Mambo 3 Wanayofanya Watu Waliofanikiwa.

Mambo 3 muhimu wanayofanya watu Waliofanikiwa Duniani.

Katika kufanya utafiti na kusoma kwangu vitabu nilitamani kujifunza jinsi watu waliofanikiwa na matajiri duniani wanavyoishi. Lengo la kusoma kwangu vitabu lilikuwa ni kujua siri ya maisha yao na kufahamu vitu vya tofauti wanavyofanya na hivyo kuweza kujitofautisha na watu wa kawaida. Miongoni mwa watu ambao niliowahi kusoma vitabu vyao ni aliyekuwa Rais wa Marekani, Donard Trump pamoja na matajiri wengine wengi. Katika kusoma kwangu, niligundua kuna mambo matatu muhimu ambayo watu waliofanikiwa huwa wanafanya. Katika Makala ya leo nitakushirikisha mambo matatu muhimu wanayofanya watu waliofanikiwa Duniani ambayo hata wewe unaweza kuyafanya ili uweze kufanikiwa.
Mambo 3 muhimu wanayofanya watu waliofanikiwa duniani.
1. Ni wasomaji wazuri sana wa vitabu.
Jambo la kwanza kabisa ambalo watu waliofanikiwa hufanya ni wasomaji wazuri sana wa vitabu. Ukifuatilia matajiri wote wakubwa wa dunia kama vile Donard Trump, hutumia muda wao mwingi katika kuongeza maarifa kupitia usomaji wa vitabu. Lengo kubwa la usomaji wao wa vitabu ni kuongeza ujuzi na maarifa kuhusiana na biashara pamoja na shughuli zao zingine wanazozifanya. Hivyo, hata wewe kama unataka kufanikiwa kwenye malengo yako, wekeza muda wako katika kujenga ujuzi wako kwenye shughuli unayofanya ili uweze kupata matokeo makubwa. Akili ya mwanadamu ni kama panga la kukatia ambalo linatakiwa kunolewa ili liweze kukata kwa urahisi. Tunanoa akili zetu kwa kujifunza maarifa mapya kila siku kupitia usomaji wa vitabu. Hivyo, kama unataka kufanikiwa, panga ratiba ya kusoma vitabu kila siku.
2. Hawaishi maisha ya kujionyesha ili kuridhisha watu.
Changamoto kubwa iliyopo kwa watu wengi ni kuishi maisha yasiyokuwa na uhalisia. Unakuta mtu anatamani kuishi maisha ya juu kuliko kipato chake. Anatamani awe na gari, awe na nguo za gharama kubwa, apange kwenye nyumba ya bei ya juu wakati kipato chake hakiwezi kuhimili gharama hizo. Wanaishi maisha yao ili kuwaridhisha watu. Matokeo yake ni kuingia kwenye madeni na kupata stress za maisha. Watu waliofankiwa hawafanyi hivyo. Wanaishi maisha yao kulingana na kipato chao. Hawaishi kuwaridhisha watu. Hivyo, ili uweze kufanikiwa, unapaswa kuwa na bajeti na matumizi yako yasizidi kipato chako. Ishi maisha yako na siyo kuishi ukishindana na watu.
3. Matumizi yao makubwa ya pesa yanaenda kwenye uwekezaji.
Watu waliofanikiwa wanapopata kipato chao hawaelekezi kipato chao chote kwenye matumizi ya kawaida. Asilimia kubwa ya kipato chao huwa wanakielekeza kwenye uwekezaji. Kila wanapopata kipato, asilimia Fulani wanawekeza kwenye biashara, kwenye kununua hisa, kwenye kununua hatifungani na kadhalika. Kabla ya kuanza kufanya matumizi ya kawaida, jambo la kwanza kabisa huwa wanatenga pesa kwa ajili ya uwekezaji. Hebu jiulize swali hili, kila unapopata pesa, ni asilimia ngapi unawekeza? Kama hauwekezi, na pesa yote unatumia kwa matumizi ya kawaida, basi hautaweza kufanikiwa. Haijalishi unapata kiasi gani cha pesa. Hata kama ni kidogo kiasi gani, kumbuka kutenga kwanza kiasi cha pesa ambacho utawekeza.
Kwa leo niishie hapo. Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kutosha kuhusiana na mambo wanayofanya watu waliofanikiwa ambayo hata wewe pia ukifanya utapata mafanikio makubwa. Kama una maoni au swali lolote usisite kuweka maoni yako hapa chini. Pia kwa ushauri wowote, usisite kuwasiliana name kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu tena kwenye Makala zinazofuata.

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

2 Replies to “Mambo 3 Wanayofanya Watu Waliofanikiwa.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp