Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni: Makosa 7 Ya Kuepuka.

Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni.

Ni rahisi sana kuanzisha biashara mtandaoni. Lakini, ikiwa hutafuata njia sahihi hutaweza kamwe kufanikiwa. Watu wengi wanaoanzisha biashara mtandaoni hukata tamaa na kuachana nazo baada ya muda mfupi sana. Mimi sitaki wewe uwe miongoni mwao.
Katika makala hii nitakushirikisha makosa 7 ya kuepuka ili uweze kuwa na biashara yenye mafanikio mtandaoni. Unapoepuka makosa haya utakuwa na nafasi kubwa zaidi ya kufanya biashara yako mtandaoni kwa mafanikio makubwa.

Makosa 7 Ya Kuepuka Ili Kuwa Na Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni.

1.Kutoichukulia Biashara Yako Mtandaoni Kama Biashara Halisi.
Watu wengi wanaoanzisha biashara mtandaoni hufanya hivyo kwa kujaribu. Wamesikia madai mengi kuhusu jinsi watu wanavyoweza kupata utajiri kwa urahisi mtandaoni. Ni kweli, gharama ni ndogo sana kuanzisha biashara mtandaoni. Unahitaji tu kuwa na blog yako ambapo gharama yake ni ndogo sana.

Kutokana na gharama kuwa ndogo, watu wengi hutamani kuanzisha biashara mtandaoni. Lakini baada ya kugundua kuwa siyo kazi rahisi kama walivyokuwa wanafikiria, hukata tamaa na kuachana na biashara ya mtandaoni.

Ikiwa hutaichukulia biashara yako ya mtandaoni kama biashara halisi basi uwezekano wa kushindwa ni mkubwa zaidi. Ni kweli huna haja ya kuwekeza pesa nyingi lakini unahitajika kuwekeza hisia, nguvu na akili yako yote katika biashara yako ya mtandaoni kama zilivyo biashara zingine.

Kujenga biashara mtandaoni yenye mafanikio kunahitaji kufanya kazi kila siku. Unahitajika kujifunza kufanya mambo sahihi na kutangaza biashara yako mtandaoni wakati wote.

Ikiwa biashara yako ya mtandaoni utaichukulia tu kama hobi, basi nafasi zako za mafanikio zitapungua sana. Hili ni kosa kubwa miongoni mwa makosa ambayo watu wengi huwa wanafanya.

Fikiria kwamba umewekeza akiba yako yote katika duka lako la mjini au mtaani kwako. Je, ungeichukulia biashara yako kama tu ni hobi? Hapana usingefanya hivyo. Kwa hiyo, fikiria kwamba umewekeza akiba yako yote ya maisha katika biashara yako mtandaoni. Kutakuwa na siku ambapo mambo yataenda mrama na biashara yako ya mtandaoni haitaenda kama ulivyokusudia. Unahitaji ustahimilivu na kujitolea kukabili matatizo haya na kusonga mbele na hivyo kujenga biashara yenye mafanikio mtandaoni. Kuchukulia biashara yako ya mtandaoni kama biashara halisi kutakusaidia kupata mafanikio.

2.Kutokuwa na mpango.
Hivi unafikiri ni watu wangapi wanaoanzisha biashara mtandaoni wanaweka mpango kwa ajili ya biashara zao? Jibu ni wachache sana. Hakuna anayejua ni biashara ngapi mtandaoni zinashindwa kila mwaka, lakini ni nyingi. Wamiliki wengi wa biashara mpya mtandaoni hawaweki malengo au kuwa na mpango. Kisha wanashangaa biashara zao zinaposhindwa kabisa.

Ikiwa unaanzisha biashara mtandaoni, weka lengo. Lengo rahisi la kuweka ni lile la kifedha. Fikiria kiasi gani unataka biashara yako ya mtandaoni ikuzalishie katika miezi 12 ya kwanza na kisha geuza kuwa lengo lako la kifedha.

Biashara yako ya mtandaoni ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Kizuizi pekee ni wewe. Tumia mchakato wa kuweka malengo wa SMART kuweka malengo yako. SMART ni ufupisho wa maneno kadhaa kama ifuatavyo:

  • Specific– lengo lako lazima liwe maalum, kwa mfano, biashara yangu ya mtandaoni itazalisha sh 1,000,000 mwaka ujao.
  • Measurable – lazima uweze kupima jinsi unavyosonga mbele kuelekea lengo lako. Bahati nzuri, kuna zana nyingi za kupima mafanikio ya biashara yako mtandaoni.
  • Achievable– Lengo lako lazima liwe linalofikika. Ni vigumu sana kuingiza dola milioni katika mwaka wako wa kwanza. Hivyo weka lengo unaloweza kulifikia.
  • Realistic– fikiria muda ulionao na rasilimali nyingine kama vile pesa.
  • Timed– lazima uweke muda kwa lengo lako, kama vile mwaka mmoja. Malengo yasiyo na kikomo hayana maana.
    Baada ya kuweka lengo lako, unahitajika kuweka mpangokazi wa kufikia lengo lako. Unatakiwa kuwa na orodha ya kazi za kila siku ambazo utazifanya ili kusonga mbele kutimiza lengo lako. Kwa hiyo fikiria kuhusu majukumu makubwa ya mpangokazi wako na kisha uyavunje kuwa majukumu madogomadogo ya kila siku. Kwa kufanya hivyo utakuwa umeepuka makosa ambayo watu wengi hufanya na hivyo kuwafanya wakate tamaa kwenye biashara ya mtandaoni.

Mpangokazi rahisi unaweza kuwa:

  1. Chagua mada (niche) na aina ya biashara yako ya mtandaoni.
  2. Kutengeneza blog.
  3. Kuweka maudhui.

Unaweza kuanza leo kwa kuchagua niche unayotaka kuingia.

3. Kutokuchagua Niche Sahihi.

Kuchagua niche sahihi ni muhimu sana katika kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni. Usifanye makosa katika hili. Ikiwa utakosea, unaweza kutumia muda mwingi, jitihada, na pesa bila kupata mafanikio makubwa. Kuna maelfu ya niche, lakini sio zote zinafaa kwa biashara mtandaoni.

Kwa nia njema, ikiwa utaanza biashara mtandaoni katika niche unayoipenda, utakuwa na motisha zaidi kufanya kazi kwa bidii na hivyo kupata mafanikio makubwa kwa haraka.

Hata hivyo, jambo hili linaweza kuwa na matokeo mazuri ikiwa niche unayoipenda ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Labda unapenda kushona nguo za kawaida, lakini je, kuna watu wengi watakaonunua nguo hizo?

Kuna mambo mawili unayopaswa kuzingatia unapochagua niche:

Je, kuna mahitaji? Tafuta kujua kama kuna watu wanaotafuta bidhaa au huduma katika niche hiyo. Unaweza kutumia Google kujua idadi ya utafutaji wa maneno muhimu katika niche unayotaka kuanzisha biashara mtandaoni. Kadri idadi ya utafutaji inavyokuwa kubwa, ndiyo kiashiria kuwa niche yako ni maarufu na inahitajika.

Je, kuna pesa katika niche hiyo? Fanya utafiti kwenye Google kwa kutumia maneno muhimu ya niche yako. Je, kuna matangazo mengi kwenye ukurasa wa kwanza wa matokeo ya utafutaji? Ikiwa ni ndiyo, hii inaonyesha kuwa kuna fursa ya kupata pesa.
Ikiwa bado una shaka kuhusu kuchagua niche sahihi, chagua ile unayohisi itakuwezesha kupata pesa. Usijali kama sio mtaalamu wa niche hiyo sasa. Unaweza kujifunza na kuwa bingwa baadaye. Ni bora kufanya hivyo kuliko kuchagua niche isiyo sahihi ambayo unaijua vizuri lakini haiwezi kukupatia kipato.

4.Kutokuchagua mfumo sahihi wa biashara mtandaoni:

Kuna mifumo kadhaa ya biashara mtandaoni ambayo unaweza kuchagua. Baadhi ya mifumo hii ni:

  • Uuzaji wa Washirika (Affiliate marketing): Hapa unatangaza bidhaa za makampuni mbalimbali kwa lengo la kupata gawio baada ya kupata wateja na kufanya mauzo.
  • Kuuza bidhaa na huduma zako mwenyewe: Hapa unakuwa ukiuza bidhaa au huduma zako.
  • Duka lako la e-commerce: Kuanzisha duka lako la mtandaoni na kuuza bidhaa.

Je, una ujuzi maalum unaohitajika? Baadhi ya huduma za kujitegemea zinazohitajika sana ni:

  • Kuandika makala.
  • Ubunifu wa picha (kama vile nembo) na kadhalika.
  • kutengeneze Programu za simu na computer.
  • kutengeneza blog na wavuti (websites)
  • Kutafuta masoko kwenye mitandao ya kijamii na kadhalika.

Ikiwa una ujuzi wa aina hizi, unaweza kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni kwa kuuza huduma zako na kupata pesa mtandaoni. Kumbuka kuwa utahitajika kuwa na nidhamu ili kutoa kazi bora kwa wateja wako kwa wakati unaostahili.

Mifano yote hii ya biashara mtandaoni ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Chagua ile inayokufaa na endelea nayo. Kumbuka kujifunza kuhusu mifumo hii. Usibadilishebadilishe biashara mtandaoni, kwani hautapata matokeo unayoyategemea.

5. Ugonjwa Wa Vitu Vinavyong’aa (Shiny Object Syndrome).
Mara nyingi utasikia msemo “nyasi ni za kijani zaidi huko.” Hii inamaanisha kuwa kuna fursa bora za mafanikio ya biashara mtandaoni mahali pengine kuliko hapa. Tunaiita ” Shiny Object Syndrome – ugonjwa wa vitu vinavyong’aa.”

Unapochagua aina ya biashara mtandaoni, kutakuwa na watu wanaokwambia kuwa umefanya uchaguzi mbaya na unapaswa kubadili biashara yako na kununua mafunzo yao ili ujifunze jinsi ya kupata utajiri kutoka kwao.

Watu wengi wanaochagua niche wanakabiliwa mara kwa mara na vitu vinavyong’aa vipya vinavyowadanganya. Kuna kozi na programu mpya zinazotolewa kila siku ambazo zote zitakuambia kuwa unahitaji kuacha unachofanya sasa na kufuata mwelekeo wao.

Simaanishi kuwa usiwekeze katika mafunzo zaidi kwenye biashara uliyoichagua. Unapaswa kujifunza kila kitu unachoweza kuhusu biashara yako na kuwa tayari kujaribu njia mpya ili kufanikiwa. Lakini unachopaswa kuepuka ni kubadili mwelekeo kabisa kwa sababu nyasi zinaonekana kijani zaidi upande mwingine.

6. Kutokupata watembeleaji wa kutosha.

Ikiwa ungeulizwa kwa nini biashara nyingi mtandaoni zinashindwa, sababu kuu ingekuwa nini kwa maoni yako? Je, ni ukosefu wa maslahi? Ukosefu wa rasilimali? Kutokuwa na muunganisho bora wa intaneti? Kwa maoni yangu, jibu halitakuwa lolote kati ya haya. Jibu ni: Kutokupata watembeleaji wa kutosha!

Ikiwa hutapata watembeleaji walengwa kwenye ofa zako basi hutaweza kupata pesa mtandaoni. Unaweza kuwa unapromoti ofa ya kawaida na bado ukapata pesa nzuri kutokana nayo ikiwa utavutia wageni wa kutosha kwenye ofa hiyo.

Kwa upande mwingine, unaweza kuwa na ofa bora zaidi duniani, lakini ikiwa hautavutia watembeleaji walengwa wa kutosha basi hutafanya mauzo mengi. Watembeleaji ni sehemu muhimu zaidi ya biashara yenye mafanikio yoyote mtandaoni bila kujali aina ya biashara mtandaoni uliyoichagua.

Ikiwa wewe umejiajiri mtandaoni na hakuna mtu anayejua kuhusu huduma zako, basi biashara yako mtandaoni itashindwa. Kama mfanyabiashara mshirika (affiliate ) ikiwa hautavutia wageni wa kutosha kwenye ofa unazopromoti basi hutapata kamisheni yoyote. Bila watembeleaji walengwa kwenye duka lako la biashara mtandaoni hutauza chochote – na hivyo ndivyo inavyokuwa.

Mara tu unapoweka biashara yako mtandaoni unahitajika kutumia muda mwingi kuitangaza. Kuna njia kadhaa unazoweza kufanya hivyo. Ikiwa hutaki kutumia pesa unaweza kuitangaza biashara yako kwa kushea kwenye mitandao ya kijamii na kadhalika.

Ikiwa una pesa kidogo za kuwekeza basi unaweza kutumia matangazo ya kulipia kuitangaza biashara yako mtandaoni. Unaweza kununua wageni wa kulipia matangazo ya Google (Google ads) au matangazo ya facebook (facebook ads). Ninapendekeza ufanye mchanganyiko wa matangazo ya bure na matangazo ya kulipia.

Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kutafuta watembeleaji kwenye biashara yako ya mtandaoni. Hakuna watembeleaji inamaanisha hakuna biashara. Kwa hiyo fanya kila jitihada kuitangaza biashara yako mtandaoni wakati wote. Wageni wengi zaidi unapopata ndivyo unavyoweza kuwa na biashara yenye mafanikio na hivyo kupata pesa zaidi.

7.Kutokupima na kutathimini maendeleo ya biashara yako ya mtandaoni.

Moja ya faida kubwa ambayo biashara ya mtandaoni inayo ikilinganishwa na biashara ya kawaida ni kwamba unaweza kupima karibu kila kitu kwa wakati halisi. Lakini wamiliki wengi wa biashara mtandaoni hupuuza hili au hawalizingatiii vya kutosha.

Ikiwa unataka kujua ni wageni wangapi walitembelea tovuti yako wiki iliyopita unaweza kutumia programu kama Google Analytics kukujulisha hili. Pia unaweza kujua wageni wako walitoka wapi na ni kurasa zipi za tovuti yako walizotembelea.

Ni muhimu pia kujua walikaa muda gani kwenye tovuti yako. Watembeleaji wako wanapaswa kukaa kwa muda mrefu iwezekanavyo. Ikiwa wanaondoka haraka basi unahitajika kuchunguza kwa nini na kurekebisha tatizo hili.

Huwezi kusimamia kile usichoweza kupima. Na pia kwenye biashara ya mtandaoni unaweza kupima vitu vingi kwa hiyo tumia fursa hii. Itakuambia ni kampeni zipi zinazofanya kazi na pia itaangazia maeneo ya tovuti yako ambayo unahitajika kuyafanyia maboresho. Taarifa hii ni ya thamani kwa hiyo hakikisha unaitumia.

Nimatumaini yangu kuwa umenufaika kiasi cha kutosha na makala hii ya Makosa 7 Ya Kuepuka Ili Kuwa Na Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni. Nimeelezea kwa undani makosa 7 ambayo wamiliki wapya wa biashara mtandaoni hufanya ambayo yanawazuia kuwa na mafanikio. Sasa kwa kuwa unafahamu makosa haya unahitajika kujizatiti ili uweze kuyaepuka na hivyo kukuza biashara yako.

Kama una swali lolote kuhusiana na jinsi ya kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp