Sifa 6 Chaneli Yako ya YouTube Lazima Iwe Nazo Ili Kufanikiwa

Sifa 6  Chaneli Yako ya YouTube Lazima Iwe Nazo Ili Kufanikiwa

Tangu mwaka 2006, wakati Google iliponunua YouTube, jukwaa la video limeendelea kuwa maarufu. Leo hii, sio tu kwamba ni injini ya utafutaji ya pili kwa ukubwa baada ya Google, lakini pia ni tovuti ya tatu inayotembelewa zaidi mtandaoni. Hii imeleta fursa mpya na za kusisimua kwa wamiliki wa biashara ambao wanataka kuwafikia watazamaji na wateja wengi zaidi. Katika makala ya leo nitakushirikisha sifa 6 ambazo chaneli yako ya YouTube lazima iwe nazo ili uweze kufanikiwa.

Sifa 6 Channel Yako ya YouTube Lazima Iwe Nazo Ili Uweze Kufanikiwa.

1.Kuwa na ratiba maalumu ya kuweka video.
Channel ya YouTube yenye mafanikio zaidi, huweka video mpya kila siku au hata mara mbili kwa siku. Kwa aina hii ya kuweka video mara kwa mara, wafuasi wake daima huwa wanakumbushwa juu ya channel hiyo na wanapewa nafasi zaidi ya kuwasiliana na kampuni. Hivyo unahitajika kuwa na ratiba maalumu ya kuweka video mpya kwenye chaneli yako. Ikiwa hauna wakati wa kuandaa video kila siku, basi unahitajika kuweka video mpya angalau mara moja kwa wiki.

2.Jitofautishe.
Ikiwa unataka channel yako iwe na mafanikio, basi unahitajika kufanya kitu cha kipekee ambacho kitakufanya uwe tofauti na wengine. Kwa mfano, ikiwa una channel ya kilimo, kuandaa video zinazofundisha kilimo peke yake haitoshi kukufanya uwe tofauti na wengine. Unaweza kujitofautisha zaidi kwa kubobea kwenye aina fulani ya mazao kwa mfano mbogamboga na matunda. Kwa kufanya hivyo utakuwa umejitofautisha na chaneli zingine.

3.Ubora wa maudhui yako ni muhimu sana katika mafanikio yako kwenye YouTube.
Ikiwa maudhui yako hayana umahiri, watazamaji hawatakuchukulia kwa uzito kuangalia video zako. Hii hasa ni muhimu ikiwa unajaribu kuanzisha akaunti ya YouTube kwa ajili ya biashara yako. Unatakiwa kuhakikisha kuwa vifaa unavyotumia ni vya ubora wa juu, iwe ni simu yako ya mkononi inayoweza kurekodi video za HD na 4K au kamera ya video ya HD yenye gharama nafuu.

4.Jumuisha Bidhaa Zako Katika Video Zako.
Sababu kuu kwa nini biashara nyingi zinageukia YouTube ni kuongeza njia nyingine ya masoko ambayo itasaidia biashara zao kukua. Mojawapo ya njia za msingi za kufanya hivyo ni kwa kutangaza bidhaa zako katika video zako. Tafuta njia ya kufanya bidhaa zako kuwa sehemu muhimu ya maudhui yako ya video.

5.Maudhui yanapaswa kulenga kundi fulani la jamii.
YouTube imekuwa maarufu kimataifa, hivyo unahitajika kuzingatia hadhira gani unayolenga watazame video zako. Ikiwa Kiingereza siyo lugha yako ya asili, usisumbuke, jikite kwenye lugha inayotumika katika biashara yako na jamii unayolenga na hivyo utaweza kufanya vyema sana kwenye jukwaa hilo.

6.Weka burudani kwenye video zako.
Sehemu kubwa ya chaneli za YouTube zilizofanikiwa zimegundua njia ya kuunganisha aina fulani ya burudani katika maudhui yao. Maudhui yoyote unayoandaa kupitia video zako, jitahidi kuchanganya na burudani ili watu wafurahie kuangalia video zako mwanzo hadi mwisho.

Ni matumaini yangu umejifunza maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kukuza chaneli yako ya YouTube. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante, karibu katika makala zinazofuata.

Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

Katika kipindi hiki, maudhui yaliyoandaliwa kwa mfumo wa video ndiyo yanayochukua sehemu kubwa ya maudhui yote mtandaoni. Utafiti unaonyesha kuwa mpaka sasa, video inachukua asilimia 82 ya watu wanaotafuta maudhui mtandaoni. Ikiwa unapenda kufaidika na idadi ya watu wanaotafuta maudhui mtandaoni kwa wingi, basi unahitajika kuanzisha Chaneli ya YouTube. Katika makala ya leo nitakushirikisha mambo 5 ya kuzingatia ili kuwa na chaneli bora ya YouTube.

Mambo 5 Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Chaneli Bora Ya YouTube

1.Wekeza katika kupata mada bora zinazoelimisha, Sio Vifaa.
Kifaa pekee unachohitaji kuanzisha chaneli ya YouTube ni simu yenye kamera nzuri. Unachoweza kukosa ni mada bora zinazoelimisha kwa ajili ya video zako. Ikiwa unataka kuwa na chaneli ya YouTube iliyofanikiwa, basi unahitaji kutumia muda kutafakari mada yako. Unaweza kuanza kwa kuandika mawazo 25 hadi 50 kwa ajili ya video zako. Fikiri kuhusu mada za video na utafute YouTube ili kuona mada ulizochagua zina ushindani gani na hivyo kujua unahitaji juhudi kiasi gani ili kushinda ushindani wa chaneli zingine zinazotoa video zenye mada kama za kwako.

2.Andaa video fupi
Watazamaji leo wanatumia muda mfupi sana kusoma au kuangalia habari mtandaoni. Kama ndio unaanza, jitahidi uwe unaweka video fupi. Hii ni kwa sababu Unapoanza, watazamaji wanakuwa hawakujui. Kitu pekee watakachokifanya ni kuangalia maudhui ya video zako kama yanatatua changamoto zao. Hivyo weka video fupi na zenye ujumbe ili kuwafanya watazamaji wako wafurahie na bila kuchoka kuangalia.

3.Weka picha nzuri (thumbnail) kwenye video zako.
Kitu pekee kinachooneka kwenye video zako kabla watu hawajazifungua ni picha (thumbnail). Hivyo, unapoweka thumbnail zinazovutia na zinazoendana na maudhui ya video zako, basi utaweza kuvutia watazamaji wengi kuangalia video zako.

4.Weka vichwa vya habari vinavyovutia.
Jambo jingine la kuzingatia ni kuwa, Unahitajika kuhakikisha kuwa mada za video zako zinavutia watazamaji wako. Pia hakikisha kuwa unaweka vichwa vya habari vinavyovutia na vinavyojumuisha maneno muhimu yanayoendana na maudhui ya video zako ili kuvutia umakini wa injini za utafutaji.


5.Shirikisha Watazamaji Wako Kupitia Maoni
Jambo la mwisho unalotakiwa kufanya ni kujibu maoni pamoja na maswali ya watazamaji wako. Watazamaji wa YouTube huwa wanapenda kujiunga na chaneli ambazo zinawathamini kwa kujibu maoni yao. Hivyo, mojawapo ya njia rahisi zaidi za kukuza Chaneli yako, ni kwa kuwashirikisha watazamaji wako kwenye video unazoweka kwenye chaneli yako.

Kuanzisha chaneli ya YouTube ambayo watu watapenda kuitazama siyo jambo gumu. Ingawa itachukua muda na juhudi kwa upande wako. Kwa kuzingatia mambo haya matano niliyoyaeleza kwenye makala hii kutakusaidia kukuza chaneli yako.

Nimatumaini yangu umepata maarifa ya kukusaidia kuanzisha chaneli bora ya YouTube. Kama una swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa kunipigia moja kwa moja au kupitia WhatsApp kwa namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Tiba 7 Za Umaskini Na Sheria 5 Za Jinsi Ya Kuwa Tajiri.

Tiba 7 Za Umaskini Na Sheria 5 Za Jinsi Ya Kuwa Tajiri.

George Samuel Clason ni mwandishi aliyeishi mwanzoni mwa karne ya 20 ambaye alibadilisha kabisa mtizamo wa watu katika mambo yote yanayohusu ushauri wa kifedha. Baada ya kuhudumu katika Vita vya Uhispania na Amerika, George alianza kuandika vipeperushi vya jinsi ya kupata mafanikio ya kifedha. The Richest Man In Babylon (Mtu Tajiri Zaidi katika Babeli ) ni mkusanyiko wa machapisho yake maarufu zaidi alivyowahi kuandika. George anasifiwa kwa kubuni neno ‘Jilipe kwanza’ yaani ‘pay yourself first.’ kitabu hiki kinaelezea kanuni za jinsi ya kuwa tajiri.

The Richest Man In Babylon (Mtu Tajiri Zaidi katika Babeli) ni kitabu ambacho kimedumu kwa karibu miaka 100. Pamoja na kuwa kitabu cha zamani, kitabu hiki bado kinatumika leo kama kilivyokuwa kinatumika wakati kinachapishwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 1926. Kitabu hiki kinaelezea ushauri wa kifedha kupitia mkusanyiko wa mifano. Mifano hii imetoka Babeli ya kale. Mhusika mkuu wa kitabu hiki ni Arkadi. Arkadi ni mwandishi maskini ambaye alikuja kuwa ‘mtu tajiri zaidi Babeli.

Babeli lilikuwa jiji tajiri zaidi ulimwenguni wakati huo kwa sababu watu wake walithamini thamani ya pesa. Kitabu hiki ni mojawapo ya vitabu vya kitamaduni vyenye ushawishi mkubwa vinavyotoa ushauri wa kifedha. Mwishoni mwa muhtasari wa kitabu hiki, utakuwa na ufahamu mkubwa kuhusiana na fedha kupitia ushauri wa kifedha wa Arkad. Hapa, utajifunza tiba saba za umaskini na sheria tano za dhahabu. Hizi zitakusaidia kuzalisha pesa, kuzilinda na kuziwekeza na hivyo kuwa tajiri.

Tiba Saba za Arkad.


1.Jilipe Kwanza

Unapaswa kuangalia kila wakati jinsi ambavyo unaweza kuokoa pesa unazopata kwa kupunguza matumizi kadiri unavyoweza. Clason anapendekeza kuokoa angalau 10% ya mapato yako. Ikiwa unaweza kuokoa sehemu kubwa kuliko hii, basi hiyo ni nzuri zaidi. Pesa hizi unapaswa kuziwekeza Ili zizae na kuongezeka. Ikiwa una deni, unapaswa kuishi kwa 70% ya kile unachopata. Okoa 10% kwa ajili ya kuwekeza na utumie 20% iliyobaki kulipa deni lako. Unapaswa kuweka kando hii pesa kabla ya kufanya matumizi yoyote mengine ya pesa zako. Hivyo, mwandishi anasisitiza kujilipa kwanza kwenye kila kipato unachokipata kabla ya kuanza matumizi mengine.

2.Dhibiti Gharama Zako Za Maisha.
Unatakiwa kudhibiti gharama zako. Ili kuokoa angalau 10% ya mapato yako, itabidi upunguze matumizi yako. Unahitajika kutumia 90% au chini ya mapato yako. Kwa hiyo, unapaswa kujifunza kuishi chini ya kipato chako kwa kuzuia gharama zisizo za lazima. Kama gharama zako zitakua sawa na mapato yako, basi hutapata pesa inayobaki ambayo utaiwekeza. Kaa chini na utafakari ni matumizi gani ambayo unaweza kuyapunguza. Kama utashindwa kupunguza matumizi yako yaani mapato yako yakiwa sawa na matumizi, basi utakuwa ukiokoa 0% ya mapato yako kila mwezi. Mfano kamili wa hili ni wakati watu wanapopata nyongeza ya mshahara. Badala ya kutumia hii kama fursa ya kuokoa pesa zaidi, watu huanza kutumia zaidi na hivyo kushindwa kuweka akiba. Unaweza kuokoa pesa kwa kudhibiti hamu yako ya kununua vitu visivyo vya lazima na kudumisha tabia hii maisha yako yote.

Huwezi kuwa tajiri bila kudhibiti gharama zako za maisha. Ili uweze kudhibiti gharama zako za maisha ni lazima uwe na bajeti. Ili kupanga bajeti kwa ufanisi unahitajika kugawanya gharama zako katika makundi mawili: mahitaji ya lazima na mahitaji yasiyo ya lazima. Tenga takriban 50% ya bajeti yako kwa mahitaji ya lazima kama vile kodi ya nyumba, chakula na kadhalika. Kisha unapaswa kutenga salio kwa ajili ya matumizi yasiyo ya lazima.

3.Ifanye Pesa Ikufanyie Kazi.
Kuokoa pesa na kutotumia pesa bila mpangilio, haitoshi kukufanya uwe tajiri. Unapaswa kuwekeza pesa zako. Tiba mbili za kwanza yaani kuokoa pesa kwa kuweka akiba na kudhibiti gharama za maisha, zitakusaidia katika tiba hii ya tatu. Tiba mbili za kwanza zitakupatia pesa za kuwekeza.

Kila senti ya akiba yako inapaswa kuwekezwa. Kila unapopata faida ya pesa uliyowekeza, unapaswa kuiwekeza pia faida hiyo. Ukifanya hivi, utajiri wako utaongezeka polepole. Utakuwa unaunda jeshi la wafanyakazi ambao watakuwa wanakufanyia kazi.

Baadhi ya maeneo bora ya kuwekeza akiba yako ni kwenye hisa, hati fungani au mali isiyohamishika. Ikiwa utafanya uwekezaji mzuri, pesa zako ulizowekeza zitaongezeka sana. Kwa hiyo, usiruhusu fursa kubwa zikupite. Ikiwa fursa nzuri ya uwekezaji itatokea, hakikisha umeielewa vizuri kabla ya kuwekeza pesa zako. Hivyo, ili uwe na pesa nyingi kwa ajili ya kuwekeza, unapaswa kupunguza matumizi yako zaidi.

Jambo la muhimu hapa unalopaswa kuzingatia ni kuwa, hakikisha unawekeza pesa zako katika maeneo ambayo una ujuzi. Au, ikiwa kuna fursa ambayo huna ujuzi nayo, huenda ukahitaji kujifunza zaidi, watu bora wa kujifunza kutoka kwao ni washauri wa kifedha.

4.Linda Utajiri Wako
Kuna hatari zinazohusiana na kujaribu kuwa tajiri Kwa haraka. Ni rahisi kupoteza pesa kwa kufanya uwekezaji duni. Hivyo, ili kupunguza hatari ya kupoteza pesa zako, njia moja ya kufanya ni kujifunza kutoka kwa wale ambao wamefanikiwa kujenga utajiri katika eneo unalotaka kuwekeza.

5.Miliki Nyumba Yako

Kumiliki nyumba humpa mtu kujiamini zaidi.

Kukodisha nyumba ni njia rahisi ya kupoteza pesa. Unakuwa unampa pesa zako tu mwenye nyumba. Ni bora kuchukua mkopo na kununua au kujenga nyumba. Wakati utakapokuwa umemaliza kulipa mkopo, utakuwa unamiliki nyumba yako. Baada ya kuwa umemiliki nyumba yako, unaweza kuitumia vyovyote utakavyopenda. Unaweza kuipangisha na ikawa ni uwekezaji unaokuletea pesa. Lakini, mwandishi anashauri kuwa, njia bora zaidi ni kununua nyumba bila mkopo.

6.Jiandae kwa maisha yako ya uzeeni au kipindi ambacho hutakuwa tena na nguvu za kufanya kazi.
Maisha ya kila mtu huanzia utotoni hadi uzeeni. Hii ndiyo njia ya maisha na hakuna mtu anayeweza kukwepa kupita kwenye njia hiyo. Kwa hiyo, unapaswa kufanya maandalizi kwa kuwa na kipato kwa ajili ya siku zijazo kwako wewe pamoja na familia yako. Hali ya kifedha inaweza kubadilika ghafla. Kwa hiyo, unahitajika kuwa na mpango madhubuti ili hali ikiwa mbaya uweze kujikwamua na kuendeleza maisha yako. Kwa mfano, unaweza kuugua na hivyo usiweze kufanya kazi au kupoteza kazi yako. Unatakiwa kuwa na vitega uchumi mahali ambavyo vinakuletea kipato .

7.Wekeza Ndani Yako
Mali yako ya thamani kuliko zote ni akili yako. Kwa hivyo, ili kuongeza uwezo wako wa kupata utajiri, lazima uwekeze ndani yako. Unahitajika kuboresha uwezo wako wa kuongeza kipato chako. Unaweza kufanya hivyo kwa kupata ujuzi na maarifa mapya muhimu kwa ajili ya kupata utajiri katika kipindi hicho. Fikiria jinsi unavyoweza kupata pesa zaidi. Kisha, fikiria ni mabadiliko gani unayohitaji kujifanyia mwenyewe ili kupata utajiri huo unaoutamani. Wekeza katika kufanya mabadiliko hayo.

Pamoja na kujifunza ujuzi mpya, kuwekeza ndani yako kunaweza kumaanisha kukuza tabia mpya nzuri zitakazokusaidia kufikia malengo yako ya kifedha. Mifano ya tabia nzuri ni kufanya mazoezi kila siku, kusoma vitabu vya elimu ya fedha kabla ya kulala na kuacha tabia ya matumizi mabaya ya fedha.

Sheria Tano za Dhahabu.

Uhuru wa kifedha

Katika kitabu hiki, Clason pia anatoa muhtasari wa jinsi ya kuwa na mafanikio ya kifedha. Anatupatia sheria tano za jinsi ya kuwa tajiri. Sheria hizi anaziita sheria Tano za dhahabu. Ametumia neno dhahabu kwa sababu dhahabu ilitumika kupima kiasi cha utajiri kipindi cha Babeli ya zamani. Hivyo kwa sasa unaweza

kutumia neno pesa badala ya dhahabu.
Zifuatazo ni sheria tano za jinsi ya kuwa tajiri kama zilivyoelezwa kwenye kitabu hiki cha The Richest Man In Babylon:

1. Dhahabu huja kwa urahisi kwa wale wanaookoa angalau 10% ya mapato yao.

2. Dhahabu huongezeka kwa wale watu ambao wataiwekeza Ili iendelee kuwazalishia faida.

3. Dhahabu inashikamana na watu wanaowekeza dhahabu zao kwa watu wenye busara.

4. Dhahabu hukimbia kutoka kwa watu wanaoiwekeza kwenye biashara au uwekezaji ambao hawana elimu ya kutosha au taarifa za kutosha.

5. Dhahabu hukimbia kutoka kwa watu wanaolazimisha dhahabu kuzalisha utajiri wa haraka isivyowezekana.

Siri ya kutengeneza utajiri ni kuwa na matumizi kidogo iwezekanavyo, kuokoa pesa ili uweze kuwekeza. Pia kuwekeza kwako mwenyewe ili uweze kuwa na maarifa ya kutosha kukamata fursa za kifedha zinapojitokeza.

Ili uweze kuwa tajiri, lazima ufikirie juu ya pesa zako kama mti. Mti hukua polepole kutoka kwenye mbegu, na unahitaji maji na mwanga ili uweze kusitawi. Tiba hizi saba ni chakula cha mti wako wa pesa. Kwa kuzingatia tiba hizi saba huku ukifanya kazi kwa bidii, utaweza kufikia uhuru wa kifedha na kuwa tajiri.

Ni matumaini yangu umepata maarifa ya kutosha ya tiba saba za Umaskini na sheria tano za jinsi ya kuwa tajiri kama zilivyoelezwa kwenye kitabu hiki cha The Richest Man In Babylon. Kama una maoni au swali lolote, usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Njia Rahisi 4 Za Kuongeza Watazamaji Kwenye Chaneli Yako.

Njia Rahisi 4 Za Kuongeza Watazamaji Kwenye Chaneli Yako.

Utafiti unaonyesha kuwa watu sita kati ya kumi wanapendelea kutazama video mtandaoni badala ya kutumia T.V. Hii ndiyo sababu makampuni, wafanyabiashara, wajasiriamali na brand nyingi kwa sasa zinajaribu kujenga uwepo wao mtandaoni katika mtandao wa YouTube. Kwa bahati mbaya, kwa sababu kuna video nyingi sana zinazopakiwa kwenye mtandao huu kila siku, inawezekana ikawa ni changamoto kwa video zako ambazo umejitahidi sana kuziandaa kuonekana kwa urahisi. Kwa bahati nzuri, kuna njia kadhaa rahisi za kuongeza watazamaji kwenye chaneli yako ya YouTube. Katika makala ya leo, nitakushirikisha njia rahisi 4 za kuongeza idadi ya watazamaji kwenye chaneli yako ya YouTube.

Njia Rahisi 4 Za Kuongeza Idadi ya Watazamaji Kwenye Chaneli Yako Ya YouTube

2.Weka wito wa kuchukua hatua kwenye video zako (call-to -action)
Kuweka wito wa kuchukua hatua ndani ya video zako kunaweza kusaidia kukuza ushirikiano wako na watazamaji wako na hivyo kukuza chaneli yako. Unaweza kuweka maelezo katika video zako yanayowahimiza watazamaji wako kujisajiri kwenye chaneli yako na kadhalika.

3.Unganisha chaneli yako na Tovuti au Blogu yako
YouTube hukupa uwezo wa kuunganisha tovuti ya kampuni yako au blogu kwenye chaneli yako. Hii inaweza kusaidia kuboresha matokeo ya utafutaji watu wanapokutafuta mtandaoni. Pia inakusaidia kuthibitisha kuwa chaneli yako ni uwakilishi rasmi wa brand yako inayopo kwenye tovuti au blog yako.

4.Weka video ya kionjo (video trailer) kwenye chaneli yako.
YouTube hukuruhusu kutumia video kama kionjo kwa ajili ya kuelezea malengo ya chaneli yako na hivyo kuwakaribisha watazamaji wako kuangalia chaneli yako. Si lazima trela ya kukaribisha iwe ndefu, lakini ni fursa nzuri kwako kuwafahamisha watu ni video zenye mambo gani unaweka kwenye chaneli yako.

Kuongeza watazamaji kwenye chaneli yako ni kazi kubwa inahitaji kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Hii inajumuisha kuandaa video bora na zenye kuelimisha. Utahitajika kutumia muda mwingi na kazi ngumu ili uweze kuona chaneli yako ikikua kwa kuwa na watazamaji wengi.

Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuongeza watazamaji kwenye chaneli yako. Kama una swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752081669. Karibu sana katika makala zinazokuja.

Njia 7 za Kupata Subscribers Wengi Kwenye Chaneli Yako.

Njia 7 za Kupata Subscribers Wengi Kwenye Chaneli Yako.

Mafanikio kwenye chaneli ya YouTube yanatokana na kuwa na subscribers wengi. Hivyo mojawapo ya vipimo muhimu vya kupima mafanikio kwenye chaneli yako ya YouTube ni kupitia idadi ya watu wanaofuatilia Chaneli yako (subscribers). Ukiwa na subscribers wengi maana yake ni kuwa, video zako zitakuwa na watazamaji wengi. Kuweka video mara kwa mara huwa na athari kubwa kwenye idadi ya watu wanaofuatilia chaneli yako kwa sababu, kadiri unavyoweka video, ndivyo watu wanavyozitazama na kuzishea kwa marafiki zao. Hivyo, unapokuwa na video nyingi ambazo watu watazitazama na kuwashirikisha marafiki zao, utaweza kuongeza idadi ya wafuasi (subscribers). Hata hivyo, kupata subscribers kwenye YouTube hutokana na sababu nyingi zaidi ya kuweka video tu. Katika makala ya leo nitakushirikisha vidokezo 7 vya kusisimua vya jinsi ya kuongeza wanaofuatilia chaneli yako.

Kidokezo #1: Andaa video zenye maudhui yanayovutia na kuelimisha
Ikiwa unataka watu watazame video zako, unahitajika kuwa na maudhui yanayovutia na yenye kuelimisha. Hapa kuna baadhi ya njia ambazo zitakusaidia kuandaa maudhui bora zaidi:

Andaa maudhui ya video zako kwa kulenga kundi fulani la jamii.
Hakikisha kwamba unaandaa maelezo ya video yako (script) kabla ya kuanza kurekodi video yako ili kuepuka kuwajaza watazamaji taarifa zisizo za lazima. Iwapo unahisi kuwa kuna maelezo mengi katika video moja, yagawanye katika video kadhaa.
Watazamaji wanapenda unapotumia mfano kila baada ya muda fulani. Tumia mifano kadiri uwezavyo na uhakikishe kuwa inatoka kwenye tovuti au vyanzo vya habari vinavyoaminika na vyenye ubora wa hali ya juu.

Weka vivutio kwenye video zako ili watazamaji wawe na hamu ya kuangalia.
Anza video zako kwa kitu kinachogusa changamoto ya watazamaji. Kitu hicho kitakuwa ni ndoano (hook) ya kuvutia ambayo itawafanya watu watake kuendelea kutazama video yako mpaka mwisho.

Kidokezo #2: Andaa na Uweke Video Mara Kwa Mara
Hakuna shaka kwamba kuandaa na kuweka video mara kwa mara husaidia kuongeza wanaofuatilia kwenye chaneli yako. Kinyume chake, ikiwa hutaweka video kwa muda mrefu, watu hawatataka kujisajili kwenye chaneli yako.
Kulingana na utafiti uliofanyika, chaneli za YouTube zinazoweka video zaidi ya mara moja kwa wiki hufanya vyema zaidi kuliko zile ambazo haziweki video mara kwa mara. Mtu anapojisajili kweye chaneli yako, huwa anapata taarifa kwenye barua pepe yake kila unapopakia video mpya. Mtu akipata taarifa ya barua pepe mara moja kwa wiki, kuna uwezekano mkubwa kwamba atashiriki video yako, hasa ikiwa maudhui yake yanavutia na yanaelimisha. Hivyo, ikiwa unaweka zaidi ya video moja kwa wiki, kuna uwezekano mkubwa wa kupata subscribers wengi zaidi.

Kidokezo #3: Boresha Video Zako
Kuboresha video zako husaidia maudhui yako kuwa ya hali ya juu kwenye YouTube. Ili kuhakikisha kuwa video zako zinafikia hadhira inayofaa, unaweza kuboresha idadi ya vipengele vya video zako kama vile kichwa cha habari, maelezo, video na meta tagi zingine.

Kichwa cha habari.
Kutumia neno kuu la msingi katika kichwa chako cha video kunaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa video yako kutazamwa zaidi.

Maelezo.
Unapoandika maelezo ya video yako, hakikisha kuwa unatoa taarifa zote muhimu zinazohusiana na malengo ya video yako.

Weka tagi kwenye video zako.
Tagi ni maneno muhimu ambayo watu wakitafuta mtandaoni, wataiona video yako. Hivyo, ukiweka tagi kweye video zako, utawezesha video zako kuonekana kwa urahisi mtandaoni na hivyo kupata watazamaji wengi.

Kidokezo #4: Boresha chaneli yako ya YouTube
Ili kupata wafuatiliaji zaidi kwenye YouTube, unahitaji kuboresha sio tu video zako lakini pia hata Mwonekano wa chaneli yako. Hapa kuna baadhi ya njia rahisi zaidi za kufanya:

1.Weka video ya kionjo (trailer) inayoelezea kwa ufupi lengo la chaneli yako.
Kionjo huwapa hadhira yako muhtasari wa kile chaneli yako inatoa. Kupitia trela yako, unaweza kuwapa hadhira yako wazo kuhusu:
aina ya video unazoweka
ratiba yako ya kuweka video na kadhalika.

2.Tengeneza Mwonekano wa Kuvutia wa Chaneli yako
Ili chaneli yako ivutie, weka maelezo yanayoitambulisha kwa watazamaji wako. Tumia maneno ya msingi na yanayoendana na maudhui unayotoa kwenye chaneli yako. Kwa kufanya hivyo, utaiwezesha chaneli yako kuonekana kwa urahisi mtandaoni.

Kidokezo #5: Andaa Video za Ubora wa hali ya Juu
Jambo jingine linalochangia kuongeza wanaofuatilia chaneli yako ni kuweka video za ubora wa juu! Watu hawapendi kutazama video ambazo hazina sauti na video duni. Ikiwa unaweka video bora, watu watakuchukulia kwa uzito wa hali ya juu na kujihusisha na video zako.

Kidokezo #6: Shirikiana na hadhira yako kwa kujibu maswali na maoni yao.
Unapotangamana na watazamaji wako, unawapa hisia ya kuridhika kuwa unawajali na kuwapenda. Hii husababisha uwezekano mkubwa wa watu wengine kutamani kujisajili kwenye chaneli yako. Pia wahimize watazamaji wako kujisajiri kwenye chaneli yako.

Kidokezo #7: Tangaza Video Zako Kwenye Majukwaa Mengine Na Mitandao Ya Kijamii.
Ikiwa utapenda video zako zifikie watu nje ya YouTube, ni wazo zuri kutangaza video zako kwenye majukwaa mengine na mitandao ya kijamii.

Ni matumaini yangu kuwa makala hii ya “jinsi ya Kupata Wafuasi (Subscribers) Wengi Kwenye Chaneli Yako Ya YouTube” itakusaidia kufikia malengo yako ya YouTube. Ili kujitambulisha kama mtaalamu kwenye YouTube, unahitaji kupata idadi kubwa ya subscribers. Njia pekee ya kufanya hivyo ni kwa kutoa maudhui mazuri, kuboresha maeneo muhimu ya chaneli yako pamoja na kuandaa video zenye ubora wa hali ya juu.

Kama una swali au maoni yoyote, usisite kuandika maoni yako hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Makosa 4 Ya Kuepuka Kwenye Chaneli Yako Ya YouTube

Makosa 4 Ya Kuepuka Kwenye Chaneli Yako Ya YouTube

Unapoanzisha chaneli yako mpya ya YouTube, pengine tayari una mambo machache unayohitaji kuyafanya ili uweze kufanikiwa. Lakini, kama ilivyo muhimu kujua mambo unayopaswa kufanya, ni muhimu pia kujua ni makosa gani ya kuepuka. Katika makala ya leo nitakushirikisha makosa manne ambayo unapaswa kuyaepuka unapoanzisha chaneli yako ya YouTube.

Kosa #1 – Kupuuzia kujibu maoni na maswali ya watazamaji wako.
Watazamaji wako ndiyo sababu pekee inayokufanya uwe na chaneli ya YouTube. Bila wao, huwezi kupata mafanikio. Ikiwa watazamaji wako watakuuliza maswali au kukuachia maoni katika sehemu ya maoni ya video zako, basi unahitajika kuwajibu mapema iwezekanavyo. Unahitajika kuhakikisha kuwa unajibu kwa ufasaha majibu yanayoendana na swali lililoulizwa. Kadiri unavyojihusisha na watazamaji wako, ndivyo watakavyohisi wameunganishwa zaidi na biashara yako.

Kosa #2 – Kutoboresha Vichwa vya habari vya Video Zako
Ikiwa hutajumuisha maneno muhimu yanayoendana na maudhui ya video zako kwenye vichwa vya habari vya video zako, watazamaji wako hawataweza kukupata kwa urahisi katika matokeo ya utafutaji wanapokuwa wametafuta video zako mtandaoni. Unatakiwa kuhakikisha kuwa, unaandaa video za kipekee na zinazovutia ambazo zinajumuisha kwenye vichwa vya habari maneno muhimu ili video zako ziweze kuonekana juu zaidi katika viwango vya utafutaji.

Kosa #3 – Kutotangaza video zako.
Ukishindwa kutangaza video zako, inakuwa vigumu zaidi kwa watazamaji wako kutambua video ambazo umetayarisha. Ili uweze kupata watazamaji wengi kwenye video zako, unahitajika kushea video zako kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, telegram na kadhalika. Pia unaweza kushare video zako kwenye blog au tovuti yako kama utakuwa nayo. Pia katika kila video unayoweka kwenye chaneli yako, hakikisha unaweka logo inayowakilisha utambulisho wako (brand). Usipoweka utambulisho (brand) kwenye video zako, itakuwa ni vigumu kukuza jina la chaneli yako pamoja na biashara au huduma unayotoa.

Kosa #4 – Kutokuweka picha (thumbnail) kwenye video zako.
YouTube huruhusu kuweka picha inayotambulisha maudhui ya video yako (thumbnail). Picha hii ndiyo itaayoonekana karibu na kichwa cha habari cha video yako katika matokeo ya utafutaji. Usipochagua picha yako mwenyewe, YouTube itaipa video yako picha ambayo haitaendana na maudhui uliyoyakusudia ya video yako. Hivyo, ili kuwashirikisha watazamaji wako vyema zaidi, unahitajika kuhakikisha kuwa unaweka picha yako maalum ambayo inawakilisha vyema maudhui ya video yako.

Unapoanzisha chaneli yako ya YouTube, haya ni mambo manne ambayo unapaswa kuyaepuka. Kwa kuzingatia mambo haya niliyoyaeleza katika makala hii utakuwa kwenye njia nzuri ya kukuza chaneli yako ya YouTube na kupata mafanikio makubwa kwenye biashara yako.

Kwa leo niishie hapo. Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuwa na chaneli ya YouTube yenye mafanikio. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami kwa kupiga au WhatsApp 0752 081669. Karibu tena kwenye makala zinazokuja.

Maswali 5 Ya Kujiuliza Kabla ya Kuanzisha Channel Ya YouTube

Channel ya YouTube

Katika makala zangu zilizopita nilielezea njia mbalimbali za kuanzisha biashara mtandaoni na kutengeneza kipato. Miongoni mwa njia hizo ni kuanzisha na kumiliki channel ya YouTube.Ikiwa umekuwa ukifikiria kuanzisha channel ya YouTube Kwa ajili ya biashara yako na hivyo kutengeneza kipato, kabla ya kuchukua hatua hiyo ni muhimu kujiuliza maswali kadhaa. Katika makala ya leo nitakushirikisha maswali matano muhimu Unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha channel ya YouTube ili uweze kupata mafanikio kwenye channel yako.

Maswali 5 Unayopaswa Kujiuliza Kabla ya Kuanzisha Channel Ya YouTube.

1.Kwa nini Unataka Kuanzisha Channel Ya YouTube?
Huenda hili ndilo swali muhimu zaidi unalohitaji kujiuliza kabla ya kuanzisha channel ya YouTube. Je, unahitaji kuanzisha channel ya YouTube kwa ajili ya kupeleka watembeleaji wengi kwenye tovuti ya kampuni yako? Je, unahitaji kuanzisha channel ili kujitangaza watu wafahamu biashara au huduma unayotoa ? Je, una maarifa au ujuzi na hivyo una shauku ya kuwashirikisha watu maarifa yako? Je, unaona kuna tatizo fulani katika jamii na unahisi unaweza kulitatua kupitia kuelimisha kwa kurekodi video? Je, una kipaji fulani na hivyo unahitaji kukionyesha ili watu wakutambue? Hizi zote ni sababu nzuri za kutaka kuanzisha channeli ya YouTube. Hata hivyo, ikiwa unataka kuanzisha channel kwa lengo tu la kutengezeza pesa nyingi, basi unahitaji kufikiria upya kabla ya kufanya uamuzi wako. Kumbuka kuwa kupata pesa kinatakiwa kiwe kipaumbe chako cha mwisho. Kumbuka kuwa, pesa ni matokeo ya kutatua changamoto katika jamii. Hivyo channel yako inapaswa kujikita katika kutatua changamoto fulani katika jamii. Hivyo, ukiweza kutatua changamoto fulani kupitia channel yako, pesa zitakuja tu.

2.Je, nitakuwa ninaweka video zinazotangaza biashara na huduma zangu?
Watu wengi huwa wanaingia YouTube kwa sababu wanataka kuburudishwa, kufahamishwa na kuelimishwa, si kutazama matangazo ya biashara. Ili uweze kuwa na mafanikio kwenye channel ya YouTube ni sharti uwe unatengeneza video zenye manufaa na taarifa zinazoboresha taswira ya kampuni yako bila kutangaza sana. Kuandaa video za ” jinsi ya kufanya”, kunaweza kukusaidia kujenga uaminifu (trust) na kukubalika ( authority) kwa kwa wateja wako na wafuasi wako bila kulazimika kuuza bidhaa kwenye video zako.

3.Je, Nielezeje Video Zangu za YouTube?
Maelezo ya video zako yanapaswa kuwa mafupi na yanapaswa kujumuisha URL ya tovuti ya kampuni yako katika sentensi ya kwanza ya maelezo ili kuwahimiza watazamaji wako kutembelea tovuti yako. Pia hakikisha unajumuisha maneno ya msingi (keywords) kwenye maelezo yako ambayo yanawiana na malengo ya video zako pamoja na channel yako kwa ujumla. Hii itasaidia kuzifanya video zako zionekane kwa urahisi watu wanapozitafuta mtandaoni.

4.Je, Nitayarishe Video Zangu Mimi Mwenyewe?
Unaweza kuchagua kutayarisha video zako wewe mwenyewe au kuajiri mtu au kampuni ya utayarishaji. Hii itategemea ni pesa kiasi ngapi na wakati unaotaka kuwekeza. Ikiwa una rasilimali chache, unaweza kupiga video na smartphone yako au kamera ya HD. Hata hivyo unaporekodi video, unatakiwa kuhakikisha kuwa unapakia video mpya mara kwa mara. Ukiweza kurekodi video mpya na ya kusisimua kila wiki, utaweza kukuza idadi ya watu wanaofuatilia channel yako haraka.

5.Je, Niruhusu Maoni kwenye Video Zangu?
Kuruhusu watu kutoa maoni na kuuliza maswali kwenye video zako za YouTube kutawahimiza kushiriki uzoefu wao na kampuni yako na itaonyesha kuwa uko tayari kupokea maoni yao. Unaweza kufanya maoni yaonyeshwe kiotomatiki, au tu baada ya kuwa umeyaidhinisha.

Kuanzisha Channel ya YouTube kwa ajili ya biashara yako ni njia nzuri ya kukuza brand yako na biashara yako kwa ujumla. Hivyo, kujiuliza maswali haya kabla ya kuanzisha channel yako kunaweza kukuweka kwenye njia ya mafanikio.

Nimatumaini yangu umepata maarifa ya kutosha ambayo yatakusaidia kupata mafanikio unapokuwa umeanzisha channel yako ya YouTube. Kama una maoni au swali lolote usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

Hatua 7 Za Kufuata Ili Uweze Kufikia Uhuru Wa Kifedha.

Uhuru wa kifedha

Katika maisha lengo moja ambalo sote tunalo sawa ni kwamba, sote tunataka kuwa na kipato zaidi ili tuweze kuwa na uhuru wa kifedha. Hata hivyo, ni asilimia ndogo tu kati yetu tunapata uhuru wa kifedha tunaotamani. Sote tunataka kuwa na pesa za kutosha ili tuwe na maisha bora. Swali pekee ni, “Je, uko tayari kuwa na uhuru wa kifedha?” Habari njema ni kwamba kuna watu wengi zaidi wanaopata uhuru wa kifedha haraka zaidi kuliko hapo awali. Kupitia mipango sahihi ya kifedha pamoja na utekelezaji makini unaweza kuboresha kipato chako na kuwa miongoni mwa watu wenye uhuru wa kifedha . Katika makala ya leo nitakushirikisha hatua saba za kufuata ili uweze kukuza kipato chako na kuwa na uhuru wa kifedha.

Kanuni ya kuwa na Uhuru wa Kifedha
Uhuru wa kifedha unamaanisha kuwa una uwezo wa kuishi maisha yako bila kuwa na wasiwasi wa kupungukiwa au kuishiwa na fedha. Ikiwa uko tayari kupata uhuru wa kifedha, hapa kuna Kanuni yenye vipengele saba unayoweza kutumia ili kukusaidia kukusanya mali, kuwa na furaha zaidi, na kupata uhuru wa kifedha katika miaka ijayo.

1.Anza Kuwa na mtizamo chanya Kuhusu fedha.
Hatua ya kwanza ya kuwa tajiri na kupata uhuru wa kifedha inahusisha kuwa na mtizamo chanya kuhusu fedha. Kufikiria vibaya kuhusu fedha ni kikwazo cha kihisia ambacho lazima ukiondoe ili uweze kufikia uhuru wa kifedha. Lazima uondoe mawazo kwamba, kuwa na pesa nyingi husababisha uovu au kwamba, pesa haiwezi kununua furaha. Unapoanza kuwa na mtizamo chanya kuhusu pesa, utavutia fursa na kufungua milango zaidi ya kutengeneza kipato.

2.Andika Upya Malengo Yako Makuu ya Uhuru wa Kifedha
Jiwekee malengo ya kifedha. Andika upya na uhakiki malengo yako kwenye karatasi kila siku na ufikirie jinsi unavyoweza kuyatimiza. Hii itakuchukua kati ya dakika tano mpaka kumi. Kitendo cha kuandika upya malengo yako, na kuyafikiria kila asubuhi kabla ya kuanza ratiba yako ya siku nzima, kutaongeza nafasi zako za kuyatimiza.

3.Panga Ratiba Yako Ya Siku.
Panga ratiba yako ya siku mapema. Wakati mzuri wa kufanya hivyo ni usiku uliopita. Kitendo chenyewe cha kupanga kila siku, kila wiki, na kila mwezi mapema mambo ambayo utayafanya, kitakufanya uwe na hamasa zaidi na makini zaidi katika kila kitu unachofanya.Unapoweka mambo utakayofanya kwenye orodha, utaweza kujidhibiti ili ufanye tu mambo ambayo umeyakusudia kwa muda husika. Unapopanga kila siku mapema utaweza kudhibiti na kufuatilia tabia zako za matumizi pia. Panga kiasi unachopaswa kutumia kwa wiki, mwezi, au mwaka na uamue ni kiasi gani utaweza kuweka akiba.
Kwenye pesa yako uliyoitenga Kwa ajili ya akiba, weka sehemu ya pesa hivyo kwenye akaunti ya akiba, nyingine kwenye hazina ya dharura, nyingine kwa ajili ya kulipia madeni Pia unaweza kufikiria kutenga sehemu yako ya akiba kwa ajili ya kuwekeza kwenye soko la hisa na mifuko ya pamoja ya uwekezaji.

4.Kanuni ya Kuzingatia
Zingatia kwa nia moja, kila saa ya kila siku, inatumika vyema kwa ajili ya malengo uliyojiwekea. Kanuni ya umakini ni muhimu kabisa kufikia uhuru wa kifedha. Hakikisha kuwa kila kitu unachokifanya katika suala la kuweka malengo na mipango ya kifedha, kinalenga kukuwezesha kuamua jambo moja au mawili ambayo unapaswa kuzingatia zaidi kuliko kitu kingine chochote. Mambo unayozingatia zaidi na kutumia muda mwingi kufanya yanapaswa kuwa katika upatanishi wa moja kwa moja na malengo yako ya kifedha.Tumia muda wako kuzingatia kile kitakachokutengenezea pesa nyingi zaidi.

5.Wekeza Ndani Yako
Sikiliza programu za sauti za mafunzo mbalimbali kuhusu fedha kwenye gari lako. Kwa kugeuza gari lako kuwa chuo kikuu cha magurudumu, unaweza kuwa mmoja wa watu wenye ujuzi zaidi katika taaluma yako.
Nunua kozi za usimamizi wa fedha, soma vitabu kuhusu maendeleo binafsi ya kifedha na utafute makala mtandaoni kuhusu fedha. Unaweza hata kuwekeza kwako mwenyewe kwa kupata ushauri kutoka kwa mshauri wa kifedha. Baada ya muda utakuwa na maarifa mengi katika eneo la fedha kiasi kwamba watu watakuja kwako kutaka ushauri.

Jiulize Maswali Haya Ya Ajabu.
Jiulize “Maswali ya ajabu” mawili baada ya kila tukio muhimu maishani mwako.
Swali la kwanza ni, “Nilifanya nini Kwa usahihi?”

Na swali la pili ni, “Nitafanya nini Kwa namna tofauti, wakati ujao?”

Kwa kukagua utendaji wako mara baada ya kila tukio muhimu maishani mwako kama vile, mkutano, simu ya mauzo, na uwasilishaji, utakuwa bora haraka kuliko unavyoweza kufikiria. Majibu ya maswali haya yote mawili ni chanya. Kwa kukagua ulichofanya vizuri na kile ambacho ungefanya kwa njia tofauti wakati ujao, unapanga akilini mwako mwelekeo wa kuwa bora zaidi wakati ujao. Ikiwa utachukua dakika chache na kuandika kila kitu ulichofanya kwa usahihi na kila kitu ambacho ungefanya kwa njia tofauti mara tu baada ya tukio muhimu kama vile, simu au wasilisho, utajifunza kukua na kuboresha kazi yako kwa haraka zaidi. Unapojitathimini na kufanya maboresho kwenye kazi yako, kwa kweli, kutaboresha pia pesa ambazo utakuwa unapata.

7.Kuwa Mkarimu kwa Wengine
Jambo la mwisho ni kumtendea kila mtu unayekutana naye kama mteja wa mamilioni. Mtendee kila mtu, nyumbani na kazini, kana kwamba ndiye mtu muhimu zaidi ulimwenguni. Kwa kuwa kila mtu anaamini kwamba yeye ndiye mtu muhimu zaidi ulimwenguni, unapomtendea kana kwamba ndiye mtu wa thamani na muhimu kuliko wote, atathamini kwa jinsi ulivyomtambua na kumthamini na hivyo atakupenda na huduma yako au bidhaa yako pia ataipenda. Ni ukweli uliothibitishwa kwamba kuwa mtu mkarimu zaidi kutakusaidia kuvutia utajiri zaidi na kuwa mtu mwenye furaha zaidi.

Jinsi ya Kuokoa Pesa na Kupata Uhuru wa Kifedha.

Uhuru wa kifedha

Katika jambo hili, ninapendekeza mchakato wa polepole wa kujifunza kuokoa pesa. Kwa kuanzia, anza na 1% ya mapato yako na kuishi kwa 99% nyingine.
Kwa mfano, ikiwa unapata Tsh.200,000 kwa mwezi, fanya uamuzi leo wa kuokoa Tsh.2000 kwa mwezi. Kisha unaweza kuishi kwa kutumia Tsh.198, 000 nyingine. Okoa pesa kwa muda mrefu kwa kufungua akaunti tofauti ya benki, akaunti yako ya “uhuru wa kifedha”.
Mara tu unapoweka pesa kwenye akaunti hii ya akiba/uwekezaji, hutazitoa au kuzitumia kwa sababu yoyote ile.

Mara tu unapokuwa na maisha mazuri kwa 99% ya mapato yako, ongeza kiwango chako cha akiba cha kila mwezi hadi 2% na kuendelea.
Ndani ya mwaka mmoja, utajikuta unaishi kwa raha kabisa kwa 98% ya mapato yako ya sasa.

Endelea na mchakato huu hadi uokoe 15% na kisha 20% ya mapato yako. Hutaona hata tofauti katika kiwango chako cha maisha kwa sababu badiliko litakuwa ni la taratibu sana. Lakini tofauti katika maisha yako ya kifedha itakuwa ya kushangaza kabisa.

Kwa leo niishie hapo. Ni matumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kupiga hatua kuelekea kwenye uhuru wa kifedha. Kama una swali au maoni yoyote, usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa simu namba 0752 081669. Asante na karibu kwenye makala zijazo.

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp