
Unapoanzisha chaneli yako mpya ya YouTube, pengine tayari una mambo machache unayohitaji kuyafanya ili uweze kufanikiwa. Lakini, kama ilivyo muhimu kujua mambo unayopaswa kufanya, ni muhimu pia kujua ni makosa gani ya kuepuka. Katika makala ya leo nitakushirikisha makosa manne ambayo unapaswa kuyaepuka unapoanzisha chaneli yako ya YouTube.
Kosa #1 – Kupuuzia kujibu maoni na maswali ya watazamaji wako.
Watazamaji wako ndiyo sababu pekee inayokufanya uwe na chaneli ya YouTube. Bila wao, huwezi kupata mafanikio. Ikiwa watazamaji wako watakuuliza maswali au kukuachia maoni katika sehemu ya maoni ya video zako, basi unahitajika kuwajibu mapema iwezekanavyo. Unahitajika kuhakikisha kuwa unajibu kwa ufasaha majibu yanayoendana na swali lililoulizwa. Kadiri unavyojihusisha na watazamaji wako, ndivyo watakavyohisi wameunganishwa zaidi na biashara yako.
Kosa #2 – Kutoboresha Vichwa vya habari vya Video Zako
Ikiwa hutajumuisha maneno muhimu yanayoendana na maudhui ya video zako kwenye vichwa vya habari vya video zako, watazamaji wako hawataweza kukupata kwa urahisi katika matokeo ya utafutaji wanapokuwa wametafuta video zako mtandaoni. Unatakiwa kuhakikisha kuwa, unaandaa video za kipekee na zinazovutia ambazo zinajumuisha kwenye vichwa vya habari maneno muhimu ili video zako ziweze kuonekana juu zaidi katika viwango vya utafutaji.
Kosa #3 – Kutotangaza video zako.
Ukishindwa kutangaza video zako, inakuwa vigumu zaidi kwa watazamaji wako kutambua video ambazo umetayarisha. Ili uweze kupata watazamaji wengi kwenye video zako, unahitajika kushea video zako kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, telegram na kadhalika. Pia unaweza kushare video zako kwenye blog au tovuti yako kama utakuwa nayo. Pia katika kila video unayoweka kwenye chaneli yako, hakikisha unaweka logo inayowakilisha utambulisho wako (brand). Usipoweka utambulisho (brand) kwenye video zako, itakuwa ni vigumu kukuza jina la chaneli yako pamoja na biashara au huduma unayotoa.
Kosa #4 – Kutokuweka picha (thumbnail) kwenye video zako.
YouTube huruhusu kuweka picha inayotambulisha maudhui ya video yako (thumbnail). Picha hii ndiyo itaayoonekana karibu na kichwa cha habari cha video yako katika matokeo ya utafutaji. Usipochagua picha yako mwenyewe, YouTube itaipa video yako picha ambayo haitaendana na maudhui uliyoyakusudia ya video yako. Hivyo, ili kuwashirikisha watazamaji wako vyema zaidi, unahitajika kuhakikisha kuwa unaweka picha yako maalum ambayo inawakilisha vyema maudhui ya video yako.
Unapoanzisha chaneli yako ya YouTube, haya ni mambo manne ambayo unapaswa kuyaepuka. Kwa kuzingatia mambo haya niliyoyaeleza katika makala hii utakuwa kwenye njia nzuri ya kukuza chaneli yako ya YouTube na kupata mafanikio makubwa kwenye biashara yako.
Kwa leo niishie hapo. Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuwa na chaneli ya YouTube yenye mafanikio. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa kupiga au WhatsApp 0752 081669. Karibu tena kwenye makala zinazokuja.
- Mbinu Tatu Rahisi Za Mafanikio Zinazopuuzwa. - August 9, 2024
- Jinsi Ya Kugundua Kusudi La Maisha Yako - August 7, 2024
- Kanuni za Kujiwekea Malengo - August 5, 2024