maoni
Jambo la mwisho unalotakiwa kufanya ni kujibu maoni pamoja na maswali ya watazamaji wako. Watazamaji wa YouTube huwa wanapenda kujiunga na chaneli ambazo zinawathamini kwa kujibu maoni yao. Hivyo, mojawapo ya njia rahisi zaidi za kukuza Chaneli yako, ni kwa kuwashirikisha watazamaji wako kwenye video unazoweka kwenye chaneli yako.

Kuanzisha chaneli ya YouTube ambayo watu watapenda kuitazama siyo jambo gumu. Ingawa itachukua muda na juhudi kwa upande wako. Kwa kuzingatia mambo haya matano niliyoyaeleza kwenye makala hii kutakusaidia kukuza chaneli yako.

Nimatumaini yangu umepata maarifa ya kukusaidia kuanzisha chaneli bora ya YouTube. Kama una swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa kunipigia moja kwa moja au kupitia WhatsApp kwa namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp