Jinsi Ya Kufanya Utafiti Wa Wateja Wako

Jinsi Ya Kufanya Utafiti Wa Wateja Wako

Katika somo lililopita tuliangalia Jinsi Ya Kugundua Biashara Unayopaswa Kufanya Mtandaoni. Nilikuelezea kwa kina kanuni rahisi kabisa ambayo ukiitumia itakusaidia kugundua wateja wako watarajiwa wa biashara yako ya mtandaoni. Kanuni hii inaitwa PPP au 3P. Unaweza kupitia kanuni hii kwani nimeielezea kwa kina kwenye somo langu lililopita. Sasa, baada ya kuwa umegundua biashara unayopaswa kuanzisha mtandaoni, hatua inayofuata ni kufanya utafiti wa wateja wako ili uweze kufahamu mahitaji yao. Katika somo la leo nitakushirikisha kanuni nyingine ya Jinsi Ya Kufanya Utafiti Wa Wateja Wako (Researching Your Customers). Kanuni hiyo inaitwa P.L.A.N.

Jinsi Ya Kufanya Utafiti Wa Wateja Wako (Researching Your Customers).

Katika somo lililopita tuliangalia jinsi ya kugundua biashara unayopaswa kuanzisha mtandaoni. Na katika somo lililopita tulichukulia mfano wa biashara ambayo tulikuwa tumeipata kuwa ni biashara ya Ushauri wa Kibiashara. Katika somo la leo tutaangalia jinsi ya kufanya utafiti wa wateja wako kwenye hii biashara unayotaka kuanzisha. Ili uweze kufahamu mahitaji ya wateja wako, kanuni rahisi unayoweza kuitumia ni P.L.A.N. Kanuni hii ni ufupisho wa maneno matatu ya Kingereza ambayo ni P-PROBLEM ,LA-LANGUAGE, na N-NEEDS (Customer’s needs). Sasa. tuanze kuchambua kwa kina jinsi ya kufanya utafiti wa wateja wako kwa kutumia kanuni hii.

P-PROBLEM- Matatizo ya wateja.

Hatua ya kwanza kabisa ni kuangalia matatizo au changamoto ambazo wateja wako watarajiwa wanazo. Hii ni kwa sababu, matatizo ya wateja wako ndiyo msingi halisi wa biashara yako. Hivyo unatakiwa kuangalia wateja wako watarajiwa wanapitia matatizo gani. Kumbuka kuwa, lengo la kuanzisha biashara mtandaoni ni kutatua matatizo ya watu. Pesa itakuja kama matokeo ya baadaye. Hivyo, ili uweze kufanikiwa kwenye biashara yako, jikite zaidi katika kutatua matatizo ya wateja wako. Utakapoweza kutatua matatizo ya wateja wako, nakuhakikishia kuwa pesa itakuja tu.

Ili uweze kufahamu matatizo ya wateja wako, ingia Google na uangalie blog, majukwaa na channel mbalimbali za YouTube zinazotoa mafunzo ya kibiashara ili waweze kuangalia watu wanauliza na kuchangia nini. Komenti mbalimbali za watembeleaji ndiyo changamoto au matatizo wanayokutana nayo katika maisha yao. Hivyo, tumia maoni na maswali ya watu wanayouliza ili kuweza kuanzisha biashara ambayo itajikita kutatua matatizo yao.

LA-LANGUAGE- Lugha wanayotumia.

Baada ya kuwa umetambua matatizo yao, jambo linalofuata ni kuainisha aina ya watu unaoenda kuwahudumia. Je wanatumia lugha gani? Hapa utazingatia umri wao, jinsia na kadhalika. Kama unaenda kuhudumia vijana, hakikisha unatumia lugha inayoendana na rika lao. Hali kadhalika wazee, wanawake na makundi mengine. Kumbuka kuwa ili uweze kufanya biashara mtandaoni ni lazima kwanza utengeneze mahusiano na wateja wako watarajiwa. Hivyo, ukitumia lugha yao waliyoizoea, itakuwa rahisi kujenga nao mahusiano na hivyo kuwa tayari kupokea huduma yako.

N-NEEDS – Mahitaji ya wateja.

Baada ya kuwa umetambua matatizo ya wateja wako watarajiwa na kufahamu lugha yao, hatua inayofuata ni kuangalia mahitaji yao. Kimsingi, mahitaji ya wateja wako watarajiwa yatatokana na matatizo waliyonayo. Kwa mfano, kama wateja wako wana changamoto ya jinsi ya kuanzisha biashara, basi, hitaji lao litakuwa ni elimu ya jinsi ya kuanzisha biashara. Unaweza kuwapatia elimu kwa kuandaa kozi au kitabu pepe ambacho utawauzia na kadhalika.

Nimetumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kufanya utafiti wa wateja wako watarajiwa. Kama una swali au maoni yoyote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kupitia 0752 081669. Asante sana na karibu katika somo linalofuata.

Masomo yaliyopita.

1. Jinsi ya kuanzisha biashara mtandaoni: Utangulizi.

2. Biashara inayolipa mtandaoni ni ipi?

3. Jinsi ya kutafuta wazo bora la biashara yako ya mtandaoni.

4. Jinsi ya kugundua biashara unayopaswa kufanya (Discovering your niche).

Kingi Kigongo
Ungana nae
Latest posts by Kingi Kigongo (see all)

2 Replies to “Jinsi Ya Kufanya Utafiti Wa Wateja Wako”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp