Watu waliofanikiwa ni wale tu wenye tabia za mafanikio. Brian Tracy aliposema hivyo, alieleza ukweli muhimu kuhusu kufanikiwa katika maisha binafsi na ya kitaaluma. Ili uweze kufanikiwa, kuna tabia na mbinu rahisi ambazo unapaswa kuzifuata. Kuzingatia mbinu hizi rahisi mara nyingi ni jambo lenye nguvu zaidi unaloweza kufanya ili uweze kufikia mafanikio yako. Katika makala hii nitakushirikisha Mbinu Tatu Rahisi za Mafanikio Zinazopuuzwa.
Mbinu Tatu Rahisi Za Mafanikio Zinazopuuzwa.
Mbinu Namba 1: Usingizi
Katika dunia yetu ya kisasa, watu wengi wanakosa usingizi kutokana na sababu mbalimbali. Sababu ya kwanza ni kwamba tunaishi maisha yenye shughuli nyingi na msongo wa mawazo. Tuko katika hali ya harakati za kila namna. Ni rahisi kukosa usingizi mzuri kwa kujidanganya kwamba hii inatupa muda zaidi wa kumaliza kazi nyingine. Au, msongo wa siku unaweza kufanya kuwa vigumu kwa baadhi ya watu kutuliza akili zao na hivyo kusababisha kulala kuwa ni changamoto.
Sababu nyingine inayosababisha kukosa usingizi katika nyakati hizi ni kukaa muda mrefu kwenye kompyuta, TV, na skrini za simu usiku wa manane. Jambo hili linaathiri uzalishaji wa melatonini na kufanya kuwa vigumu kulala. Ili kusaidia kuepukana na tatizo hili, jaribu kuepuka au kupunguza muda wa kutumia kompyuta, TV na simu angalau saa moja kabla ya kulala.
Tabia nyingine inayoweza kuongeza usingizi ni pamoja na kuandika diary au kufanya shughuli yoyote inayosaidia kutuliza akili na mwili kama vile kusoma kwa utulivu au kutafakari. Ukianza kupata usingizi wa kutosha kila usiku, mwili na akili yako itajiandaa kufurahia siku inayofuata na hivyo utashangazwa na matokeo yatakayokuja. Utaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Mbinu Namba 2: Mazoezi
Mbali na kuboresha usingizi wako, mazoezi ya kawaida ni lazima. Faida za kimwili za mazoezi zinafahamika vizuri, lakini faida za kiakili za mazoezi pia ni za kuzingatiwa. Tafiti nyingi zimeonyesha kuwa mazoezi ya kawaida yana athari kubwa kwa kuongeza kujiamini, matumaini, na ari. Unapofanya mazoezi, mwili wako hutoa endorphins, homoni inayokufanya ujisikie vizuri siku nzima na kutoa faida nyingi za kiakili, kihisia pamoja na za kimwili.
Hii itakuruhusu kufanya kazi zaidi siku nzima, na kukufanya uhisi umekamilika na kufanikiwa, kukionyesha kuwa unaweza kuweka malengo na kuyafanikisha. Kwa hiyo fanya mazoezi unayoyafurahia, na uyafanye mara kwa mara ili kufaidika na matokeo yake.
Mbinu Namba 3: Mawazo Chanya
Hatimaye, lazima ufikirie kwa njia chanya. Kuna nukuu maarufu ya Henry Ford inayosema, “Iwapo unafikiri unaweza au unafikiri huwezi, labda uko sahihi.” Hii ina maana kwamba, mtazamo wako juu ya maisha yako mara nyingi hugeuka kuwa unabii unaotimia kwako.
Unapojaza akili yako kwa mawazo chanya na matumaini, matokeo chanya kwa kawaida hufuatia. Kinyume chake, ikiwa unajaza akili yako na mawazo hasi na kukata tamaa, matokeo hasi utayapata. Kwa hiyo kuwa makini na mawazo yako, na ukiona mawazo hasi yanakuja, jaribu kuyabadilisha na mawazo chanya.
Mawazo chanya ni kama mafuta kwa akili yako, yanayokusukuma kufanikiwa na kukusaidia kushinda changamoto utakazokutana nazo badala ya kuvunjika moyo au kuziona kama vikwazo vya kudumu. Ili kuwa na mawazo yanayojielekeza kwenye mafanikio, ni muhimu kuanza kuwa na mtazamo chanya katika nyanja zote za maisha yako.
Kwa kuzingatia mbinu hizi tatu za msingi ambazo mara nyingi hupuuzwa, utaweza kuweka msingi wa kufanikisha malengo yako binafsi na ya kitaaluma. Kwa kupata usingizi mzuri, kujenga mwili wako, na kujaza akili yako na mawazo chanya, utaweza kuupatia mwili na akili yako kile kinachohitajika kufikia malengo yako na kushinda changamoto yoyote inayoweza kukujia.
Hatua za Kuchukua Leo
Sasa swali la leo ni hili, ni hatua zipi maalum utachukua leo kuboresha usingizi wako, mazoezi yako na mtazamo wako wa maisha? Acha maoni hapa chini nami nitahakikisha ninakujibu.
Ikiwa umefurahia makala hii na unadhani imekuwa na thamani katika kukuonyesha Mbinu Tatu za Mafanikio Zinazopuuzwa, usisite kushiriki na marafiki zako au mtu yeyote ambaye anaweza kufaidika na makala hii.Kama una swali au maoni yoyote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala inayofuata.
Kusudi lako kuu maishani ni jambo ambalo unapaswa kulijua na hivyo kupanga malengo pamoja na kufanya shughuli zako kwa kuzingatia kutimiza kusudi lako. Brian Tracy, mtaalamu wa maendeleo binafsi aliwahi kusema kuwa, “Umewekwa kwenye hii dunia ili uweze kutimiza jambo kubwa, zuri na la kushangaza kupitia maisha yako. Kazi yako ni kugundua ni jambo gani hilo na kisha ulifanye kwa moyo wako wote, ili uache urithi kwa vizazi vijavyo.”
Lakini mara nyingi, watu wengi huishi maisha yao yote bila kutumia uwezo wao au kuziishi ndoto zao. Badala ya kuishi kusudi lao la kweli maishani, wanaishi maisha ya kubahatisha, ambayo yanasukumwa na shinikizo, watu wengine, na majukumu ya kila siku ambayo yako mbali sana na kile wanachotaka hasa maishani. Katika makala hii nitakushirikisha Jinsi ya Kutambua Kusudi la Maisha Yako.
Jinsi ya Kutambua Kusudi la Maisha Yako.
Ili uweze kutambua kusudi la maisha yako, jiulize maswali haya manne muhimu kwa uaminifu kadri uwezavyo.
Swali la Kwanza: Malengo Yangu Ya Maisha Ni Yapi?
Unapopita katika maisha, utapitia hatua nyingi tofauti. Ni muhimu kuwa na lengo lililo wazi la kile unachotaka kufanikisha katika kila hatua, na hasa katika kila kipengele cha maisha yako kama vile familia, mahusiano, kazi, uchumi, burudani na kadhalika. Kuwa na uwazi kuhusu kile unachotaka kufanikisha katika maeneo haya kutakuruhusu kupanga maisha yako kwa namna ya kufanikisha malengo hayo. Hii itakusaidia kuweka lengo kubwa na kisha kuligawanya na kuwa hatua ndogo ndogo za kuchukua ili kufanikisha lengo hilo. Hili ni swali la kwanza unalopaswa kulijibu unapokuwa unataka kutambua kusudi la maisha yako.
Swali la Pili: Kwa Nini Nipo Hapa?
Uwezekano wa wewe kuzaliwa ni 1 kati ya trilioni 400. Unapoangalia namba hiyo, ni uwezekano adimu sana, lakini umezaliwa. Uko kwenye sayari hii kwa sababu maalumu na kila mtu ana sababu tofauti. Je, ni kwa ajili ya kutunza familia yako? Je, ni kwa ajili ya kuunda kitu cha ajabu ambacho dunia inakihitaji? Je, umewekwa hapa duniani ili kuanzisha na kukuza biashara? Au ni ili kufurahia kadri uwezavyo kile kilichopo kwenye sayari hii? Ili kujibu swali hili, orodhesha sababu na njia zote unazodhani unahitajiwa kufanya maishani mwako ili kutimiza kusudi la maisha yako.
Swali la Tatu: Ninataka Nini Hasa Maishani?
Sasa kwa kuwa umejua malengo yako na kwa nini uko hapa, hatua inayofuata ni kufafanua kile unachotamani kuwa au kuwa nacho. Kusudi lako linapaswa kuendana na kile unachofurahia kufanya zaidi muda wako mwingi. Haina maana kutumia muda wako wa thamani, nguvu, na juhudi kwa kitu usichokipenda. Ndiyo maana ni muhimu sana kugundua kile unachotaka kufanya maishani na jinsi unavyotakiwa kutumia muda wako ili kubaini kusudi la maisha yako.
Swali la Nne: Ninaenda Wapi na Mafanikio ni Nini Kwangu?
Sasa kwa kuwa una wazo wazi la kile unachotaka maishani na una kusudi lililofafanuliwa vyema, sasa ni wakati wa kuchora njia ya unakoenda. Ili kufanya hivyo, unahitajika kuangalia mbele kwa siku zijazo na kufikiria jinsi unavyofikiri maisha yenye mafanikio yanavyoonekana kwako. Ili kukusaidia kufanya hivyo, fikiria jinsi maisha yako kamili yangekuwa baada ya miaka 3-5. Yatakuwa tofauti vipi na leo? Mara tu unapokuwa na wazo wazi kuhusu maswali haya muhimu, basi ni wakati wa kufanya kazi kwa nguvu ili uweze kutimiza malengo yako.
Unapoanza kufanya kazi kutimiza maono hayo, utagundua polepole hatua unazohitajika kuchukua kuanzia leo ili kujenga maisha ambayo yanakidhi kusudi lako la maisha. Haya ni maswali unayohitajika kujiuliza na hatua unazohitajika kuchukua ili kutengeneza maisha yako kamili. Siyo kazi rahisi, lakini kwa kupitia maswali haya muhimu, utaweza kufafanua kusudi la maisha yako.
Sasa, swali la leo ni hili, ni hatua gani umechukua leo kufafanua kusudi la maisha yako? Acha maoni yako hapa chini, na mimi nitahakikisha ninakufuatilia. Asante kwa kufuatilia makala hii. Ikiwa umefurahia makala hii na unahisi imekuwa na thamani katika kukufundisha kuhusu Jinsi ya Kupata Kusudi la Maisha Yako, usisite kuwashirikisha ndugu na marafiki zako.
Kama una maswali au maoni yoyote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.
Ili uweze kufanikiwa ni lazima uwe na malengo. Kujiwekea malengo kunaweza kuwa na uzoefu wenye nguvu wa kubadilisha maisha yako ikiwa utafanya kwa usahihi. Katika makala hii nitakushirikisha kanuni tano za msingi za kujiwekea malengo ambazo ni muhimu kwa mafanikio yako makubwa.
Kanuni ya Kwanza: Ulinganifu
Ili uweze kufanya vizuri zaidi katika maisha yako, malengo yako na maadili yako lazima yaendane. Maadili yako yanawakilisha imani yako ya kina kuhusu kile unachoona kuwa ni chema na chenye manufaa na kile unachoona kuwa ni kibaya kwako. Utendaji wako wa juu na mafanikio yako yatategemea tu pale ambapo malengo yako na maadili yako yapo katika upatanifu kamili.
Kanuni ya Pili: Eneo la Ubora
Kila mtu ana uwezo na ni bora katika kitu fulani, na pengine vitu kadhaa. Unaweza kufikia mafanikio makubwa tu kwa kupata eneo lako la ubora na kisha kuweka moyo wako wote katika kukuza vipaji vyako katika eneo hilo. Kwa lugha nyingine eneo la ubora ni kitu kimoja ambacho una uwezo wa kipekee wa kukifanya kwa ubora. Ni jukumu lako kukibaini kitu hicho, ikiwa bado hujakibaini.
Eneo lako la ubora linaweza kubadilika kadri taaluma yako inavyokua, lakini watu wote waliofanikiwa kwa kweli ni wale ambao wamegundua na kuwekeza nguvu zao zote kwenye maeneo yao ya ubora. Eneo lako la ubora mara zote ni kufanya kile unachokifurahia zaidi na kukifanya vizuri. Hivyo, kanuni ya pili ya kujiwekea malengo ni kwa kutambua eneo lako la ubora.
Kanuni ya Tatu: Kanuni ya Shamba la Almasi
Kanuni ya Shamba la Almasi inatokana na jina la hotuba iliyotolewa na mhubiri aitwaye Russell Conwell. Hotuba hiyo ilipendwa sana.
Katika hotuba hiyo alielezea hadithi ya mkulima mmoja mzee wa kiafrika ambaye alifurahia sana siku moja aliposikia kutoka kwa mfanyabiashara aliyesafiri kwenda Afrika kugundua migodi ya almasi na kuwa tajiri sana. Hivyo na yeye aliamua kuuza shamba lake, kuandaa safari, na kuelekea ndani ya Afrika ili kutafuta almasi kwa lengo la kuwa tajiri mkubwa.
Kwa miaka mingi, alisafiri sehemu kubwa ya bara la Afrika akitafuta almasi. Hatimaye, aliishiwa pesa. Mwishoni kabisa, akiwa peke yake, katika hali ya kukata tamaa, alijitupa baharini na kuzama.
Wakati huo huo, ndani ya shamba alilouza, siku moja mkulima mpya alikuwa akinywesha punda katika kijito kilichokatisha shamba hilo. Alipata jiwe la ajabu lililotoa mwanga kwa namna ya kushangaza. Alilipeleka nyumbani kwake na hakuwa anafahamu lolote kuhusiana na jiwe hilo. Baadaye, mfanyabiashara yule yule alipita kwenye shamba lile na yule mkulima mpya akamwonyesha lile jiwe. Mfanyabiashara alifurahi sana na akauliza kama yule mkulima mzee alikuwa amerudi hatimaye. Hapana, aliambiwa. Mkulima mzee hakuwa ameonekana tena tangu aondoke.
Mfanyabiashara alichukua jiwe hilo na kusema, “Hii ni almasi ya thamani kubwa.” Mkulima mpya alikuwa na shaka, lakini mfanyabiashara alisisitiza na akaomba aonyeshwe wapi alipata almasi hiyo. Wakaenda kwenye shamba ambalo mkulima alikuwa akinywesha punda, na walipozunguka, walipata almasi nyingine, na nyingine, na nyingine. Ikabainika kwamba shamba lote lilikuwa limejaa madini ya almasi. Mkulima mzee alikuwa ameenda Afrika kutafuta almasi bila ya kutazama chini ya miguu yake mwenyewe.
Hadithi hii inafundisha kwamba mkulima mzee hakuweza kutambua kwamba almasi hazionekani kama almasi katika hali yake ya asili. Huonekana kama mawe kwa macho yasiyo na elimu. Almasi inapaswa kukatwa, kupigwa msasa, na kung’arishwa kabla haijawa kama ile inayouzwa kwenye maduka ya vito.
Vivyo hivyo, mashamba yako ya almasi pengine yapo chini ya miguu yako mwenyewe. Lakini mara nyingi yamejificha yanahitaji juhudi kuweza kuyagundua. Mashamba yako ya almasi pengine yapo kwenye vipaji vyako, elimu yako, uzoefu wako, tasnia yako, mji wako, mawasiliano yako na kadhalika. Mashamba yako ya almasi yapo chini ya miguu yako mwenyewe na unachotakiwa kufanya ni kuchukua muda kuyatambua na kisha kuyafanyia kazi.
Theodore Roosevelt aliwahi kusema, “Fanya kile unachoweza, kwa kile ulicho nacho, hapo hapo ulipo.” Huna haja ya kuhamia nchi nyingine au kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yako. Mara nyingi, kile unachokitafuta kiko karibu sana na wewe. Lakini hakionekani kama fursa kwa sababu hujatumia muda wako kuchunguza na kufanyia kazi kwa bidii uwezo ulionao.
Kanuni ya Nne: Uwiano
Kanuni ya uwiano inasema kwamba, unahitaji malengo mbalimbali katika maeneo sita muhimu ya maisha ili uweze kufanya vizuri zaidi. Kama vile gurudumu la gari linavyopaswa kuwa na uwiano ili liweze kuzunguka kwa urahisi, unapaswa kuwa na malengo yenye uwiano ili maisha yako yaweze kwenda vizuri.
Unahitajika kuweka malengo katika maeneo yafuatayo: malengo ya kifamilia malengo ya kimwili kiafya. malengo ya kielimu na maendeleo binafsi (self development). malengo ya kazi na taaluma. malengo ya kifedha na mali. Hatimaye, unahitaji malengo ya kiroho,
Ili kudumisha uwiano mzuri, unahitajika kuwa na malengo mawili au matatu katika kila eneo, jumla ya malengo kumi na mawili hadi kumi na nane. Aina hii ya uwiano itakuwezesha kuwa unafanya kazi kila wakati juu ya kitu muhimu kwako. Unapokuwa haufanyi kazi kwenye ajira yako, unaweza kufuatilia malengo ya kifamilia. Unapokuwa haufanyi kazi juu ya afya ya mwili, unaweza kufanya kazi juu ya maendeleo binafsi na kadhalika.Lengo ni kutokupoteza muda wako kwa kufanya vitu ambavyo havipo kwenye malengo yako.
Kanuni ya Tano: Kusudi Kuu la Maisha
Kanuni ya tano ya kujiwekea malengo ni uamuzi wa kusudi kuu la maisha yako. Kusudi lako kuu ni lengo lako nambari moja, lengo ambalo ni muhimu zaidi kwako kuliko lengo lingine lolote kwa wakati huu. Unaweza kuwa na malengo mbalimbali lakini unaweza kuwa na kusudi kuu moja tu. Kukosa kwa mtu kuchagua lengo au kusudi kuu ni sababu kuu ya kutawanya juhudi, kupoteza muda na kushindwa kupiga hatua.
Jinsi ya kuchagua lengo kuu ni kwa kuchanganua malengo yako yote na kujiuliza, “Ni lengo gani, nikilifikia, litanisaidia zaidi katika kufanikisha malengo yangu mengine yote?”
Kwa kawaida, linaweza kuwa ni lengo la kifedha au kibiashara, lakini wakati mwingine linaweza kuwa lengo ni la afya au mahusiano. Uchaguzi wa kusudi lako kuu ndio mwanzo wa mafanikio yako makubwa. Lengo hili linakuwa ndiyo”dhamira” yako na kanuni ya kupanga shughuli zako zingine zote. Unapokuwa na msisimko au hamasa kuhusu kufanikisha lengo kuu lililo wazi, unaanza kusonga mbele haraka licha ya vikwazo na vizingiti vyote ambavyo utakutana navyo.
Kwa kutumia kanuni hizi tano za kujiwekea malengo, unaweza kufanikisha mambo makubwa na kuwa na mabadiliko ya kweli katika maisha yako. Ulinganifu kati ya malengo na maadili yako, kutambua eneo lako la ubora, kugundua mashamba yako ya almasi, kudumisha uwiano katika malengo yako yote, na kuchagua kusudi lako kuu la maisha, ni mambo muhimu yatakayokupeleka kwenye viwango vya juu vya mafanikio. Kumbuka, fursa yako kubwa inaweza kuwa karibu zaidi kuliko unavyofikiria, na mara nyingi inahitaji kazi ngumu na kujitolea ili uweze kuitambua na kuifanikisha.
Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa yatakayo kusaidia kuwa na kanuni za kujiwekea malengo. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.
Katika maisha, ili uweze kufanikiwa kuna kanuni ambazo unapaswa kuzifahamu na kuzifanyia kazi. Kanuni hizi ni za msingi sana kwa mtu yeyote anayetaka kufanikiwa. Hivyo, katika makala hii nitakushirikisha kanuni au sheria sita za mafanikio.
Sheria 6 Za Mafanikio
1.Sheria Ya Sababu Na Matokeo (The Law of Cause and Effect)
Sheria ya Sababu na Matokeo inasema kuwa, kwa kila tukio linalotokea katika maisha yako kuna sababu maalum. Inasema kuwa kila kitu huwa kinatokea kwa sababu, iwe unaijua sababu hiyo au la. Hakuna ajali.
Sheria ya Sababu na Matokeo inamaanisha kuwa, kuna sababu maalum za mafanikio na kuna sababu maalum za kushindwa. Kuna sababu maalum za afya na za ugonjwa. Kuna sababu maalum za furaha na za huzuni. Ikiwa kuna jambo katika maisha yako unalotaka kulifanikisha, unahitajika tu kufuatilia sababu zake na kuzirejea. Ikiwa kuna tukio katika maisha yako usilolifurahia, unahitajika kufuatilia sababu zake na kuziacha.
Sheria hii ni rahisi kiasi kwamba inawachanganya watu wengi. Wanaendelea kufanya, au kuto kufanya, mambo yanayosababisha wao kuwa na huzuni na kuchanganyikiwa, na kisha wanawalaumu wengine, au jamii, kwa matatizo yao.
Uendawazimu umefafanuliwa kama “kufanya mambo yale yale kwa njia ile ile na kutarajia kupata matokeo tofauti.” Hivyo, ili uweze kupata matokeo ya tofauti, unahitajika kufanya mambo yako kwa namna tofauti.
Kuna methali ya Kiskoti inayosema, “Ni bora kuwasha mshumaa mdogo kuliko kulaani giza.” Ni bora zaidi kukaa chini na kuchambua kwa makini sababu za shida zako kuliko kukasirika na kuzilalamikia.
Katika kitabu cha Wagalati 6:7 Biblia inasema, “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.” Sheria ya Sababu na Matokeo linaitwa Sheria ya Kupanda na Kuvuna. Inasema kuwa chochote unachopanda, ndicho utakachovuna. Pia inasema kuwa chochote unachovuna leo ni matokeo ya kile ulichopanda hapo awali. Ikiwa unataka kuvuna mavuno tofauti katika eneo lolote la maisha yako katika siku zijazo, unahitajika kupanda mbegu tofauti leo, na bila shaka, hii inahusu zaidi mbegu za akili.
Matumizi muhimu zaidi ya Sheria ya Sababu na Matokeo, au kupanda na kuvuna, ni hii: “Mawazo ni sababu na hali ni matokeo.”
Mawazo yako ndio sababu kuu ya hali ya maisha yako. Kila kitu katika uzoefu wako kimeanza na wazo la aina fulani, lako au la mtu mwingine.
Jinsi ulivyo au utakavyokuwa, ni matokeo ya jinsi unavyofikiria. Ikiwa utabadilisha ubora wa mawazo yako, utabadilisha ubora wa maisha yako. Mabadiliko katika uzoefu wako wa nje yatatokana na mabadiliko katika uzoefu wako wa ndani. Utavuna kile unachopanda.
Uzuri wa sheria hii isiyobadilika ni kwamba kwa kuikubali, unachukua udhibiti kamili wa mawazo yako, hisia zako na matokeo yako.
Kila kipengele cha mafanikio au kushindwa kwenye biashara kinaweza kuelezewa na sheria hii ya msingi. Ikiwa unapanda sababu sahihi, utavuna matokeo unayotarajia. Ikiwa unazalisha bidhaa au huduma zenye ubora ambazo wateja wanazihitaji na wako tayari kuzilipia, na kisha kuzitangaza kwa nguvu, utafanikiwa katika kuuza. Ikiwa haufanyi hivyo, hautafanikiwa.
Ikiwa unafanya kazi ya ubora wa hali ya juu na kufikia matokeo ambayo kampuni yako inayahitaji ili kukua na kustawi, utafanikiwa na utakuwa na furaha katika kazi yako. Ikiwa unawatendea wengine vizuri, watakutendea vizuri pia.
2.Sheria Ya Imani (The Law of Belief)
Sheria ya Imani inasema kuwa chochote unachokiamini, kwa hisia, kinakuwa ukweli wako. Kadri unavyoamini kwa nguvu kuwa kitu hiki ni cha kweli, ndivyo kinavyokuwa cha kweli zaidi kwako. Ikiwa unaamini kitu kwa dhati, huwezi kukifikiria kwa njia tofauti. Imani yako ko inakupa aina ya mtazamo wa maisha yako. inahariri au kukufanya kupuuza taarifa zinazoingia ambazo hazilingani na kile ulichoamua kuamini.
William James wa Harvard alisema, “Imani huunda ukweli halisi.” Katika Biblia, inasema, “Kwa kadiri ya imani yako [imani] itafanyika kwako.” Kwa maneno mengine, hauamini kile unachokiona bali unaona kile unachoamini.
Kwa mfano, ikiwa unaamini kabisa kuwa unastahili kuwa na mafanikio makubwa maishani, basi bila kujali kinachotokea, utaendelea kusonga mbele kuelekea malengo yako. Hakuna kitu kitakachokukwamisha.
Kwa upande mwingine, ikiwa unaamini kuwa mafanikio ni suala la bahati au ajali, basi utakatishwa tamaa kwa urahisi na kuvunjika moyo wakati mambo yanapokuwa hayaendi sawa kwako. Imani yako inakuandaa kwa ajili ya mafanikio au kushindwa.
Watu kwa ujumla wana mitizamo miwili ya kuangalia dunia. Mtizamo wa kwanza ni mtazamo chanya wa dunia. Ikiwa una mtazamo chanya wa dunia, kwa ujumla unaamini kuwa dunia ni mahali pazuri pa kuishi. Hivyo unakuwa na mwelekeo wa kuona mazuri kwa watu na hali, na kuamini kuwa kuna fursa nyingi karibu nawe na unaweza kuzitumia. Unaamini kuwa ingawa huenda wewe si mkamilifu, wewe ni mtu mzuri kwa ujumla. Kimsingi, wewe ni mtu mwenye matumaini.
Njia ya pili ya kuangalia dunia ni kwa mtazamo hasi wa dunia. Ikiwa una mtazamo hasi wa dunia unakuwa na mwelekeo wa kukata tamaa juu yako mwenyewe na maisha yako. Kwa ujumla unakuwa unaamini kuwa “Hauwezi kupambana na hali ya maisha yako,” na kwamba “Wenye nacho huendelea kuwa na nacho na wasio nacho huendelea kuwa maskini,” na pia unaamini kuwa, haijalishi anavyofanya kazi kwa bidii, hauwezi kufanikiwa kwa sababu mambo yamepangwa kinyume na wewe.
Watu wenye mtazamo hasi huona ukosefu wa haki, ukandamizaji na bahati mbaya kila mahali. Wakati mambo yanapokwenda vibaya kwao, kama inavyotokea mara nyingi, wanalaumu bahati mbaya au watu wabaya. Wanajiona kama wahanga. Kwa sababu ya mtazamo huu, hawajipendi wala kujiheshimu.
Hivyo, vizuizi vikubwa vya kiakili ambavyo utahitajika kuvishinda ni vile vilivyomo katika imani yako vinavyokuzuia kuchukua hatua kuhusu maisha yako. Vizuizi hivi vinakurudisha nyuma kwa kukuzuia hata kujaribu. Mara nyingi vinakufanya kuona vitu ambavyo si vya kweli kabisa.
3.Sheria Ya Matarajio (The Law of Expectations)
Sheria ya Matarajio inasema kuwa, chochote unachotarajia kwa kujiamini kinakuwa ni unabii wako mwenyewe. Kwa maneno mengine, kile unachopata sio lazima kile unachotaka maishani, bali ni kile unachotarajia. Matarajio yako yana athari kubwa na isiyoonekana ambayo inasababisha kufanikiwa au kushindwa.
Kwa njia fulani, kila mara unakuwa kama mtabiri wa maisha yako. Watu waliofanikiwa wana mtazamo wa matarajio ya kujiamini na chanya. Wanatarajia kuwa na mafanikio, wanatarajia kupendwa, wanatarajia kuwa na furaha, na mara chache wanavunjika moyo.
Watu wasiofanikiwa wana mtazamo wa matarajio hasi, wa ukosoaji na wa kukata tamaa ambao kwa namna fulani unafanya hali kutokea kama walivyotarajia.
Katika kitabu cha “Pygmalion in the Classroom,” Dkt. Robert Rosenthal wa Chuo Kikuu cha Harvard anaelezea jinsi matarajio ya walimu yanavyokuwa na athari kubwa kwenye utendaji wa wanafunzi wao. Aligundua kuwa ikiwa wanafunzi wanahisi kuwa wanatarajiwa kufanya vizuri, huwa wanajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko ambavyo wangekuwa bila matarajio hayo. Kwa hiyo, ni muhimu kuhakikisha kwamba matarajio yako yanakubaliana na kile unachotaka kuona kinatokea maishani mwako. Kuwa na matarajio mazuri kwako mwenyewe, na matarajio hayo yatakuwa na nguvu ya kubadilisha utu wako na maisha yako kwa ujumla.
4.Sheria ya Mvuto (The Law of Attraction)
Sheria ya Mvuto inasema kwamba wewe ni sumaku hai. Unavuta bila kukosea katika maisha yako watu na hali zinazolingana na mawazo yako yanayokutawala. Ndiyo maana waswahili wanasema kuwa, ” ndege wa aina moja huruka pamoja.” Kila kitu katika maisha yako umekivuta mwenyewe kutokana na mawazo yako.
Marafiki zako, familia yako, mahusiano yako, kazi yako, matatizo yako, na fursa zako vyote vimevutwa kwako kutokana na njia yako ya kawaida ya kufikiri katika kila eneo.
Unapoangalia kila kipengele cha maisha yako, chanya au hasi, utaona kwamba ulimwengu wako wote umeutengeneza mwenyewe. Na kadiri unavyoweka hisia zaidi kwenye wazo, ndivyo kasi ya mtetemo itakuwa kubwa zaidi na ndivyo utakavyovuta watu na hali zinazolingana na wazo hilo katika maisha yako kwa haraka zaidi.
Utaona kuwa, sheria hii huwa inafanya kazi kila wakati katika maisha yako. Kwa mfano, Unamfikiria rafiki yako na mara hiyo hiyo anakupigia simu. Unaamua kufanya jambo fulani na mara tu baada ya hapo unaanza kupata mawazo na msaada kuhusiana na jinsi utakavyofanikisha jambo hilo. Unakuwa kama sumaku inayovuta vipande vya chuma.
Watu wengi wanajizuia wenyewe kufanikiwa kwa sababu hawajui jinsi ya kutoka walipo hadi wanapotaka kwenda. Lakini kwa sababu ya Sheria ya Mvuto, si lazima uwe na majibu yote kabla hujaanza. Mradi tu unaelewa vizuri unachotaka na aina ya watu unaotaka kuwa nao, utawavuta katika maisha yako.
Watu wenye furaha wanaonekana kuvutia watu wengine wenye furaha katika maisha. Mtu aliye na ufahamu wa ustawi anaonekana kuvutia mawazo na fursa za kutengeneza pesa. Wauzaji wanaoaminika na wenye msisimko huvutia wateja wakubwa na bora zaidi. Wafanyabiashara chanya huvutia rasilimali, wateja, wasambazaji na mabenki wanayohitaji kujenga biashara zenye mafanikio. Sheria ya Mvuto inafanya kazi kila mahali na wakati wote.
5.Sheria ya Uwiano (The Law of Correspondence).
Sheria ya Uwiano ni mojawapo ya sheria muhimu zaidi, na kwa namna nyingi ni sheria ya muhtasari inayofafanua sheria nyingine nyingi. Inasema kuwa, “Jinsi ulivyo ndani, ndivyo ulivyo nje.” Sheria hii inamaanisha kwamba, ulimwengu wako wa nje ni taswira ya ulimwengu wako wa ndani. Sheria hii inafafanua kuwa, unaweza kujua kinachoendelea ndani yako kwa kuangalia kinachoendelea kukuzunguka wewe.
Katika Biblia, kanuni hii inaelezwa kwa maneno haya, “Kwa matunda yao, mtawatambua.” Kila kitu katika maisha yako ni kutoka ndani kwenda nje. Ulimwengu wako wa nje ni udhihirisho unaolingana na ulimwengu wako wa ndani wa mawazo na hisia.
Ulimwengu wako wa nje wa mahusiano unaendana na mtu uliye ndani, utu wako wa kweli wa ndani. Ulimwengu wako wa nje wa afya unaendana na mitazamo yako ya ndani ya akili. Ulimwengu wako wa nje wa mapato na mafanikio ya kifedha unaendana na ulimwengu wako wa ndani wa mawazo na maandalizi. Jinsi ambavyo watu wanakuitikia na kuingiliana na wewe inaakisi mitazamo na tabia yako kwao.
Mwanafalsafa Mjerumani Goethe alisema, “Lazima uwe kitu ili uweze kufanya kitu.” Lazima ubadilike wewe mwenyewe. Lazima uwe mtu tofauti ndani kabla ya kuona matokeo tofauti nje.
6.Sheria ya Usawa wa Akili (The Law of Mental Equivalency)
Sheria ya Usawa wa Akili inajulikana pia kama Sheria ya Akili na inaweza kufikiriwa kama ufafanuzi wa sheria zilizotangulia. Kimsingi, inasema kwamba, Mawazo yako, unayoyafikiria kwa undani na kuyarudia yakiwa na hisia, baadaye huwa yanakuwa ukweli wako. Karibu kila kitu ulicho nacho katika maisha yako kimeundwa na mawazo yako mwenyewe, kwa ubora au ubaya.
Kwa maneno mengine, mawazo ni vitu. Yanachukua maisha yako mwenyewe. Kwanza unakuwa nayo, kisha yanakumiliki. Unatenda kwa namna inayolingana na kile unachofikiria mara nyingi zaidi. Hatimaye, unakuwa kile unachofikiria. Na ukibadilisha mawazo yako, unabadilisha maisha yako.
Kila kitu kinachotokea katika maisha yako kwanza huanza kutokea katika namna ya wazo. Hii ndio sababu tafakari ni sifa muhimu ya wanaume na wanawake waliofanikiwa.
Nguvu ya Kufikiri Chanya
Unapoanza kufikiri kwa njia chanya na kwa kujiamini kuhusu vipengele vikuu vya maisha yako, unachukua udhibiti wa kile kinachotokea kwako. Unaleta maisha yako katika maelewano na sababu na athari. Unapanda sababu chanya na kuvuna athari chanya. Unaanza kuamini zaidi katika nafsi yako na uwezo wako. Unatarajia matokeo chanya zaidi. Unavuta watu na hali chanya, na hivi karibuni maisha yako ya nje ya matokeo yataanza kulingana na ulimwengu wako wa ndani wa mawazo ya kujenga.
Mabadiliko haya yote yanaanza na mawazo yako. Badilisha mawazo yako na maisha yako yatabadilika.
Nimatumaini yangu kuwa umenufaika na makala hii ya sheria 6 za mafanikio. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.