Jinsi ya Kujenga Ujasiri Usiotetereka

Kujenga ujasiri.

Je, kungekuwa na tofauti gani katika maisha yako ikiwa ungekuwa na ujasiri usiotikisika katika uwezo wako wa kufanikiwa katika kila kitu ambacho unakiwaza kwenye akili yako? Msichana mmoja alimwandikia Brian Tracy akimwambia kwamba maisha yake yote yalikuwa yamebadilika kabisa tangu alipomsikia akiuliza swali, “Ni jambo gani kubwa ambalo ungethubutu kulifikiria na kulifanya ikiwa ungejua huwezi kushindwa?” Aliandika kwamba hadi wakati huo hili lilikuwa ni swali ambalo hakuwahi kulifikiria katika maisha yake. Baada ya kusikia swali hilo la Brian Tracy aligundua kuwa jambo kuu lililomtenganisha na matumaini na ndoto zake ni imani katika uwezo wake wa kuzifanikisha.

Wengi wetu tuko hivyo kwa sehemu kubwa ya maisha yetu. Kuna mambo mengi ambayo tunataka kuwa nayo na kuyafanya, lakini tunajizuia. Hatuna uhakika wa kufanikiwa kwa sababu hatuna ujasiri wa kutosha kutoka kwa imani katika mwelekeo wa ndoto zetu.

Hebu fikiria, ingekuwa na tofauti gani katika maisha yako ikiwa ungekuwa na imani isiyotikisika kabisa katika uwezo wako wa kufikia jambo lolote unaloliwaza akilini mwako? Je, ungetaka, kutamani na kutumaini nini? Ungethubutu kuota nini ikiwa unajiamini kwa imani kubwa kiasi kwamba huna hofu ya kushindwa hata kidogo? Jambo kuu ni kuwa mwaminifu kwako mwenyewe, kuwa mwaminifu kwa yaliyo bora zaidi yaliyo ndani yako, na kuishi maisha yako kulingana na maadili na matarajio yako ya juu. Chukua muda kufikiria wewe ni nani na unaamini nini na ni nini muhimu kwako.

Kuwa na ujasiri wa kujikubali jinsi ulivyo, si vile unavyoweza kuwa au jinsi mtu mwingine anavyofikiri unapaswa kuwa. Zingatia kuwa, wewe ni mtu wa thamani sana. Kuwa mwaminifu kwako mwenyewe inamaanisha kujua kile unachotaka na kuwa na mpango wa kukifanikisha. Kujiamini kunakodumu kunatokana na kujua kabisa kwamba unao uwezo wa kutoka hapo ulipo kwenda popote unapotaka kwenda.

Uko nyuma ya gurudumu la maisha yako. Wewe ndiye mbunifu wa hatima yako na bwana wa hatima yako. Tenda kana kwamba haiwezekani kushindwa.

Fanya kana kwamba tayari una kiwango cha juu cha ujasiri na endelea kujiuliza, ni jambo gani kubwa ambalo ningethubutu kulifikiria na kulifanya nikijua siwezi kushindwa? Chochote unachokiwaza kwenye jibu lako, unaweza kukipata ikiwa unajiamini kutoka na kukipokea. Hapa kuna hatua tatu unazoweza kuchukua mara moja ili Kujenga Kujiamini Kusikotetereka.

Kwanza, amua kuchukua hatua kwa imani katika mwelekeo wa ndoto zako. Fanya tu, usiwaze kushindwa.

Pili, jiulize, “ni kitu gani kikubwa ambacho ningethubutu kukiota na kukifanya nikijua siwezi kushindwa?”

Tatu, kuwa mwaminifu kwako mwenyewe, na uanze kuchukua hatua. Usiweke visingizio vingi vya kushindwa.

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya jinsi ya kujenga ujasiri usiotetereka ili uweze kufikia mafanikio yako. Ikiwa umefurahia makala hii na unahisi kuwa ilikuwa ya thamani kwako, usisite kuwashirikisha marafiki zako. Kama una swali au maoni usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp