
Kwenye maisha, ili uweze kuweka malengo ambayo yatakupa matokeo makubwa katika maisha yako ni lazima utaanzia katika wazo. Mambo yote makubwa unayoyaona hapa duniani yalianzia kwenye wazo. Mtu alikaa akawaza na akaamua kuchukua hatua. Ili wazo liweze kufanikiwa, ni lazima lipitie mchakato wa hatua mbalimbali. Watu wengi huwa wanaishia njiani kwenye mchakato huo na ndio maana mawazo yao huishia njiani na hivyo kushindwa kufikia malengo waliyokusudia. Katika Makala ya leo nitakushirikisha na kukupitisha kwenye hatua hizi nne muhimu ambazo ni lazima upitie kabla wazo lako halijafanikiwa.
Hatua 4 ambazo utapitia kabla wazo lako halijafanikiwa.
1. Conception stage
Katika hatua hii, unakuwa umepata wazo ambalo unafikiria linaweza kukutoa kimaisha. Ni hatua ambayo unakuwa na hamasa kubwa ya kufanya. Katika hatua hii hauoni vikwazo vyovyote ambavyo vinaweza kusababisha wazo lako lisiweze kufanikiwa. Unakuwa na hamu ya kumshirikisha kila mtu wazo lako. Hii ni hatua ya mwanzo kabisa.
2. Rejection stage
Baada ya conception stage, hatua inayofuata ni rejection stage. Katika hatua hii, wazo lako linaanza kupata upinzani. Unaanza kupata ukosoaji kutoka kwa marafiki, ndugu na jamaa wa karibu yako ambao mwanzoni uliamini kuwa wanaweza kukusaidia. Katika hatua hii watu wako wa karibu wanageuka na kuwa wakosoaji wakubwa. Ni hatua ambayo watu wanakuwa wanakueleza mapungufu tu ya wazo ulilowashirikisha na hawakupi mazuri ambayo yapo kwenye wazo lako. Ili uweze kuvuka kwenye hatua hii ni lazima uwe na uvumilivu wa kukabiliana na wakosoaji wote na usonge mbele ili uweze kupata mafanikio.
3. Implementation stage
Baada ya kuwa umevuka vikwazo vya wakosoaji wote, hatua inayofuata kuelekea mafanikio ya wazo lako ni implementation stage. Hapa unaanza kufanya kile ambacho ulikuwa umekipanga. Katika hatua hii unapaswa kufanya kwa bidii bila kuacha. Watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu walipofikia kwenye hatua hii walifanya kidogo halafu wakaacha na kuhamia kwenye wazo lingine jipya. Kwa lugha nyingine wanaacha kufanyia kazi mawazo yao wanaanzisha wazo jipya na hivyo kurudi kwenye hatua ya mwanzo ambayo ni conception stage. Ili uweze kufanikiwa, fanyia kazi wazo lako bila kuacha na kwa muda mrefu. Komaa na wazo lako na mafanikio utayaona.
4. Celebration stage
Hatua ya nne ni celebration stage. Hii ni hatua ambayo, mafanikio yameanza kuonekana. Hata wale waliokuwa wanakukosoa na kukupinga wanapoona umeanza kufanikiwa wanarudi kuungana na wewe na kujisifia kuwa na wao walikuwa ni sehemu ya mafanikio yako. Ni hatua nzuri ambayo unatakiwa kuendelea kufanyia kazi wazo lako.
Hivyo, mafanikio yoyote huwa hayaji kirahisi. Kila aliyefanikiwa alianza na wazo. Baada ya kuwa amepata wazo na kuanza kulifanyia kazi, alipitia vikwazo vingi vya wakosoaji na hatimaye baada ya kushinda vikwazo hivyo, mafanikio yalipatikana. Hivyo, kama una wazo na unafikiria kuwa linaweza kukutoa kimaisha, usihofu kufanya. Utapitia katika hatua hizi nilizozizungumzia kwenye somo hili, ukiweza kuvuka hatua tatu za mwanzo, mafanikio utayaona.
Kwa leo niishie hapo. Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kushinda vikwazo vyote ili uweze kufanikiwa. Kama una swali au maoni yoyote, usisite kuandika hapo chini. Pia unaweza kuwasiliana name moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye Makala zinazofuata.
- Mbinu Tatu Rahisi Za Mafanikio Zinazopuuzwa. - August 9, 2024
- Jinsi Ya Kugundua Kusudi La Maisha Yako - August 7, 2024
- Kanuni za Kujiwekea Malengo - August 5, 2024