Sababu 10 Za Kuanzisha Blog Yako.

Sababu 10 Za Kuanzisha Blog Yako.

Kama unafikiria kuanzisha blog lakini huna uhakika kama uko sahihi na uamuzi wako, usiwe na wasiwasi kwani makala hii inakwenda kukupatia majibu yote ambayo yamekuwa yakikutatiza. Katika makala hii nitakushirikisha sababu 10 za kuanzisha blog. Basi karibu tuendelee .

Je Ninapaswa Kuanzisha Blog? Sababu 9 kwa nini unapaswa kuanzisha na kuwa na Blog yako mwenyewe. (na maswali 7 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog)

  1. Sababu 6 za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe.
  2. Sababu 3 ambazo sio za msingi za wewe kuanzisha blog (Kama una sababu hizi usianzishe blog)
  3. Maswali 7 ya muhimu unayopaswa kujiuliza kabla ya kuamua kuanzisha blog.
  4. Sasa fanya maamuzi.

Katika Makala hii tunaenda kuangalia maswali muhimu na ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha blog. Lakini kabla hatujaendelea na maswali hayo, hebu kwanza tuangalie sababu za msingi za wewe kuwa na blog yako mwnyewe.

Tutaangalia sababu 6 za msingi za wewe kuwa na blog yako mwenyewe. Lakini pia tutaangalia sababu 4 ambazo sio za msingi.

 Sasa hebu tuendelee.

1. Sababu 6 za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe.

Kama una miongoni mwa sababu hizi au nzuri zaidi ya hizi za wewe kuanzisha blog , basi ukianzisha blog utafanikiwa sana.

Sababu ya msingi #1: Unahitaji kuandika na kufundisha watu kuhusiana na mada unayoipenda.

Kama una ujuzi ,au mada unayoipenda na unahitaji kuwashirikisha watu ujuzi wako, ukiamua kuanzisha blog na kufundisha watu ujuzi wako unaoupenda, utafanikiwa sana kwenye kazi yako ya blog.

Sababu ya Msingi #2: Unahitaji kuanzisha na kujenga Biashara kupitia mtandao wa internet.

Inawezekana unahitaji kuanzisha blog ukiwa na sababu ya kuanzisha biashara yako na kuitangaza kuipitia mtandao wa internet. Au inawezekana tayari una biashara na kupitia kuanzisha blog,unahitaji kutangaza biashara yako ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi.

Pia kupitia blog unaweza kujiajiri na kutengeneza kipato.Kwa mfano,unaweza kuuza maarifa yako mtandaoni kwa kuuza kozi mbalimbali, vitabu pepe (ebooks) au kuuza ushauri wako wa kitaalamu kwa watu.

Sababu ya msingi #3: Unahitaji kutengeneza Brand yako.

Blog ni njia nzuri sana ya kukuza jina lako na kulifanya litambulike na kuwa maarufu kwa watu. Hivyo, kama unataka watu na jamii kwa ujumla wakutambue, anzisha blog na uwasaidie watu kutatua matatizo yao kupitia kuandika makala kwenye blog yako.

Sababu ya Msingi #4: Unahitaji kutatua changamoto zinazoikabili jamii na kufanya maisha ya watu yabadilike.

Kama utaanzisha blog ili kutatua matatizo ya watu utafanikiwa sana kwani watu wana changamoto nyingi zinazowakabili na wanahitaji mtu atakayeweza kutatua changamoto zao.Hivyo kama unahitaji kuanzisha blog ili kuweza kubadilisha maisha ya watu,nakutia moyo songa mbele kwani utafanikiwa sana katika kazi yako.

Sababu ya msingi #5: Unahitaji kujiajiri na kujipatia kipato kupitia maarifa,ujuzi au hobby yako.

Pia sababu nyingine unaweza kuanzisha blog ili kujiajiri na kutumia ujuzi ulionao kufundisha watu na kujipatia kipato mtandaoni.

Soma:Njia 9 za kutengeneza kipato kupitia blog.

Sababu ya Msingi#6: Unafurahia Kujifunza Vitu Vipya Kila Siku.

Unapoanzisha blog umeanza safari ndefu ya uandishi. Hivyo utatakiwa ujifunze vitu vipya kila siku ili uweze kubobea kwenye mada unayofundisha.

2. Sababu 3 ambazo sio za msingi za wewe kuanzisha blog(Kama una sababu hizi usianzishe blog)

Pamoja na kuwa sababu nilizozielezea hapo juu ni za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe, Sababu zifuatazo sio za msingi. Hivyo, kama una sababu hizi ninazoenda kuzielezea sasa au zinazofanana na hizi, usianzishe blog kwani itakuwa vigumu sana kwako kufanikiwa.

Sababu isiyokuwa ya msingi #1: Unahitaji kutengeneza Pesa Haraka.

Kama unahitaji kuwa n blog kwa lengo la kutengeneza pesa haraka ,basi unaweza kushindwa kufikia malengo yako. Hii ni kwa sababu ili uweze kutengeneza pesa kupitia blog unapaswa kujipa muda kuijenga blog yako kwa kuweka makala mara kwa mara ili ujenge mahusiano na wasomaji wako. Hivyo, kama utaweka nguvu katika kuandika makala za kuelimisha jamii, watu watakupenda na hivyo watakuwa tayari utakapoamua kuwauzia bidhaa au huduma unayotoa.

Sababu isiyokuwa ya msingi #2: Huna kitu cha kuelimisha bali unahitaji kuwa unaweka mambo maisha yako binafsi mtandaoni.

Kama unahitaji kutengeneza kipato kupitia blog kuandika maisha yako binafsi haitakusaidia kukuza blog yako. Kumbuka kuwa watu huwa wanaingia mtandaoni kujifunza maarifa ambayo yatatatua changamoto zao.Hivyo ukianzisha blog ili kuweka mambo yako binafsi hutaweza kukuza blog yako.

Hata hivyo, unaweza kuanzisha blog kutokana na hobby yako ambayo unahisi itakuwa msaada kwa watu kutatua changamoto zao.

Sababu isiyokuwa ya msingi  #3: Huwa unasoma blog nyingi na unaona ni fahari na wewe kumiliki blog.

Inawezekana ukaona kuwa kwa kuwa unapenda kusoma Makala kwenye blog mbalimbali na wewe ukafikiria kuwa na blog yako mwenyewe. Japokuwa sababu hii sio mbaya ,lakini sio sababu ya kutosha kwa wewe kuanzisha blog. Wazo hili ni sawa na la mtu anayependa kuangalia movie halafu akatamani na yeye awe muigizaji. Kuanzisha blog kunahitaji kujitoa kiasi cha kutosha kusoma na kuandika Makala mara kwa mara kama unataka kufanikiwa kwenye kazi hii. Hivyo kusema tu kuwa kwa kuwa unapenda kusoma blog mbalimbali na wewe unahitaji kuwa na blog yako mwenyewe haitoshi kukufanya na wewe uanzishe blog. Kama unataka kuanzisha blog  unapaswa kutafakari Zaidi na uwe na sababu za msingi kama nilizoziainisha hapo kabla.

Hatari nyingine ya kuanzisha blog kwa sababu tu unapenda kusoma blog zingine ni kuwa , kwa kuwa utakuwa huna maandalizi na sababu za msingi za wewe kuwa na blog utaishia kunakiri (copy and paste) blog zile unazopenda kuzisoma.

Maswali 7 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog.

Sasa tayari umefikiria kwa kina na umeona kuwa una sababu za msingi za kuanzisha blog. Je uendelee mbele au unaenda kupoteza muda wako bure?

Hapa nimekuwekea Maswali 8 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog.

Swali #1: Je umechagua mada unayoipenda?

Unapokuwa umechagua mada unayoipenda, hiyo ni hatua ya kwanza kuelekea mafanikio. Hii ni kwa sababu unapoanzisha blog, utaendelea kuweka Makala kwa miaka mingi ijayo. Hivyo ukiwa umechagua mada unayoipenda , utakuwa unafurahia kuandika mara kwa mara na kusoma zaidi kujiongezea ujuzi kwenye mada yako.

Swali #2: Je una ujuzi wa kutumia computer na mtandao wa internet?

Hapa sizungumzii kuwa uwe umesoma sana kuhusiana na mambo ya computer,ninachosema ni ule uelewa tu wa msingi wa jinsi ya kutumia internet.

Swali #3: Je utakuwa na muda na nguvu ya kutosha kuandika Makala?

Jambo jingine la msingi unalopaswa kujiuliza ni kuwa ,utakuwa na muda na nguvu kuendesha blog yako? Kumbuka kuwa ili uwe na blog yenye mafanikio, unapaswa uwe unaweka Makala mara kwa mara. Hivyo unapaswa ujiulize na uwe mkweli kwenye nafsi yako kama utaweza kuwa na muda wa kuandika Makala za blog yako.

Swali  #4: Jinsi gani utatengeneza kipato (pesa) kupitia blog yako?

Jambo jingine la msingi unalopaswa kulifikiria ni kuwa , ni jinsi gani utatengeneza kipato kupitia blog yako.Je utakuwa ukiuza kozi mbalimbali ulizoandaa,vitabu pepe au utakuwa ukitoa huduma ya ushauri na watu wakakulipa? Au utatumia blog yako kuuza bidhaa zako mwenyewe au kutangaza bidhaa za makampuni mengine na wewe ukapata gawio (commission)? Kimsingi kuna njia nyingi sana ambazo unaweza kuzitumia kwenye blog yako kupata kipato. Hivyo unapaswa kufikiria jinsi ambavyo blog yako itakuingizia kipato toka siku ya kwanza unapoianzisha.

Swali#5: Utakuwa ukiandaa Makala za aina gani?

Kwa kuwa Makala ndio msingi wa blog, hivyo unapaswa kufikiria Makala zako zitakuwa za aina gani. Je ni kurekodi video au kuandika Makala? Na Je utakuwa ukiandika Makala zenye urefu gani?

Hivyo, unapaswa kujiuliza jambo hili mapema kabla ya kuanzisha blog yako.

Swali #6: Utapimaje maendeleo ya blog yako?

Kuna njia nyingi za kupima maendeleo ya blog yako.

Kama lengo lako si kutengeneza pesa bali ni kuelimisha jamii, unaweza kupima maendeleo ya blog yako kwa kuangalia ongezeko la idadi ya watembeleaji kwenye blog yako na ongezeko la email za watu waliojiunga na blog yako.

Kama lengo lako ni kujiajiri na kutengeneza kipato kupitia blog utapima maendeleo ya blog yako kwa kuangalia ni kiasi gani cha pesa unatakiwa uwe umepata kupitia blog kwa kipindi ulichojiwekea. Inaweza kuwa mwezi au mwaka.

Swali #7: Utakuwa ukiweka Makala mpya kila baada ya muda gani?

Kabla ya kuanzisha blog unatakiwa pia kujua ratiba yako ambayo utaitumia kuweka Makala kwenye blog yako. Inaweza kuwa mara moja kila siku au mara moja kwa juma n.k . Hii itawafanya wasomaji wako kujua wakati maalumu ambao wakiingia kwenye blog yako watapata maarifa mapya.

Sasa ni wakati wako wa kuamua,Je unahitaji kuanzisha blog?

Katika Makala hii nimejitahidi kuelezea faida za kuanzisha blog na kumiliki blog yako mwenyewe. Pia nimezungumzia maswali ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla hujaingia kwenye kazi hii.

Kumbuka kuwa , kama unaweza kupata masaa machache tu kwa juma na ukawa na mada unayopenda kufundisha, hakuna kitakachokuzuia wewe kuanzisha na kujipatia kipato kupitia blog. Songa mbele!

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuanzisha blog .Kama una maoni yoyote, usisite kudondosha maoni yako hapa chini! Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kama unahitaji ushauri, kuhusiana na jinsi ya kujiajiri na kutengeneza pesa mtandaoni kwa simu namba 0752081669.

Asante na karibu katika makala ijayo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

6 Replies to “Sababu 10 Za Kuanzisha Blog Yako.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp