Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

Katika maisha, kujitazama nyuma na kutafakari mafanikio uliyoyapata ni jambo muhimu sana. Pia ni vyema kuzingatia changamoto ulizokutana nazo na jinsi zilivyokusaidia kukua. Kitendo cha kufikiria uzoefu wako wa zamani, mafanikio, na mafunzo uliyoyapata, kutaweza kuamua malengo unayotarajia kufikia siku za usoni. Iwe umeweka malengo ya juu zaidi au umelenga kubaki thabiti na malengo yako, unatakiwa kuepuka mambo na tabia fulani ili uweze kufanikiwa. Katika makala hii nitakushirikisha mambo 10 ya kuacha ili ufanikiwe siku za usoni:

Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

1. Visingizio:
Jifunze kuwajibika. Kuwa na malengo na ujikite kufanyia kazi malengo yako bila kuwa na visingizio. Kila kisingizio kinakurudisha nyuma kufikia lengo lako.

2. Kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja:
Ingawa inaweza kuonekana kuwa kama suluhisho la ufanisi, kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja kunaweza kuharibu malengo yako. Fikiria kufanya kazi moja kwa wakati mmoja.

3.Kusema ndiyo kwa mambo yasiyosaidia malengo yako:
Mara nyingine tunajisikia lazima tuseme ndiyo. Lakini kusema ndiyo kwa mambo ambayo hayasaidii malengo yako kunaweza kukurudisha nyuma. Jifunze kusema hapana kwa mambo yasiyo na maana ambayo hayachangii kwenye mafanikio yako.

4. Epuka watu wenye sumu:
Kuna wakati utakutana na watu wasio na nia njema na mafanikio yako. Ikiwa hawakusaidii kufikia malengo yako, waache. Kuacha uhusiano na watu wenye mawazo hasi kunaweza kuwa kugumu, lakini kutakusaidia kufanikiwa baadaye.

5. Muda wa kutumia kwenye mitandao ya kijamii:
Kwa wastani, mtu hutumia dakika 145 kwa siku, zaidi ya masaa 2 kwenye mitandao ya kijamii. Kudhibiti muda wako kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kukuepushia kupoteza muda na badala yake kufanya vitu vingine vyenye tija.

6.Kutothamini kile ulichonacho sasa:
Thamini vitu ulivyonavyo sasa. Kudharau vitu ulivyonavyo kunaweza kuzuia kufikia malengo yako. Kuwa na shukrani kwa kila unachokuwa nacho katika maisha yako. Kujifunza kushukuru imegundulika kuwa kunaimarisha mtazamo chanya na afya ya akili kwa ujumla. Hata kama kuna nyakati ambazo hauna furaha, unapothamini mafanikio yako unaongeza motisha ya kupiga hatua zaidi kuelekea kwenye mafanikio yako. Hivyo, unapaswa kuacha tabia hii ili uweze kufanikiwa.

7.Kutafuta idhini kutoka kwa watu wengine.
Ikiwa unangoja mtu akuruhusu kufanikiwa, utangoja milele. Usisubiri mtu akwambie unaweza kufanya nini. Badala yake, onyesha uwezo wako. Jitwike jukumu la maisha yako na malengo yako wewe mwenyewe. Jiruhusu kufanikiwa.

8. Uvivu.
Kama vile kutoa visingizio, kuchelewesha kazi pia kunazuia kufikia malengo yetu. Badala ya kusubiri kufanya kazi yako hadi dakika ya mwisho, au kuendelea kuahirisha, jichukulie kuwajibika na kufanya kazi kwa bidii.Tunaona mafanikio tunapochukua hatua na kufanya jambo.

9.Kuamini malengo yako ni makubwa au madogo sana.
Malengo yako ni tofauti kabisa na ya mtu mwingine, hivyo unapaswa kuacha kulinganisha malengo. Badala yake, jikite katika jinsi unavyoweza kufikia malengo yako. Usipoteze muda kwa kufikiria sana au kuchambua mambo kama vile ukubwa au udongo wa malengo yako. Anza tu kuyatimiza.

10. Kulinganisha maisha yako na ya wengine.
Kama vile malengo yanavyotofautiana na ya mtu mwingine, maisha yako pia ni tofauti kabisa na ya mtu mwingine.

Rais Theodore Roosevelt aliwahi kusema, Kujilinganisha na wengine ni mwizi wa furaha. Tunapojilinganisha na wengine, tunajihisi duni na tusiofaa. Tunapogundua kuwa tunaweza vya kutosha na tuna njia za kufikia malengo yetu, hatutajisikia vibaya kuhusu safari yetu ya mafanikio. Tutagundua kuwa kujilinganisha na wengine kunatuzuia tu kufikia safari yetu.

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa kuhusu mambo 10 ya kuacha ili ufanikiwe siku za usoni. Kama una swali au maoni usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

    Kingi Kigongo
    Ungana nae
    Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    error

    Enjoy this blog? Please spread the word :)

    Follow by Email
    WhatsApp