Kanuni Ya Mafanikio ‘Choma Meli Zako Zote’

Kanuni ya Mafanikio

Hernan Cortes, kamanda wa Hispania alikuja na Kanuni ya Mafanikio moja inayojulikana kama “Choma Meli Zako Zote'”. Kanuni hii inatokana na kazi aliyopewa ya kwenda kuvamia kisiwa kilichokuwa kinajulikana Kwa jina la Veracruz nchini Mexico mwaka 1519.

Kitu alichokifanya ni kuwa, alichukua makamanda 500 pamoja na Meli 11 za kivita na akawapandisha kwenda kuvamia kwenye kile kisiwa. Alipofika kwenye kile kisiwa, akaamuru makamanda pamoja na mabaharia wote washuke. Baada ya wote kuwa wameshuka, akaagiza Meli Zote zichomwe moto. Wakati Meli zilipokuwa zinaungua, akawauliza makamanda pamoja na mabaharia ” mnaona nini?” wakamjibu “Tunaona moto pamoja na moshi, meli zetu zinaungua”. Akawaambia ” Hivyo basi, hatuna uchaguzi zaidi kwenye vita hii. Ni lazima tuchague moja kati ya mambo haya mawili: Moja, tuamue kufa tushindwe vita, au pili, tupigane tushinde vita ambayo tumeianza.”

Unajua nini kilitokea? Ingawa walikuwa ni wachache ukilinganisha na jeshi ambalo walilikuta pale kisiwani, walishinda ile vita. Hapa ndipo tunapata Kanuni ya kuchoma meli zako zote. Kanuni ya kuchoma meli zako zote inamaanisha, ili uweze kufanikiwa kwenye malengo yako uliyojiwekea, jitahidi kufanya jambo na kulifuatilia kwa kutoa kila kitu ulichonacho. Hata Biblia inasema:
“Lolote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako, kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe” Mhubiri 9:10.
Maana yake ni kuwa, Katika maisha, ili uweze kufanikiwa kwenye jambo lolote ni lazima uwekeze nguvu zako zote na kila kitu ulichonacho. Kutokana na kanuni hii ya ‘choma meli zako zote’, kuna mambo matatu ambayo lazima uyazingatie:

  1. Lazima uamue kuhusu hatma ya maisha yako (Your future)

Lazima uamue kuhusu hatma ya maisha yako (your future). Usiruhusu maisha yako yaendeshwe na hali zinazokuzunguka au na matokeo ambayo yanaambatana na maisha yako. Hivyo, lazima uamue kuhusiana na kazi uliyonayo, kama ni mahusiano yako hauyafurahii, amua leo kuboresha mahusiano yako. Hivyo, haupaswi kuona kuwa, hali yako uliyonayo hauna mamlaka nayo na kwamba hauwezi kufanya kitu chochote kuboresha hali yako. Hivyo, jambo la kwanza kwenye Kanuni hii ya kuchoma meli zako zote ni , amua kuhusiana na kesho yako.

2. Achilia na usahau mambo yaliyopita.

Moja ya vitu ambavyo vinawafanya watu wengi washindwe kufanikiwa Katika maisha yao ni Kwa sababu wameruhusu mambo yao yaliyopita yaendeshwe maisha yao. Pengine kuna mambo ya kukatisha tamaa uliyopitia huko nyuma, pengine kuna maumivu uliyoyapata kutokana na mahusiano yako au uzoefu fulani unaoumiza ulioupitia. Mambo haya yote yamekusababisha mpaka sasa ukijiangalia unajiona kuwa ni mtu ambaye hauwezi kusonga mbele au kuchukua hatua na kufikia kule unakotaka kwenda. Hivyo, jambo la pili, usiruhusu mambo yaliyopita yaendelee kutembea na wewe. Hesabu mambo yaliyopita kuwa yalikuwa ni mambo ya kukufundisha, kukukomaza na kufanya uwe bora zaidi leo.

3. Tumia Kila kitu ulichonacho kufuatilia ndoto ambayo umechagua.

Kama alivyofanya Hernan Cortes ni kwamba, angeachia zile meli, angekuwa ameachia upenyo wa yeye kurudi atakapokuwa amezidiwa na maadui. Lakini Kwa sababu alichoma meli zote, kilichotokea ni kwamba, alihakikisha kwamba hakuna upenyo wa kukimbia. Hivyo, Ili ufanikiwe, toa kila kitu ulichonacho kupigania ndoto zako. Kama uko kwenye biashara, fanya kazi Kwa bidii, tumia nguvu zako, tumia akili zako zote. Kama uko kazini umeajiriwa na ndicho ulichokichagua, hakikisha unatumia kila kitu ulichonacho kufanya ambacho umekichagua. Tatizo la watu wengi ni kwamba, hawaweki kila kitu walichonacho Ili kufanikiwa.
Nimatumaini yangu kuwa umejifunza hizi hatua tatu kwenye kanuni ya mafanikio ya kuchoma meli zako zote kuweza kufikia ndoto zako. Kumbuka kuwa, siku zote hauwezi kufanikiwa kama ulichoamua kufanya haukifanyi Kwa nguvu zako zote. Je, wewe una ndoto gani? Nitafurahi sana kama utaniandikia hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami Kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala ijayo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

7 Replies to “Kanuni Ya Mafanikio ‘Choma Meli Zako Zote’”

  1. Asante Kwa SoMo zuri sana, nimepata ujumbe kuwa Ili uweze kufanikiwa unatakiwa kujitoa Kwa nguvu zako na akili zako zote huku ukimshirikisha Mungu.
    Ubarikiwe brother.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp