Jinsi Ya Kutambua Kusudi La Maisha Yako

Jinsi kugundua Kusudi la Maisha Yako

Katika maisha, Mungu amemuumba kila mwanadamu na kumleta duniani kwa kusudi maalumu. Hivyo Mungu amempatia kila mwanadamu uwezo mkubwa ndani yake, kila mtu kwa aina yake ili aweze kutimiza kusudi lake la kuwa duniani. Hata wewe, Mungu ameruhusu uwepo duniani kwa kusudi maalumu. Ukigundua kusudi la maisha yako, utaweza kufanya mambo makubwa sana. Kwa bahati mbaya sana, watu wengi wanazaliwa mpaka wanakufa bila kutambua kusudi la maisha yao na hivyo kushindwa kutumia uwezo mkubwa ambao Mungu ameuweka ndani yao ambao kama wangeutumia wangeweza kufanya mambo makubwa sana Duniani na wangekuwa mbaraka mkubwa kwa watu wengine. Katika Makala ya leo nitakushirikisha jinsi ya kutambua kusudi la maisha yako ili uweze kufanikiwa kufanya mambo makubwa.
Jinsi ya kutambua kusudi la maisha yako uweze kufanikiwa.
1. Chunguza nguvu (umahili) wako.
Ili uweze kugundua kusudi la maisha yako, njia ya kwanza ni kuchunguza kwenye uwezo wako wa ndani. Hebu jichunguze, ni vitu gani ambavyo ukivifanya, unavifanya kwa ubora wa hali ya juu. Kwa mfano inawezekana ukawa una uwezo wa kuongea vizuri mbele za watu, kuimba, kucheza mpira, kuandika na kadhalika. Kutambua uwezo ulio nao ni hatua kubwa sana ya kutambua kusudi ambalo Mungu amekuleta Duniani. Hii itakusaidia kuwekeza nguvu kubwa kwenye eneo ambalo una umahili wa kutosha na kukufanya uweze kufanya mambo makubwa na ya kushangaza. Kumbuka kuwa kila uwezo au umahili ulionao una uwezo kabisa wa kuubadilisha na ukawa ni chanzo cha kuuingizia kipato.
2. Ongea na watu wa karibu wakuambie uwezo wako upo kwenye maeneo gani.
Njia nyingine ya kutambua kusudi la maisha yako ni kuongea na watu wako wa karibu. Hawa wanaweza kuwa ni wale watu unaowaamini kuwa watakuambia ukweli wa jinsi ulivyo. Mfano: marafiki wako wa karibu, mke au mme wako, wazazi na kadhalika. Waulize maswali wakuambie ni kitu gani unapokuwa unakifanya, unaonekana umekifanya vizuri sana na watu huwa wanakifurahia. Kusanya majibu ambayo watakuwa wamekupatia. Majibu uliyoyapata, yatakusaidia kugundua uwezo wako na hivyo kuweza kufahamu kusudi la maisha yako.
3. Fikiria ni vitu gani ulivyowahi kuvifanya na watu wakavifurahia (Past experience).
Njia nyingine ambayo unaweza kugundua kusudi la maisha yako ni kwa kuangalia uzoefu wako wa nyuma (past experience). Hapa unaangalia mambo yote ambayo uliwahi kuyafanya na ukayafurahia na pia watu wakakupongeza kuwa umefanya vizuri. Mfano, inawezekana kuna siku uliwahi kusimama mbele ya watu na ukaongea vizuri, baada ya kumaliza kuongea watu wakakupongeza sana kuwa umeongea vizuri sana. Hii ni dalili nzuri kuwa una uwezo mkubwa wa kuongea mbele ya watu kwa sababu si kila mtu anaweza kusimama na akaongea mbele za watu vizuri. Huo ulikuwa ni mfano tu, sasa unaweza kufikiria mambo yote uliyowahi kuyafanya na watu wakakupongeza.
Baada ya kutumia njia nilizokuelezea hapo juu, sasa unaweza kujua ni mambo gani una uwezo kubwa wa kuyafanya. Kwa kuangalia mambo hayo, sasa unaweza kufikiria ni kazi au shughuli gani unaweza kuifanya ambayo inahusiana na uwezo ulio nao. Kazi utakayoifanya ndilo litakuwa ni kusudi lako la maisha kwa sababu itakuwa ni kazi ambayo utakuwa unaifurahia na ni kazi ambayo inakuwezesha kutumia uwezo wote ambao Mungu ameuweka ndani yako. Hivyo, utafanya kazi kwa viwango vya juu na Kufanikiwa sana.
Kwa leo niishie hapo. Kama una maoni yoyote kuhusiana na mada ya leo, usisite kuweka maoni au swali lolote, usisite kuweka hapo chini. Pia kama unahitaji ushauri wowote, usisite kuwasiliana name moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu tena katika Makala zinazokuja.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

One Reply to “Jinsi Ya Kutambua Kusudi La Maisha Yako”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp