Jinsi Ya Kuwa Mtu Wa Vitendo: Vidokezo Vya Usimamizi Wa Muda.

Jinsi Ya Kuwa Mtu Wa Vitendo: Vidokezo Vya Usimamizi Wa Muda.

Tunaishi katika kipindi ambacho kuna fursa na uwezekano zaidi wa wewe kufikia malengo yako zaidi kuliko hapo awali. Kwa kweli, kuna mambo mengi mazuri ambayo unaweza kuyafanya Ili uweze kufanikiwa maishani mwako. Ikiwa wewe ni kama watu wengi leo, umekuwa ukilemewa na mambo mengi ya kufanya kutokana na muda kuwa mdogo sana, unapaswa kutumia muda wako vizuri ili uweze kutimiza malengo yako. Katika makala hii nitakushirikisha jinsi ya kuwa mtu wa vitendo ili uweze kutimiza malengo yako katika maisha.

Jinsi Ya Kuwa Mtu Wa Vitendo.

Kwanza, unahitaji kuchagua.
Kuchagua ni muhimu ili kukuza tabia nzuri ya mafanikio. Uwezo wako wa kuchagua kazi yako ya muhimu zaidi kwa kila wakati, ili kuanza kazi hiyo, na kuifanya haraka na kwa ubora huleta mafanikio makubwa kuliko ujuzi mwingine wowote unaoweza kuukuza. Mtu wa kawaida mwenye mazoea ya kufanya kazi muhimu na kuikamilisha kwa haraka atakuwa na mafanikio makubwa kuliko mtu mwenye uwezo mkubwa na akili timamu ambaye anazungumza sana na kupanga mipango mizuri lakini haitekelezi.

Pili, unahitajika kuweka vipaumbele.
Mafanikio yako katika maisha yataamuliwa na aina ya tabia ambazo unakuwa umezijenga kwenye maisha yako. Tabia ya kuweka vipaumbele na kuendelea na kazi yako muhimu zaidi ni ujuzi unaopaswa kuuweka kwenye vitendo na kuudumisha.

Kwa hiyo, unaweza kujifunza tabia hii kupitia mazoezi ya kurudia tena na tena hadi inapokuwa imekazwa kwenye akili yako na kuwa sehemu ya kudumu ya tabia yako. Mara tu inapokuwa tabia, inakuwa moja kwa moja na rahisi kufanya. Kupitia usimamizi wa muda, tabia ya kuanza na kukamilisha kazi muhimu ina malipo ya haraka na endelevu.

Umeundwa kiakili na kihisia kwa njia ambayo kukamilika kwa kazi hukupa hisia chanya. Inakufanya uwe na furaha. Inakufanya ujisikie mshindi.

Wakati wowote unapokamilisha kazi kubwa au yenye umuhimu, unahisi kuongezeka kwa nguvu, shauku, na kujistahi. Umuhimu zaidi wa kazi iliyokamilishwa, unakufanya ujihisi furaha, ujasiri zaidi, na nguvu ndani yako. Kukamilika kwa kazi muhimu huchochea kutolewa kwa endorphins kwenye ubongo wako.

Endorphins hizi hukupa kiwango cha juu cha nguvu za asili. Endorphin ambayo inafuatilia kukamilishwa kwa mafanikio kwenye kazi yoyote hukufanya ujisikie chanya zaidi, mwenye utu, mbunifu na mwenye kujiamini.

Kumbuka kuna mambo matatu muhimu unayopaswa kuyafanyia mazoezi ili uweze kuwa mtu wa vitendo na hivyo kufanikiwa kwenye malengo yako. Mambo hayo ni uamuzi, nidhamu, na dhamira.

Kwanza, lazima ufanye uamuzi wa kukuza tabia ya kuwa mtu anayezingatia vitendo.

Pili, kuwa na nidhamu binafsi ili kufanya mazoezi ya kanuni unazojifunza kwa kuzirudia tena na tena hadi iwe ni mazoea yako.

Na tatu, rudisha kila kitu unachofanya kwenye dhamira yako ili iwe ni tabia na kuwa sehemu ya kudumu ya utu wako.

Jione kuwa ni aina ya mtu ambaye anafanya kazi muhimu kwa haraka na kwa kupitia usimamizi mzuri wa wakati. Picha yako ya kiakili ina athari kubwa kwenye tabia yako. Jione kama mtu unayekusudia kuwa hivyo katika siku zijazo.

Taswira yako, jinsi unavyojiona kwa ndani, kwa kiasi kikubwa huamua utendaji wako wa nje. Uboreshaji wote katika maisha yako ya nje huanza na uboreshaji wa picha zako za akili ndani. Una uwezo usio na kikomo wa kujifunza na kukuza ujuzi mpya, tabia, na uwezo.

Unapojizoeza kupitia marudio na mazoezi ya kushinda kuchelewesha na kukamilisha kazi zako muhimu zaidi haraka, utasonga mbele kwenye njia ya haraka katika maisha na taaluma yako. Sasa ningependa kusikia kutoka kwako. Swali langu la leo ni, je, unajionaje? Acha maoni hapa chini na nitahakikisha kukufuata.

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuwa mtu wa vitendo. Ikiwa umefurahia makala hii na unahisi kuwa imekuwa ni ya thamani kwako, usisite kuwashirikisha marafiki zako. Pia kama una swali lolote usisite kuandika hapa chini. Unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp