Kanuni 3 Za Kuwa Na Maisha Yenye Furaha.

Kanuni 3 Za Kuwa Na Maisha Yenye Furaha

Hivi umeshawahi kupitia kipindi ambacho umekuwa ukijihisi hauna furaha katika maisha yako? Kila kitu unachokifanya unaona kabisa kinakuletea furaha ya muda mfupi tu na baadaye furaha yako inatoweka. Tatizo ni kuwa, umekuwa ukitafuta furaha bila kuwa na kanuni madhubuti ambazo zitakuletea furaha ya kudumu katika maisha yako. Hivyo, ili uweze kuwa na furaha katika maisha yako, unaohitajika kuwa na muda wa kuweka kanuni ambazo zitakuletea furaha katika maisha yako. Katika makala ya leo nitakushirikisha kanuni 3 za kuwa na maisha yenye furaha.

Kanuni 3 za kuwa na maisha yenye furaha.

1.Kuwa mtu mwenye malengo.
Miongoni mwa kanuni ya muhimu sana ya kuwa na maisha yenye furaha ni kuwa mtu mwenye malengo. Ili uweze kuwa na furaha, unahitajika kuweka malengo ambayo yataendana na kusudi la maisha yako na kuyafanyia kazi kila siku. Hii itakupa ramani halisi ya mwelekeo wa maisha yako na jinsi ambavyo utaitumia kila siku kuweza kutimiza malengo yako. Kwa kufanya hivyo utakuwa ukisogelea mafanikio yako na hivyo furaha yako kuongezeka. Kwa kufanyia kazi malengo uliyoyaandika, utajihisi furaha unapokuwa ukipiga hatua kwa kukamilisha lengo moja baada ya lingine kwa siku hiyo. Siku inapokuwa imeisha na ukaangalia nyuma mambo uliyoyatimiza, utajiona mwenye furaha kwani utakuwa unapiga hatua kuelekea kwenye mafanikio yako.

2.Kuwa mtu unayetaka matokeo.
Unapokuwa umeandika malengo yako, utaweza kupima maendeleo yako kwa kuweka vigezo vya mafanikio. Vigezo hivi vitakuwezesha kufahamu mafanikio yako hatua kwa hatua. Utaweza kufahamu ni hatua gani uliyofikia na ni hatua gani zaidi zinahitajika kuweza kufikia matokeo uliyoyakusudia. Unapokuwa unapima hatua za mafanikio yako, utaweza pia kujifunza muda ulioutumia na hivyo kukujengea tabia ya kutunza muda. Kadiri unavyokuwa unapiga hatua kwenye mafanikio uliyojiwekea kwa kutumia vigezo vya mafanikio ulivyoviweka, ndivyo utakavyokuwa na furaha zaidi katika maisha yako.

3.Endelea kuchukua hatua bila kuacha.
Kwa kuwa kuweka malengo ni jambo la muhimu sana ambalo litakupa hamasa ya kufanya kazi, ni muhimu kuendelea kuchukua hatua bila kuacha. Kumbuka, kuwa na malengo yaliyoandikwa bado haitoshi. Unahitajika kuchukua hatua kufanyia kazi malengo yako bila kuacha. Unapokuwa unapiga hatua haijalishi ni kubwa au ni ndogo kiasi gani, furaha yako itaongezeka.

Swali la leo.
Ni kanuni gani kati ya hizi tatu za kuwa na maisha yenye furaha utaanza kuitumia leo?
Ninatamani sana unishirikishe kwa kuandika kwenye sanduku la maoni hapa chini. Pia kama una swali au maoni yoyote, usisite kuandika hapa chini. Asante na karibu tena katika makala ijayo.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

One Reply to “Kanuni 3 Za Kuwa Na Maisha Yenye Furaha.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp