
Mafanikio Katika maisha yanategemea na jinsi unavyoitumia siku moja uliyopewa ya kuishi. Pia mafanikio ya siku yanategemea ni kwa namna gani umetumia vizuri masaa na dakika kwa siku hiyo. Kumbuka kuwa, muda ni rasilimali ya muhimu sana ambayo kila mtu amepewa kwa usawa. Hivyo, mafanikio yoyote Katika maisha yanategemea kwa kiwango kikubwa na jinsi unavyotumia muda wako. Kumbuka kuwa, haitoshi kuweka malengo ya mwaka, malengo hayo hayataweza kufanikiwa kama hautajua namna ya kuitumia vyema kila siku inayokuja na kupita.
Maana ya mafanikio.
Mafanikio ni neno pana sana na tafsiri yake inatofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Kwa ujumla, mafanikio ni kuweza kufikia malengo uliyokusudia katika maisha yako kama vile: kuhitimu masomo, Kuanzisha biashara, kujenga nyumba, kuongeza kipato chako, kuwa na maisha mazuri na kadhalika. Hivyo, Kila mmoja anaweza kutafsiri neno mafanikio kwa kuhusianisha na malengo aliyojiwekea. Katika makala ya leo, nitakushirikisha mambo 3 muhimu ya kufanya Kila siku Ili uweze kufanikiwa.
Mambo 3 ya kufanya Kila siku ili uweze kufanikiwa.
1.Weka orodha ya mambo unayopaswa kuyakamilisha.
Ili uweze kufanikiwa Katika maisha, ni lazima uwe na orodha ya mambo unayopaswa kuyakamilisha ndani ya siku husika. Orodha hii unatakiwa kuiandika siku moja kabla ili unapoamka asubuhi uwe na ufahamu wa mambo unayopaswa kuyafanya. Hii itakusaidia kutokupoteza muda wako kwenye mambo ambayo si ya msingi. Pia itakusaidia kutokufanya mambo ambayo haukuwa umeyapanga.
2.Tumia Kanuni ya 80/20
Kanuni ya 80/20 ni Kanuni maarufu sana ya mafanikio ambayo Kwa jina jingine inaitwa ‘Pareto Principle‘. Hii ni Kanuni ya muhimu sana ambayo itakusaidia kufanikiwa katika maisha. Kanuni hii inasema kuwa:
“20 percent of your activities will account for 80 percent of your results”.
Maana ya kanuni hii Kwa lugha ya kiswahili ni kuwa: asilimia 20 ya mambo unayoyafanya ndiyo yanayochangia asilimia 80 ya mafanikio yako. Halafu, asilimia 80 ya mambo unayoyafanya yanachangia asilimia 20 tu kwenye mafanikio. Maana yake ni kuwa, ili uweze kufanikiwa ni lazima ufahamu kuwa, kuna mambo machache ya muhimu ambayo ukiyafanya, ndiyo yanayochangia kwa kiwango kikubwa kwenye mafanikio yako. Halafu, mambo mengine yaliyobaki yanachangia sehemu ndogo ya mafanikio yako.
Kwa mujibu wa kanuni hii,unapokuwa umeweka orodha ya mambo ambayo utayafanya Kwa siku, hakikisha unaanza na mambo muhimu yanayochangia kwa kiwango kikubwa kwenye mafanikio yako. Weka nguvu na akili zako zote kwenye kutimiza mambo hayo ya muhimu sana halafu ndio umalizie na mambo ambayo yanachangia Kwa kiwango kidogo kwenye mafanikio yako.
3. Anza na mambo magumu.
Katika orodha ya mambo ya kufanya uliyoweka, unapoamka na kuanza kutekeleza, anza na mambo ambayo ni magumu. Hii ina faida kubwa sana kwani itakusaidia kuweza kuyafanya ukiwa na nguvu na hivyo kufanya Kwa ufanisi. Baada ya kuwa umemaliza kufanya mambo magumu ambayo yanahitaji umakini wa hali ya juu, basi hapo ndio utaweza kuhamia kwenye mambo rahisi.
Kwa leo niishie hapo. Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa kuhusiana na mambo matatu muhimu unayopaswa kuyafanya kila siku ili uweze kufanikiwa. Kama una swali au maoni yoyote kuhusiana na mada hii, usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami moja Kwa moja Kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu tena katika makala ijayo.
- Mbinu Tatu Rahisi Za Mafanikio Zinazopuuzwa. - August 9, 2024
- Jinsi Ya Kugundua Kusudi La Maisha Yako - August 7, 2024
- Kanuni za Kujiwekea Malengo - August 5, 2024
Nice I Love it
Thanks!