Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

Katika maisha, kujitazama nyuma na kutafakari mafanikio uliyoyapata ni jambo muhimu sana. Pia ni vyema kuzingatia changamoto ulizokutana nazo na jinsi zilivyokusaidia kukua. Kitendo cha kufikiria uzoefu wako wa zamani, mafanikio, na mafunzo uliyoyapata, kutaweza kuamua malengo unayotarajia kufikia siku za usoni. Iwe umeweka malengo ya juu zaidi au umelenga kubaki thabiti na malengo yako, unatakiwa kuepuka mambo na tabia fulani ili uweze kufanikiwa. Katika makala hii nitakushirikisha mambo 10 ya kuacha ili ufanikiwe siku za usoni:

Mambo 10 Ya Kuacha Ili Ufanikiwe Siku Za Usoni.

1. Visingizio:
Jifunze kuwajibika. Kuwa na malengo na ujikite kufanyia kazi malengo yako bila kuwa na visingizio. Kila kisingizio kinakurudisha nyuma kufikia lengo lako.

2. Kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja:
Ingawa inaweza kuonekana kuwa kama suluhisho la ufanisi, kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja kunaweza kuharibu malengo yako. Fikiria kufanya kazi moja kwa wakati mmoja.

3.Kusema ndiyo kwa mambo yasiyosaidia malengo yako:
Mara nyingine tunajisikia lazima tuseme ndiyo. Lakini kusema ndiyo kwa mambo ambayo hayasaidii malengo yako kunaweza kukurudisha nyuma. Jifunze kusema hapana kwa mambo yasiyo na maana ambayo hayachangii kwenye mafanikio yako.

4. Epuka watu wenye sumu:
Kuna wakati utakutana na watu wasio na nia njema na mafanikio yako. Ikiwa hawakusaidii kufikia malengo yako, waache. Kuacha uhusiano na watu wenye mawazo hasi kunaweza kuwa kugumu, lakini kutakusaidia kufanikiwa baadaye.

5. Muda wa kutumia kwenye mitandao ya kijamii:
Kwa wastani, mtu hutumia dakika 145 kwa siku, zaidi ya masaa 2 kwenye mitandao ya kijamii. Kudhibiti muda wako kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kukuepushia kupoteza muda na badala yake kufanya vitu vingine vyenye tija.

6.Kutothamini kile ulichonacho sasa:
Thamini vitu ulivyonavyo sasa. Kudharau vitu ulivyonavyo kunaweza kuzuia kufikia malengo yako. Kuwa na shukrani kwa kila unachokuwa nacho katika maisha yako. Kujifunza kushukuru imegundulika kuwa kunaimarisha mtazamo chanya na afya ya akili kwa ujumla. Hata kama kuna nyakati ambazo hauna furaha, unapothamini mafanikio yako unaongeza motisha ya kupiga hatua zaidi kuelekea kwenye mafanikio yako. Hivyo, unapaswa kuacha tabia hii ili uweze kufanikiwa.

7.Kutafuta idhini kutoka kwa watu wengine.
Ikiwa unangoja mtu akuruhusu kufanikiwa, utangoja milele. Usisubiri mtu akwambie unaweza kufanya nini. Badala yake, onyesha uwezo wako. Jitwike jukumu la maisha yako na malengo yako wewe mwenyewe. Jiruhusu kufanikiwa.

8. Uvivu.
Kama vile kutoa visingizio, kuchelewesha kazi pia kunazuia kufikia malengo yetu. Badala ya kusubiri kufanya kazi yako hadi dakika ya mwisho, au kuendelea kuahirisha, jichukulie kuwajibika na kufanya kazi kwa bidii.Tunaona mafanikio tunapochukua hatua na kufanya jambo.

9.Kuamini malengo yako ni makubwa au madogo sana.
Malengo yako ni tofauti kabisa na ya mtu mwingine, hivyo unapaswa kuacha kulinganisha malengo. Badala yake, jikite katika jinsi unavyoweza kufikia malengo yako. Usipoteze muda kwa kufikiria sana au kuchambua mambo kama vile ukubwa au udongo wa malengo yako. Anza tu kuyatimiza.

10. Kulinganisha maisha yako na ya wengine.
Kama vile malengo yanavyotofautiana na ya mtu mwingine, maisha yako pia ni tofauti kabisa na ya mtu mwingine.

Rais Theodore Roosevelt aliwahi kusema, Kujilinganisha na wengine ni mwizi wa furaha. Tunapojilinganisha na wengine, tunajihisi duni na tusiofaa. Tunapogundua kuwa tunaweza vya kutosha na tuna njia za kufikia malengo yetu, hatutajisikia vibaya kuhusu safari yetu ya mafanikio. Tutagundua kuwa kujilinganisha na wengine kunatuzuia tu kufikia safari yetu.

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa kuhusu mambo 10 ya kuacha ili ufanikiwe siku za usoni. Kama una swali au maoni usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

    Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni: Makosa 7 Ya Kuepuka.

    Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni.

    Ni rahisi sana kuanzisha biashara mtandaoni. Lakini, ikiwa hutafuata njia sahihi hutaweza kamwe kufanikiwa. Watu wengi wanaoanzisha biashara mtandaoni hukata tamaa na kuachana nazo baada ya muda mfupi sana. Mimi sitaki wewe uwe miongoni mwao.
    Katika makala hii nitakushirikisha makosa 7 ya kuepuka ili uweze kuwa na biashara yenye mafanikio mtandaoni. Unapoepuka makosa haya utakuwa na nafasi kubwa zaidi ya kufanya biashara yako mtandaoni kwa mafanikio makubwa.

    Makosa 7 Ya Kuepuka Ili Kuwa Na Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni.

    1.Kutoichukulia Biashara Yako Mtandaoni Kama Biashara Halisi.
    Watu wengi wanaoanzisha biashara mtandaoni hufanya hivyo kwa kujaribu. Wamesikia madai mengi kuhusu jinsi watu wanavyoweza kupata utajiri kwa urahisi mtandaoni. Ni kweli, gharama ni ndogo sana kuanzisha biashara mtandaoni. Unahitaji tu kuwa na blog yako ambapo gharama yake ni ndogo sana.

    Kutokana na gharama kuwa ndogo, watu wengi hutamani kuanzisha biashara mtandaoni. Lakini baada ya kugundua kuwa siyo kazi rahisi kama walivyokuwa wanafikiria, hukata tamaa na kuachana na biashara ya mtandaoni.

    Ikiwa hutaichukulia biashara yako ya mtandaoni kama biashara halisi basi uwezekano wa kushindwa ni mkubwa zaidi. Ni kweli huna haja ya kuwekeza pesa nyingi lakini unahitajika kuwekeza hisia, nguvu na akili yako yote katika biashara yako ya mtandaoni kama zilivyo biashara zingine.

    Kujenga biashara mtandaoni yenye mafanikio kunahitaji kufanya kazi kila siku. Unahitajika kujifunza kufanya mambo sahihi na kutangaza biashara yako mtandaoni wakati wote.

    Ikiwa biashara yako ya mtandaoni utaichukulia tu kama hobi, basi nafasi zako za mafanikio zitapungua sana. Hili ni kosa kubwa miongoni mwa makosa ambayo watu wengi huwa wanafanya.

    Fikiria kwamba umewekeza akiba yako yote katika duka lako la mjini au mtaani kwako. Je, ungeichukulia biashara yako kama tu ni hobi? Hapana usingefanya hivyo. Kwa hiyo, fikiria kwamba umewekeza akiba yako yote ya maisha katika biashara yako mtandaoni. Kutakuwa na siku ambapo mambo yataenda mrama na biashara yako ya mtandaoni haitaenda kama ulivyokusudia. Unahitaji ustahimilivu na kujitolea kukabili matatizo haya na kusonga mbele na hivyo kujenga biashara yenye mafanikio mtandaoni. Kuchukulia biashara yako ya mtandaoni kama biashara halisi kutakusaidia kupata mafanikio.

    2.Kutokuwa na mpango.
    Hivi unafikiri ni watu wangapi wanaoanzisha biashara mtandaoni wanaweka mpango kwa ajili ya biashara zao? Jibu ni wachache sana. Hakuna anayejua ni biashara ngapi mtandaoni zinashindwa kila mwaka, lakini ni nyingi. Wamiliki wengi wa biashara mpya mtandaoni hawaweki malengo au kuwa na mpango. Kisha wanashangaa biashara zao zinaposhindwa kabisa.

    Ikiwa unaanzisha biashara mtandaoni, weka lengo. Lengo rahisi la kuweka ni lile la kifedha. Fikiria kiasi gani unataka biashara yako ya mtandaoni ikuzalishie katika miezi 12 ya kwanza na kisha geuza kuwa lengo lako la kifedha.

    Biashara yako ya mtandaoni ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Kizuizi pekee ni wewe. Tumia mchakato wa kuweka malengo wa SMART kuweka malengo yako. SMART ni ufupisho wa maneno kadhaa kama ifuatavyo:

    • Specific– lengo lako lazima liwe maalum, kwa mfano, biashara yangu ya mtandaoni itazalisha sh 1,000,000 mwaka ujao.
    • Measurable – lazima uweze kupima jinsi unavyosonga mbele kuelekea lengo lako. Bahati nzuri, kuna zana nyingi za kupima mafanikio ya biashara yako mtandaoni.
    • Achievable– Lengo lako lazima liwe linalofikika. Ni vigumu sana kuingiza dola milioni katika mwaka wako wa kwanza. Hivyo weka lengo unaloweza kulifikia.
    • Realistic– fikiria muda ulionao na rasilimali nyingine kama vile pesa.
    • Timed– lazima uweke muda kwa lengo lako, kama vile mwaka mmoja. Malengo yasiyo na kikomo hayana maana.
      Baada ya kuweka lengo lako, unahitajika kuweka mpangokazi wa kufikia lengo lako. Unatakiwa kuwa na orodha ya kazi za kila siku ambazo utazifanya ili kusonga mbele kutimiza lengo lako. Kwa hiyo fikiria kuhusu majukumu makubwa ya mpangokazi wako na kisha uyavunje kuwa majukumu madogomadogo ya kila siku. Kwa kufanya hivyo utakuwa umeepuka makosa ambayo watu wengi hufanya na hivyo kuwafanya wakate tamaa kwenye biashara ya mtandaoni.

    Mpangokazi rahisi unaweza kuwa:

    1. Chagua mada (niche) na aina ya biashara yako ya mtandaoni.
    2. Kutengeneza blog.
    3. Kuweka maudhui.

    Unaweza kuanza leo kwa kuchagua niche unayotaka kuingia.

    3. Kutokuchagua Niche Sahihi.

    Kuchagua niche sahihi ni muhimu sana katika kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni. Usifanye makosa katika hili. Ikiwa utakosea, unaweza kutumia muda mwingi, jitihada, na pesa bila kupata mafanikio makubwa. Kuna maelfu ya niche, lakini sio zote zinafaa kwa biashara mtandaoni.

    Kwa nia njema, ikiwa utaanza biashara mtandaoni katika niche unayoipenda, utakuwa na motisha zaidi kufanya kazi kwa bidii na hivyo kupata mafanikio makubwa kwa haraka.

    Hata hivyo, jambo hili linaweza kuwa na matokeo mazuri ikiwa niche unayoipenda ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Labda unapenda kushona nguo za kawaida, lakini je, kuna watu wengi watakaonunua nguo hizo?

    Kuna mambo mawili unayopaswa kuzingatia unapochagua niche:

    Je, kuna mahitaji? Tafuta kujua kama kuna watu wanaotafuta bidhaa au huduma katika niche hiyo. Unaweza kutumia Google kujua idadi ya utafutaji wa maneno muhimu katika niche unayotaka kuanzisha biashara mtandaoni. Kadri idadi ya utafutaji inavyokuwa kubwa, ndiyo kiashiria kuwa niche yako ni maarufu na inahitajika.

    Je, kuna pesa katika niche hiyo? Fanya utafiti kwenye Google kwa kutumia maneno muhimu ya niche yako. Je, kuna matangazo mengi kwenye ukurasa wa kwanza wa matokeo ya utafutaji? Ikiwa ni ndiyo, hii inaonyesha kuwa kuna fursa ya kupata pesa.
    Ikiwa bado una shaka kuhusu kuchagua niche sahihi, chagua ile unayohisi itakuwezesha kupata pesa. Usijali kama sio mtaalamu wa niche hiyo sasa. Unaweza kujifunza na kuwa bingwa baadaye. Ni bora kufanya hivyo kuliko kuchagua niche isiyo sahihi ambayo unaijua vizuri lakini haiwezi kukupatia kipato.

    4.Kutokuchagua mfumo sahihi wa biashara mtandaoni:

    Kuna mifumo kadhaa ya biashara mtandaoni ambayo unaweza kuchagua. Baadhi ya mifumo hii ni:

    • Uuzaji wa Washirika (Affiliate marketing): Hapa unatangaza bidhaa za makampuni mbalimbali kwa lengo la kupata gawio baada ya kupata wateja na kufanya mauzo.
    • Kuuza bidhaa na huduma zako mwenyewe: Hapa unakuwa ukiuza bidhaa au huduma zako.
    • Duka lako la e-commerce: Kuanzisha duka lako la mtandaoni na kuuza bidhaa.

    Je, una ujuzi maalum unaohitajika? Baadhi ya huduma za kujitegemea zinazohitajika sana ni:

    • Kuandika makala.
    • Ubunifu wa picha (kama vile nembo) na kadhalika.
    • kutengeneze Programu za simu na computer.
    • kutengeneza blog na wavuti (websites)
    • Kutafuta masoko kwenye mitandao ya kijamii na kadhalika.

    Ikiwa una ujuzi wa aina hizi, unaweza kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni kwa kuuza huduma zako na kupata pesa mtandaoni. Kumbuka kuwa utahitajika kuwa na nidhamu ili kutoa kazi bora kwa wateja wako kwa wakati unaostahili.

    Mifano yote hii ya biashara mtandaoni ina uwezo wa kukuingizia pesa nyingi. Chagua ile inayokufaa na endelea nayo. Kumbuka kujifunza kuhusu mifumo hii. Usibadilishebadilishe biashara mtandaoni, kwani hautapata matokeo unayoyategemea.

    5. Ugonjwa Wa Vitu Vinavyong’aa (Shiny Object Syndrome).
    Mara nyingi utasikia msemo “nyasi ni za kijani zaidi huko.” Hii inamaanisha kuwa kuna fursa bora za mafanikio ya biashara mtandaoni mahali pengine kuliko hapa. Tunaiita ” Shiny Object Syndrome – ugonjwa wa vitu vinavyong’aa.”

    Unapochagua aina ya biashara mtandaoni, kutakuwa na watu wanaokwambia kuwa umefanya uchaguzi mbaya na unapaswa kubadili biashara yako na kununua mafunzo yao ili ujifunze jinsi ya kupata utajiri kutoka kwao.

    Watu wengi wanaochagua niche wanakabiliwa mara kwa mara na vitu vinavyong’aa vipya vinavyowadanganya. Kuna kozi na programu mpya zinazotolewa kila siku ambazo zote zitakuambia kuwa unahitaji kuacha unachofanya sasa na kufuata mwelekeo wao.

    Simaanishi kuwa usiwekeze katika mafunzo zaidi kwenye biashara uliyoichagua. Unapaswa kujifunza kila kitu unachoweza kuhusu biashara yako na kuwa tayari kujaribu njia mpya ili kufanikiwa. Lakini unachopaswa kuepuka ni kubadili mwelekeo kabisa kwa sababu nyasi zinaonekana kijani zaidi upande mwingine.

    6. Kutokupata watembeleaji wa kutosha.

    Ikiwa ungeulizwa kwa nini biashara nyingi mtandaoni zinashindwa, sababu kuu ingekuwa nini kwa maoni yako? Je, ni ukosefu wa maslahi? Ukosefu wa rasilimali? Kutokuwa na muunganisho bora wa intaneti? Kwa maoni yangu, jibu halitakuwa lolote kati ya haya. Jibu ni: Kutokupata watembeleaji wa kutosha!

    Ikiwa hutapata watembeleaji walengwa kwenye ofa zako basi hutaweza kupata pesa mtandaoni. Unaweza kuwa unapromoti ofa ya kawaida na bado ukapata pesa nzuri kutokana nayo ikiwa utavutia wageni wa kutosha kwenye ofa hiyo.

    Kwa upande mwingine, unaweza kuwa na ofa bora zaidi duniani, lakini ikiwa hautavutia watembeleaji walengwa wa kutosha basi hutafanya mauzo mengi. Watembeleaji ni sehemu muhimu zaidi ya biashara yenye mafanikio yoyote mtandaoni bila kujali aina ya biashara mtandaoni uliyoichagua.

    Ikiwa wewe umejiajiri mtandaoni na hakuna mtu anayejua kuhusu huduma zako, basi biashara yako mtandaoni itashindwa. Kama mfanyabiashara mshirika (affiliate ) ikiwa hautavutia wageni wa kutosha kwenye ofa unazopromoti basi hutapata kamisheni yoyote. Bila watembeleaji walengwa kwenye duka lako la biashara mtandaoni hutauza chochote – na hivyo ndivyo inavyokuwa.

    Mara tu unapoweka biashara yako mtandaoni unahitajika kutumia muda mwingi kuitangaza. Kuna njia kadhaa unazoweza kufanya hivyo. Ikiwa hutaki kutumia pesa unaweza kuitangaza biashara yako kwa kushea kwenye mitandao ya kijamii na kadhalika.

    Ikiwa una pesa kidogo za kuwekeza basi unaweza kutumia matangazo ya kulipia kuitangaza biashara yako mtandaoni. Unaweza kununua wageni wa kulipia matangazo ya Google (Google ads) au matangazo ya facebook (facebook ads). Ninapendekeza ufanye mchanganyiko wa matangazo ya bure na matangazo ya kulipia.

    Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kutafuta watembeleaji kwenye biashara yako ya mtandaoni. Hakuna watembeleaji inamaanisha hakuna biashara. Kwa hiyo fanya kila jitihada kuitangaza biashara yako mtandaoni wakati wote. Wageni wengi zaidi unapopata ndivyo unavyoweza kuwa na biashara yenye mafanikio na hivyo kupata pesa zaidi.

    7.Kutokupima na kutathimini maendeleo ya biashara yako ya mtandaoni.

    Moja ya faida kubwa ambayo biashara ya mtandaoni inayo ikilinganishwa na biashara ya kawaida ni kwamba unaweza kupima karibu kila kitu kwa wakati halisi. Lakini wamiliki wengi wa biashara mtandaoni hupuuza hili au hawalizingatiii vya kutosha.

    Ikiwa unataka kujua ni wageni wangapi walitembelea tovuti yako wiki iliyopita unaweza kutumia programu kama Google Analytics kukujulisha hili. Pia unaweza kujua wageni wako walitoka wapi na ni kurasa zipi za tovuti yako walizotembelea.

    Ni muhimu pia kujua walikaa muda gani kwenye tovuti yako. Watembeleaji wako wanapaswa kukaa kwa muda mrefu iwezekanavyo. Ikiwa wanaondoka haraka basi unahitajika kuchunguza kwa nini na kurekebisha tatizo hili.

    Huwezi kusimamia kile usichoweza kupima. Na pia kwenye biashara ya mtandaoni unaweza kupima vitu vingi kwa hiyo tumia fursa hii. Itakuambia ni kampeni zipi zinazofanya kazi na pia itaangazia maeneo ya tovuti yako ambayo unahitajika kuyafanyia maboresho. Taarifa hii ni ya thamani kwa hiyo hakikisha unaitumia.

    Nimatumaini yangu kuwa umenufaika kiasi cha kutosha na makala hii ya Makosa 7 Ya Kuepuka Ili Kuwa Na Biashara Yenye Mafanikio Mtandaoni. Nimeelezea kwa undani makosa 7 ambayo wamiliki wapya wa biashara mtandaoni hufanya ambayo yanawazuia kuwa na mafanikio. Sasa kwa kuwa unafahamu makosa haya unahitajika kujizatiti ili uweze kuyaepuka na hivyo kukuza biashara yako.

    Kama una swali lolote kuhusiana na jinsi ya kuanzisha biashara yenye mafanikio mtandaoni usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazofuata.

    Kanuni 9 Za Kutengeneza Utajiri : Kitabu The Millionaire Next Door.

    Kanuni 9 Za Kutengeneza Utajiri : Kitabu The Millionaire Next Door.

    Kuna dhana iliyojengeka miongoni mwa watu wengi kuwa mamilionea wanaishi maisha ya anasa. Wanasafiri kwa ndege binafsi, wanaendesha magari ya kifahari, wanavaa nguo za mitindo mipya kila wakati na pia wanaishi katika nyumba za gharama kubwa. Ukweli ni tofauti kabisa. Thomas J. Stanley na William D. Danko wanadai kugundua siri kubwa zaidi ya mamilionea halisi wa Marekani. Katika kitabu chao cha ‘The Millionaire Next Door’, wanafichua ugunduzi wao kuhusu mtindo rahisi wa maisha ya mamilionea wa Marekani. Mtindo ambao hata wewe ukiweza kuishi utaweza kutengeneza utajiri.

    Kitabu cha ‘The Millionaire Next Door’ kina msingi mmoja mkuu: hata wewe pia unaweza kuwa na mafanikio ya kifedha ikiwa utaepuka kutumia zaidi ya unavyopata, kujitoa kikamilifu katika kuwekeza, na kupanga mipango ya fedha zako vizuri.

    Kuhusu Thomas J. Stanley na William D. Danko.

    Thomas J. Stanley (1944-2015) alikuwa ni Mmarekani mwandishi na mfanyabiashara. Aliandika na kushiriki kuandika vitabu kadhaa kuhusu tabaka tajiri la Marekani. Orodha hiyo inajumuisha kitabu kilichouza sana cha The Millionaire Next Door, ambacho alikiandika kwa kushirikiana na William D. Danko.

    Stanley alipata shahada ya uzamivu katika utawala wa biashara kutoka Chuo Kikuu cha Georgia. Baada ya kuhitimu, alihudumu katika nafasi mbalimbali za uongozi katika makampuni mbalimbali. Pia alikuwa mshauri mkuu katika Kampuni ya Datapoint iliyoanzishwa mwaka 1968. Datapoint ilikuwa kampuni ya teknolojia iliyokuwa ikitengeneza terminali za kompyuta. Baadaye katika kazi yake, alitoa mihadhara ya masoko katika vyuo vikuu vya Tennessee na Georgia.

    Dkt. William D. Danko ni mwanachama wa kitivo katika Chuo Kikuu cha Jimbo la New York (State University of New York). Katika miongo mitatu iliyopita, amesoma tabia ya watumiaji na jinsi ya kutengeneza utajiri kwa kina (consumer behavior and wealth formation). Mbali na The Millionaire Next Door, pia ameshiriki kuandika kitabu cha Richer Than a Millionaire: A Pway to True Prosperity. Dkt. Danko ni mtafiti aliyechapishwa nchini Marekani, Australia, Canada, Ujerumani, Poland, na Uswisi. Alimaliza Ph.D. yake katika chuo cha Rensselaer Polytechnic Institute’s (RPI) Lally School of Management.

    Stanley na Danko walitumia miaka 20 kusoma jinsi Wamarekani waliofanikiwa walivyopata utajiri na jinsi wanavyotumia pesa zao. Walishirikisha takriban watu 1,000, ambao walijibu maswali 200 kila mmoja. Waandishi wengi hutumia muda mwingi kusoma na kuandika jinsi ya kupata utajiri. Lakini Stanley na Danko walilenga kuelewa jinsi matajiri wanavyoishi maisha yao tofauti na Wamarekani wa kawaida. Stanley alifariki katika ajali ya gari mwaka 2015.

    Karibu sasa tuangalie kanuni za kutengeneza utajiri kutoka kwenye kitabu hiki cha The Millionaire Next Door.

    Kanuni 9 Za Kutengeneza Utajiri : Kitabu Cha The Millionaire Next Door.

    1: Mamilionea Hawatumii Kiasi Kikubwa cha Pesa Wanachopata.
    Kama milionea, unaweza kuwa umewaza kuendesha gari la kisasa na kunywa mvinyo wa bei kubwa. Lakini kwa uhalisia, mamilionea wengi ni waangalifu katika matumizi.

    “Watu wengi wanaoishi katika nyumba za gharama kubwa na kuendesha magari ya anasa, kiuhalisia hawana utajiri mkubwa. Tuligundua kitu cha ajabu zaidi kwenye utafiti wetu: Watu wengi wenye utajiri mkubwa hawaishi hata katika maeneo ya kifahari.” – Thomas J. Stanley

    Hii sio dhana ambayo utaisikia kwenye vyombo vya habari kuhusu mamilionea. Badala yake, vyombo vya habari vinaonyesha maudhui yanayosifu matumizi makubwa ya pesa na maisha ya kifahari.

    “Sekta ya matangazo na Hollywood wamefanya kazi nzuri ya kutufanya tuamini kwamba utajiri na matumizi makubwa ya pesa vinakwenda sambamba.” – Thomas J. Stanley

    Lakini, ikiiwa unataka kufikia mafanikio ya kifedha na kutengeneza utajiri, usifuatilie maisha yasiyokuwa na uhalisia kutoka kwenye vyombo vya habari. Lazima upange matumizi yako na ujifunze jinsi ya kuokoa pesa unapoanza kupata pesa zaidi ya zile unazozihitaji.

    “Kwa kipato chochote ulichonacho, ishi chini ya kipato chako. Mamilionea mara nyingi hutengeneza utajiri kwa kutotumia mali nyingi kwenye makazi yao ya kwanza, hivyo kuwafanya wawe na uwezekano mdogo wa kuishi katika maeneo tajiri” – Thomas J. Stanley

    Ili uweze kuwa millions siyo lazima uwe msomi au mtaalamu wa teknolojia. Mara nyingi mamilionea ni watu wanaoishi maisha ya kawaida kabisa jirani yako. Wanatumia kila dola kununua bidhaa zinazoongeza thamani katika maisha yao. Mamilionea pia sio lazima wamiliki magari ghali zaidi. Badala yake, wanaweza hata kumiliki magari ya kawaida ya mkono wa pili (second hand).

    Jinsi Mamilionea Wanavyoishi Maisha Yao Kwa Uangalifu.
    Bajeti madhubuti na kuishi maisha ya uangalifu ni muhimu sana katika kujenga utajiri wako. Kupata mshahara mkubwa haimaanishi kuwa wakati wewe ni tajiri. Hata kama wewe ni miongoni mwa wafanyakazi wanaolipwa vizuri zaidi, kodi itachukua sehemu kubwa ya kipato chako. Baada ya kupunguza gharama za maisha, utakuwa umebakiwa na pesa kidogo za kujikimu hadi mshahara ujao.

    Lakini huna haja ya kupata mamilioni ili kuokoa pesa na kuweka akiba kwa ajili ya siku zijazo. Kanuni rahisi ya utajiri ni kuokoa kiasi kikubwa cha pesa iwezekanavyo unapokuwa umepata pesa zaidi kuliko unazohitaji kuishi.

    “Jambo la msingi kabisa la Kutengeneza utajiri ni kuweka ulinzi, na ulinzi huu unapaswa kuwa umejikita kwenye bajeti na mipango.” – Thomas J. Stanley

    Mkakati muhimu ambao mamilionea hutumia kwa uangalifu ni kuendeleza mazingira ya kuishi maisha ya kawaida. Ingawa wanaweza kumudu chakula cha dola 200, wanachagua mlo wa dola 50. Badala ya kutumia gari la gharama kubwa, huchagua usafiri wa gharama ndogo ili kuokoa pesa.

    2: Mamilionea Wanatenga Muda na Nguvu Katika Kutengeneza Utajiri
    Subira, shauku, na uvumilivu ni thamani muhimu miongoni mwa watu waliojilimbikizia utajiri. Stanley na Danko waligundua kwamba mamilionea huwa wanawekeza muda na nguvu katika kupanga mustakabali wao wa kifedha. Wanazingatia kujenga uchumi wao wa kifedha kuliko vitu vingine maishani. Mara nyingi kutengeneza utajiri huchukua miaka, ikiwa sio miongo.

    “Kipato ni kile unachobeba kupeleka nyumbani leo. Utajiri ni kile unachokuwa nacho kesho, kesho kutwa na siku inayofuata” – Thomas J. Stanley

    Kinyume na imani inayoenezwa na vyombo vya habari, kujenga utajiri sio tukio la haraka au la mara moja. Badala yake, ni la polepole, la mfumo na linalochukua muda kukomaa.

    Kuwa na kipato cha juu sio sababu ya moja kwa moja ya kutengeneza utajiri kwa haraka. Wapokeaji wa kipato cha juu mara nyingi wanagawanywa katika makundi mawili ambayo ni Walimbikizaji wa utajiri (Prodigious Accumulators of Wealth (PAW)) na walimbikizaji duni wa utajiri (Under Accumulators of Wealth (UAW))

    Walimbikizaji wa Utajiri (PAWs) ni mabingwa wa kuokoa pesa na kukuza utajiri. Wana thamani ya utajiri mara nne zaidi ya watu wengi wenye kipato kama chao. Wanazingatia katika kufikia uhuru wa kifedha.
    Walimbikizaji Duni wa Utajiri (UAWs) wanafanya chini ya wastani katika kuokoa pesa. Hivyo, wako nyuma sana ya PAWs licha ya kuwa na kipato kama chao.

    Bahati mbaya, UAWs wengi ni wataalamu wenye elimu ya juu wanaopata kipato cha juu. Hata hivyo, wanatumia pesa zao kudumisha maisha ya anasa. Pia wanajaribu kudumisha viwango vya maisha ya juu ili kujionyesha kwa jamii inayowazunguka.

    “Ni vipi watu wenye elimu nzuri, wenye kipato cha juu wanaweza kuwa wajinga kiasi hicho kuhusu pesa? Kwa sababu kuwa na elimu nzuri, kupata kipato cha juu haimaanishi moja kwa moja kuwa na uhuru wa kifedha. Kutengeneza utajiri na kuwa na uhuru wa kifedha Inahitaji kupanga na kujinyima.” – Thomas J. Stanley

    3: Mamilionea Wanapima Uhuru wa Kifedha Kuliko Hali ya Kijamii ya Anasa.
    Tunaishi katika ulimwengu wa mitandao ya kijamii ambapo watu mara nyingi wana hamu ya kuonyesha maisha ya kifahari kwa ajili ya umaarufu. Ikiwa jambo hili ni udhaifu ulio nao, hauko peke yako. Kwa bahati mbaya, kuzuia hamu hii inaweza kuwa ngumu. Ili kuonekana tajiri katika ulimwengu wa nje, vijana wengi hujitahidi kutumia pesa nyingi kuliko uwezo wao ili kujionyesha mitandaoni.

    Ni mikopo ndiyo inayoendesha maisha ya anasa ya wafu wengi leo, sio mapato halisi. Watu wanataka kuwa na nguo za wabunifu maarufu na kukodisha magari ya starehe. Hata hivyo, nguvu zao za kifedha haziruhusu hilo. Kwa kufuata maisha haya ya anasa, huwezi kuwa na amani inayotokana na uhuru wa kifedha. Badala yake, kwa ndani kabisa, mbali na macho ya umma, utakuwa unajua kuwa haujafanikiwa kifedha.

    “Kuna uhusiano wa kinyume kati ya muda uliotumika kununua vitu vya anasa kama magari na nguo na muda uliotumika kupanga mustakabali wa kifedha wa mtu.” – Thomas J. Stanley

    Mamilionea bora wa Marekani hawahisi kuwa na shinikizo la kuthibitisha kwamba wanaishi maisha ya anasa kwa ulimwengu. Badala yake, wanapendelea kupata uhuru wa kifedha kuliko kuonekana matajiri. Wanaona uendelevu wa kifedha kama tuzo kuu ya kukua na kutengeneza utajiri.

    “Ili kujenga na kudumisha utajiri, itakuwa muhimu kwako kushughulikia usimamizi wote wa kifedha – matumizi, kuweka akiba, kuzalisha mapato, kuwekeza – kwa njia tofauti, kwa nidhamu zaidi kuliko mtu yeyote mwingine anayekuzunguka” – Thomas J. Stanley

    Kitabu cha The Millionaire Next Door kinaonyesha kwamba uhuru wa kifedha unachangia ustawi. Mamilionea wana furaha na kujiamini zaidi katika uendelevu wao wa kifedha wa sasa na wa baadaye. Wana malengo na madhumuni wazi ya muda mfupi na mrefu, yakiwaruhusu kupanga na kubajeti mahitaji yao kulingana na vipaumbele.

    Kila mtu anathamini ustawi wa familia zao kuliko vitu vingine. Zingatia uhuru wa kifedha na epuka dhana ya mitandao ya kijamii ya “tajiri.” Kwa njia hii, unaweza kufurahia uhuru wa kifedha na familia yako kama milionea bora.

    4: Mamilionea Hawaendekezi Maisha Ya Kujionyesha.
    Vijana wa kiume na wa kike wenye wazazi matajiri mara nyingi hufanya sherehe za anasa na kuonyesha maisha yao ya gharama kubwa. Hata hivyo, hilo sio zuri kwa mustakabali wa kifedha wa vijana wenyewe. Kwa kweli, hilo linaweza kuwa janga la kifedha linaloandaliwa.

    Wazazi wengi matajiri hutumia pesa nyingi kwa watoto wao kupitia zawadi za pesa taslimu na kufadhili safari zisizo za biashara.

    Kuishi maisha ya uangalifu katika maisha yako kunafundisha watoto wako kufuata mtindo huo wa maisha. Kuwa na matumizi makubwa kunahimiza watoto wako kukumbatia maisha ya anasa badala ya kutengeneza utajiri.
    Kufundisha watoto wako umuhimu wa uangalifu katika matumizi ya fedha ni ufunguo wa utajiri. Inawasaidia kuendeleza mipango ya kufikia uhuru wa kifedha.

    5: Mamilionea Wanalea Watoto Wenye Majukumu ya Kiuchumi.
    Hakuna mtu anayetaka kuacha urithi mbaya anapofariki. Kila mtu anataka urithi wake udumishwe kwa miongo na vizazi vyake viongeze utajiri. Lakini je, hili linatokea kila wakati?

    Watoto wanaotegemea wazazi watarithi utajiri zaidi kutoka kwa wazazi wao. Lakini mara nyingi wanakosa maarifa ya kuwekeza na kujilimbikizia utajiri. Hii inawapelekea kutumia vibaya utajiri kupitia maisha ya kifahari. Hata hivyo, mahojiano ya Stanley yanaonyesha jinsi mamilionea bora wanavyochukulia malezi ya watoto wanaojitegemea. Hapa kuna baadhi ya masomo ya kujifunza kutoka kwao:

    1. Usiwaambie wako kwamba wewe ni tajiri.
      Watoto wenye wazazi wa UAW huiga tabia za matumizi ya wazazi wao. Pia wana hamu ya maisha ya anasa. Lakini watoto wa wazazi wa PAW hukua bila kujua thamani ya utajiri wa wazazi wao. Hii inawasaidia kujifunza kuwa kujitegemea na kuwajibika kwa tabia zao za matumizi ya fedha.
    2. Wafundishe watoto wako kuwa waangalifu kwenye matumizi ya pesa.
      Bila kujali umekusanya utajiri kiasi gani, fanya uangalifu. Wafundishe watoto wako vivyo hivyo ili waweze kuishi maisha rahisi.
      Watoto wako hawapaswi kutambua kuwa wewe ni tajiri hadi watakapokuwa watu wazima wenye majukumu na nidhamu. Wakati wanatambua utajiri wako, wanapaswa kuwa wamekomaa vya kutosha kuchukua majukumu na kufanya maamuzi chanya ya kuongeza utajiri.
    3. Elekeza watoto wako kuelekea mafanikio.
      Mamilionea wengi wanasisitiza haja ya kuwafundisha watoto wao jinsi ya kutengeneza utajiri. Kuwafundisha watoto kwamba kupata kipato kunawezesha matumizi zaidi kutaangamiza maisha yao ya kiuchumi. Bahati mbaya, hivyo ndivyo wazazi wengi wa UAW wanavyofanya. Matokeo yake, watoto wao wanapopata ongezeko la mshahara, wanazingatia kuongeza matumizi. Badala yake, wanapaswa kujifunza kuokoa au kuwekeza pesa wasizozihitaji.

    6: Mamilionea Wanatumia Fursa za Soko.
    Mamilionea wanafanyaje maamuzi ya nini cha kutumia? Wapangaji wa kimkakati wanafahamu siri za pesa. Wanawekeza katika huduma za afya za familia zao na biashara zinazoongeza uzalishaji.

    Mamilionea wanafanya uangalifu kwa kuepuka bidhaa na huduma zisizo za lazima. Hata hivyo, hawana uoga wa kuchukua hatari zilizohesabiwa kwa fursa za biashara zenye thamani.

    “Moja ya sababu ambazo mamilionea wanafanikiwa kiuchumi ni kwamba wanafikiri tofauti.” – Thomas J. Stanley

    Ili kufuata nyayo za mamilionea, jifunze kupanga uwekezaji wako kwa uangalifu. Fursa zenye hatari kubwa zinaweza kuwa na malipo makubwa ikiwa zitachunguzwa na kutekelezwa kwa uangalifu.

    7: Mamilionea Huchagua Kazi kwa Hekima.
    Una mpango gani wa kutengeneza utajiri? Je, unataka kufikia kilele cha kazi yako au kuanzisha biashara yako mwenyewe kutoka mwanzo?

    Kitu cha kushangaza ni kuwa, mamilionea wengi nchini Marekani ni wamiliki wa biashara binafsi. Unaweza kupata mshahara mkubwa kutoka kwenye ajira yako. Hata hivyo, utajikuta unatumia sehemu kubwa ya mshahara wako kulipia bili zako na kudumisha maisha yako ya gharama kubwa.

    Kinyume chake, wamiliki wa biashara hupokea kipato kutoka vyanzo tofautitofauti. Njia hizi zinawawezesha kuzidisha uwekezaji wao huku wakiendeleza maisha rahisi.

    “Utajiri ni kile unachojilimbikizia, sio kile unachotumia” – Thomas J. Stanley

    Kuanzisha biashara sio dhamana ya kuwa milionea. Biashara nyingi hazitimizi malengo ya wamiliki. Kushindwa kwa biashara nyingi kunaweza kuwa ni kutokana na ushindani au mipango mibovu.

    Mamilionea wanazingatia kuchagua kazi za kuwekeza. Wawekezaji wengi wa kawaida hudhani kazi maarufu ndizo zenye mafanikio zaidi. Hata hivyo, mamilionea wana maoni tofauti. Hapa kuna baadhi ya mawazo kuhusu kuchagua kazi sahihi:

    1. Sekta Isiyovutia. Si ajabu kwamba mamilionea wengi wanawekeza katika biashara hizi zinazoonekana ‘zisizovutia’. Sekta zisizovutia ni thabiti zaidi lakini hazivutii watu wengi.
    2. Uangalifu katika Biashara. Unahitaji kufanya uangalifu katika maisha yako binafsi na katika biashara. Punguza matumizi katika idara zisizo na tija. Hii itakusaidia kuzidisha rasilimali katika maeneo yanayotoa faida zaidi.
    3. Maarifa Mapana ya Biashara. Usiwekeze katika biashara tu kwa sababu inaahidi kuwa na faida. Mamilionea wengi wana ujuzi katika maeneo ya biashara wanayowekeza. Ikiwa haujazoea sekta ya ukarimu, fikiria upya kabla ya kufungua mgahawa.

    8: Mamilionea Wana Malengo na Madhumuni Wazi.
    Kama vile binadamu walivyo na sifa za kipekee, vivyo hivyo katika kujenga utajiri. Umepanga kukusanya utajiri kiasi gani katika mwaka mmoja? Ni mikakati gani umeweka ili kuhakikisha unafikia lengo lako?

    Mamilionea wengi ni wapangaji wakuu na wenye ufanisi katika kufafanua malengo yao. Wanatoa kipaumbele katika usimamizi wa fedha zao. Wengi wana ratiba za kila siku, kila wiki, na kila mwezi kufuatilia maendeleo yao.

    Malengo yanatoa taarifa kuhusu mikakati na njia wanazochukua. Wanachanganua malengo ya muda mrefu katika majukumu madogo yanayoweza kusimamiwa. Hii inatoa njia wazi kuelekea lengo la mwisho.

    Katika kitabu chake, No Excuses! Brian Tracy anadai kwamba asilimia tatu tu ya Wamarekani wazima wana malengo na madhumuni. Kundi hili linajilimbikizia utajiri mkubwa zaidi kuliko sehemu nyingine ya idadi ya watu.

    Ikiwa uko tayari kufanya kile kinachohitajika kuwa milionea, anza kwa kuweka malengo na madhumuni. Changanua malengo yako kwa kuyagawa katika malengo madogomadogo na kuanzisha mipango kwa kila hatua itakayokupa mtazamo wazi wa malengo yako.

    9: Mamilionea Wamepitia Nyakati Ngumu.
    Wengi wetu tunazingatia tu hadithi za mafanikio ya mamilionea. Lakini hatuelewi historia ya mafanikio yao. Mamilionea wengi walivuka mipaka yao kufikia walichonacho. Je, umewahi kufikiria kufanya kazi mbili bila likizo? Haya ni baadhi ya mambo ambayo mamilionea wamevumilia katika safari yao.

    Safari za kujenga utajiri mara chache huwa rahisi na zinahitaji maadili makali ya kazi. Mamilionea wengi waliojijenga wenyewe wamelazimika kukabiliana na vikwazo na vizuizi ili kufikia kiwango chao cha mafanikio. Pia wamelazimika kujinyima katika sasa yao ili wawe katika nafasi nzuri kwa siku zijazo.

    Fikiria gari la michezo unalotaka kununua leo ambalo linagharimu $50,000. Hata kama una pesa taslimu za kununua, hiyo $50,000 je, huwezi kuwekeza katika masoko ili kupata faida kubwa zaidi? Mamilionea wangeona hiyo ni fursa inayostahili kuchangamkiwa ili kupata faida kubwa zaidi baadaye.

    Kila hadithi inaleta mtazamo kwamba hakuna njia rahisi ya kujilimbikizia utajiri. Inahitaji kujitoa, uvumilivu, na nidhamu.

    Muhtasari wa Mwisho na Mapitio ya Kitabu cha The Millionaire Next Door.
    Kitabu cha Stanley na Danko, The Millionaire Next Door, kinawasilisha njia ya kweli ya kuwa milionea bora. Huna haja ya kuthibitisha wewe mwenyewe au utajiri wako kwa watu. Kutumia pesa zako kwa vito vya thamani, nguo za wabunifu, na magari hupunguza utajiri wako.

    The Millionaire Next Door inaonyesha kwamba, kuwa milionea inamaanisha kuokoa mapato yako ya ziada. Zaidi ya hayo, kupata utajiri sio otomatiki unapokuwa na pesa zaidi kuliko unazohitaji. Badala yake, ni mchakato wa polepole ambao unaweza kuchukua miaka. Safari pia inaweza kujumuisha changamoto nyingi. Uvumilivu wako na utayari wa kufanya makosa na kuyarekebisha ni muhimu.

    Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kutengeneza utajiri kutoka kwenye kitabu hiki cha The Millionaire Next Door. Kama una maoni basi usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante sana na karibu katika makala zinazokuja.

    error

    Enjoy this blog? Please spread the word :)

    Follow by Email
    WhatsApp