Hatua 7 Za Kufuata Ili Uweze Kufikia Uhuru Wa Kifedha.

Uhuru wa kifedha

Katika maisha lengo moja ambalo sote tunalo sawa ni kwamba, sote tunataka kuwa na kipato zaidi ili tuweze kuwa na uhuru wa kifedha. Hata hivyo, ni asilimia ndogo tu kati yetu tunapata uhuru wa kifedha tunaotamani. Sote tunataka kuwa na pesa za kutosha ili tuwe na maisha bora. Swali pekee ni, “Je, uko tayari kuwa na uhuru wa kifedha?” Habari njema ni kwamba kuna watu wengi zaidi wanaopata uhuru wa kifedha haraka zaidi kuliko hapo awali. Kupitia mipango sahihi ya kifedha pamoja na utekelezaji makini unaweza kuboresha kipato chako na kuwa miongoni mwa watu wenye uhuru wa kifedha . Katika makala ya leo nitakushirikisha hatua saba za kufuata ili uweze kukuza kipato chako na kuwa na uhuru wa kifedha.

Kanuni ya kuwa na Uhuru wa Kifedha
Uhuru wa kifedha unamaanisha kuwa una uwezo wa kuishi maisha yako bila kuwa na wasiwasi wa kupungukiwa au kuishiwa na fedha. Ikiwa uko tayari kupata uhuru wa kifedha, hapa kuna Kanuni yenye vipengele saba unayoweza kutumia ili kukusaidia kukusanya mali, kuwa na furaha zaidi, na kupata uhuru wa kifedha katika miaka ijayo.

1.Anza Kuwa na mtizamo chanya Kuhusu fedha.
Hatua ya kwanza ya kuwa tajiri na kupata uhuru wa kifedha inahusisha kuwa na mtizamo chanya kuhusu fedha. Kufikiria vibaya kuhusu fedha ni kikwazo cha kihisia ambacho lazima ukiondoe ili uweze kufikia uhuru wa kifedha. Lazima uondoe mawazo kwamba, kuwa na pesa nyingi husababisha uovu au kwamba, pesa haiwezi kununua furaha. Unapoanza kuwa na mtizamo chanya kuhusu pesa, utavutia fursa na kufungua milango zaidi ya kutengeneza kipato.

2.Andika Upya Malengo Yako Makuu ya Uhuru wa Kifedha
Jiwekee malengo ya kifedha. Andika upya na uhakiki malengo yako kwenye karatasi kila siku na ufikirie jinsi unavyoweza kuyatimiza. Hii itakuchukua kati ya dakika tano mpaka kumi. Kitendo cha kuandika upya malengo yako, na kuyafikiria kila asubuhi kabla ya kuanza ratiba yako ya siku nzima, kutaongeza nafasi zako za kuyatimiza.

3.Panga Ratiba Yako Ya Siku.
Panga ratiba yako ya siku mapema. Wakati mzuri wa kufanya hivyo ni usiku uliopita. Kitendo chenyewe cha kupanga kila siku, kila wiki, na kila mwezi mapema mambo ambayo utayafanya, kitakufanya uwe na hamasa zaidi na makini zaidi katika kila kitu unachofanya.Unapoweka mambo utakayofanya kwenye orodha, utaweza kujidhibiti ili ufanye tu mambo ambayo umeyakusudia kwa muda husika. Unapopanga kila siku mapema utaweza kudhibiti na kufuatilia tabia zako za matumizi pia. Panga kiasi unachopaswa kutumia kwa wiki, mwezi, au mwaka na uamue ni kiasi gani utaweza kuweka akiba.
Kwenye pesa yako uliyoitenga Kwa ajili ya akiba, weka sehemu ya pesa hivyo kwenye akaunti ya akiba, nyingine kwenye hazina ya dharura, nyingine kwa ajili ya kulipia madeni Pia unaweza kufikiria kutenga sehemu yako ya akiba kwa ajili ya kuwekeza kwenye soko la hisa na mifuko ya pamoja ya uwekezaji.

4.Kanuni ya Kuzingatia
Zingatia kwa nia moja, kila saa ya kila siku, inatumika vyema kwa ajili ya malengo uliyojiwekea. Kanuni ya umakini ni muhimu kabisa kufikia uhuru wa kifedha. Hakikisha kuwa kila kitu unachokifanya katika suala la kuweka malengo na mipango ya kifedha, kinalenga kukuwezesha kuamua jambo moja au mawili ambayo unapaswa kuzingatia zaidi kuliko kitu kingine chochote. Mambo unayozingatia zaidi na kutumia muda mwingi kufanya yanapaswa kuwa katika upatanishi wa moja kwa moja na malengo yako ya kifedha.Tumia muda wako kuzingatia kile kitakachokutengenezea pesa nyingi zaidi.

5.Wekeza Ndani Yako
Sikiliza programu za sauti za mafunzo mbalimbali kuhusu fedha kwenye gari lako. Kwa kugeuza gari lako kuwa chuo kikuu cha magurudumu, unaweza kuwa mmoja wa watu wenye ujuzi zaidi katika taaluma yako.
Nunua kozi za usimamizi wa fedha, soma vitabu kuhusu maendeleo binafsi ya kifedha na utafute makala mtandaoni kuhusu fedha. Unaweza hata kuwekeza kwako mwenyewe kwa kupata ushauri kutoka kwa mshauri wa kifedha. Baada ya muda utakuwa na maarifa mengi katika eneo la fedha kiasi kwamba watu watakuja kwako kutaka ushauri.

Jiulize Maswali Haya Ya Ajabu.
Jiulize “Maswali ya ajabu” mawili baada ya kila tukio muhimu maishani mwako.
Swali la kwanza ni, “Nilifanya nini Kwa usahihi?”

Na swali la pili ni, “Nitafanya nini Kwa namna tofauti, wakati ujao?”

Kwa kukagua utendaji wako mara baada ya kila tukio muhimu maishani mwako kama vile, mkutano, simu ya mauzo, na uwasilishaji, utakuwa bora haraka kuliko unavyoweza kufikiria. Majibu ya maswali haya yote mawili ni chanya. Kwa kukagua ulichofanya vizuri na kile ambacho ungefanya kwa njia tofauti wakati ujao, unapanga akilini mwako mwelekeo wa kuwa bora zaidi wakati ujao. Ikiwa utachukua dakika chache na kuandika kila kitu ulichofanya kwa usahihi na kila kitu ambacho ungefanya kwa njia tofauti mara tu baada ya tukio muhimu kama vile, simu au wasilisho, utajifunza kukua na kuboresha kazi yako kwa haraka zaidi. Unapojitathimini na kufanya maboresho kwenye kazi yako, kwa kweli, kutaboresha pia pesa ambazo utakuwa unapata.

7.Kuwa Mkarimu kwa Wengine
Jambo la mwisho ni kumtendea kila mtu unayekutana naye kama mteja wa mamilioni. Mtendee kila mtu, nyumbani na kazini, kana kwamba ndiye mtu muhimu zaidi ulimwenguni. Kwa kuwa kila mtu anaamini kwamba yeye ndiye mtu muhimu zaidi ulimwenguni, unapomtendea kana kwamba ndiye mtu wa thamani na muhimu kuliko wote, atathamini kwa jinsi ulivyomtambua na kumthamini na hivyo atakupenda na huduma yako au bidhaa yako pia ataipenda. Ni ukweli uliothibitishwa kwamba kuwa mtu mkarimu zaidi kutakusaidia kuvutia utajiri zaidi na kuwa mtu mwenye furaha zaidi.

Jinsi ya Kuokoa Pesa na Kupata Uhuru wa Kifedha.

Uhuru wa kifedha

Katika jambo hili, ninapendekeza mchakato wa polepole wa kujifunza kuokoa pesa. Kwa kuanzia, anza na 1% ya mapato yako na kuishi kwa 99% nyingine.
Kwa mfano, ikiwa unapata Tsh.200,000 kwa mwezi, fanya uamuzi leo wa kuokoa Tsh.2000 kwa mwezi. Kisha unaweza kuishi kwa kutumia Tsh.198, 000 nyingine. Okoa pesa kwa muda mrefu kwa kufungua akaunti tofauti ya benki, akaunti yako ya “uhuru wa kifedha”.
Mara tu unapoweka pesa kwenye akaunti hii ya akiba/uwekezaji, hutazitoa au kuzitumia kwa sababu yoyote ile.

Mara tu unapokuwa na maisha mazuri kwa 99% ya mapato yako, ongeza kiwango chako cha akiba cha kila mwezi hadi 2% na kuendelea.
Ndani ya mwaka mmoja, utajikuta unaishi kwa raha kabisa kwa 98% ya mapato yako ya sasa.

Endelea na mchakato huu hadi uokoe 15% na kisha 20% ya mapato yako. Hutaona hata tofauti katika kiwango chako cha maisha kwa sababu badiliko litakuwa ni la taratibu sana. Lakini tofauti katika maisha yako ya kifedha itakuwa ya kushangaza kabisa.

Kwa leo niishie hapo. Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kupiga hatua kuelekea kwenye uhuru wa kifedha. Kama una swali au maoni yoyote, usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

2 Replies to “Hatua 7 Za Kufuata Ili Uweze Kufikia Uhuru Wa Kifedha.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp