Kutengeneza Pesa Kupitia Blog: Mambo 6 Ya Kuzingatia.

Kutengeneza Pesa Kupitia Blog: Mambo 6 Ya Kuzingatia.

Hivi unajua kuwa watu wengi wanashindwa kuanzisha na kumiliki blog kwa kudhani kuwa ni kitu kigumu na kisichowezekana? Lakini ukweli ni kuwa kuanzisha na kumiliki blog ni jambo rahisi kuliko unavyoweza kufikiria. Hivyo katika makala hii nitakuelezea mambo sita ya msingi ya kuzingatia ili uweze kuwa na blog yenye mafanikio na Kutengeneza pesa kupitia blog yako.

Katika makala iliyopita iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho “Sababu kumi za msingi za wewe kuwa na blog yako mwenyewe ambayo itakuingizia kipato“, nilielezea kwa kina maana halisi ya blog na pia nilifafanua sababu za msingi ambazo wewe mpendwa msomaji wangu unapaswa kuwa na blog yako mwenyewe na namna ambavyo itakunufaisha na kuwa chanzo cha kukuingizia kipato.Kama hukuisoma makala hiyo nakushauri uanze kwanza kuisoma makala hiyo halafu ndio uendelee na makala hii.

Ili uweze kuanzisha blog na kutengeneza pesa kupitia blog yako, unapaswa kuzingatia na kufanyia kazi mambo yafuatayo :

Kutengeneza pesa kupitia blog: Mambo 6 ya kuzingatia.

1.Andika makala nyingi iwezekanavyo.

Ili uweze kufanikiwa kutengeneza pesa kupitia blog yako, unapaswa kuandika makala nyingi iwezekanavyo. Jiwekee ratiba na uifuate ya kuandika makala kila siku au kila baada ya siku mbili. Jambo la msingi ni kuwa, blog yako isikae muda mrefu bila kuweka makala mpya.

2. Penda Kusoma Sana

Ili uweze kuwa na vitu vingi vya kuandika kwenye blog yako, unapaswa kusoma sana kuhusiana na mada unazoandikia blog yako.

3. Wapende na kuwathamini wasomaji wako.

Jambo jingine la kuzingatia ili uweze kutengeneza pesa kupitia blog, jitahidi kusoma na kujibu maoni na maswali ya wasomaji wako mara tu yanapotokea. Kwa kufanya hivyo wasomaji wako watakupenda na kukuheshimu.

4. Usiogope kuandika.

Ili uweze kufanikiwa kutengeneza pesa kupitia blog, unapaswa kutokuogopa kuandika maarifa uliyonayo kuhusiana Mada unazoandikia blog yako. Usiwaze watu watakufikiriaje. Kumbuka kuwa maarifa au ujuzi ulionao ni wa thamani sana kwa mtu fulani na kwamba akiupata utamsaidia na atakushukuru.

5. Penda kujifunza vitu vipya kila siku kuhusiana na ujuzi wako.

Jambo jingine la kuzingatia ili uweze kutengeneza pesa kupitia blog ni kutambua kuwa wewe huwezi kuwa unajua vitu vyote, hivyo unapaswa kujifunza vitu vipya kila siku ili uweze kuandika makala bora na zenye kugusa jamii.

6. Kuwa na subira.

Mafanikio katika blog hayapatikani kwa siku moja. Hivyo endelea kuandika makala nyingi iwezekanavyo zinazoelimisha jamii,watu watakupenda,watakuheshimu na kukuthamini na matokeo yake utayaona baadaye.

Kwa leo niishie hapo. Kama una maoni au swali lolote kuhusiana na makala hii ya jinsi ya kutengeneza pesa kupitia blog, usisite kuandika hapo chini. Au unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kupitia namba yangu ya whatsap 0752081669.

Asante na karibu katika makala ijayo.

Hatua 6 Za Kuanzisha Blog.

Hatua 6 Za Kuanzisha Blog.

Karibu mpendwa katika makala hii. Katika makala hii nitazungumzia hatua 6 za kufuata ili uweze kuanzisha na kumiliki blog itakayokuletea pesa mtandaoni.Hivi unajua kuwa kwa kuanzisha blog unaweza kutumia elimu au ujuzi ulionao kujiingizia kipato mtandaoni bila kuathiri shughuli zako zingine?

Katika makala zilizopita nilielezea maana ya blog na sababu za msingi za wewe kuwa na blog yako mwenyewe. Kama hujapitia makala hiyo unaweza kuipitia halafu ndio uendelee na makala hii. Katika makala hii nitakuelezea hatua sita muhimu za kufuata ili uweze kuanzisha na kumiliki blog itakayokuletea kipato mtandaoni.

1. Chagua Mada (niche) utakayokuwa ukiandikia makala zako.

Hatua ya kwanza kabisa unapotaka kuanzisha blog ni kuchagua mada (niche). Blog nyingi huwa zinaelezea Mada moja. Kwa mfano, kuna blog zinazoandika michezo, habari, afya, elimu na mada zingine nyingi. Hivyo kama wewe una ujuzi wowote, chagua mada ya kuandika kwenye blog yako. Usichanganye mada nyingi kwenye blog yako.

2. Chagua Sauti yako ya kiuandishi (choosing your own voice)

Kitu kizuri sana ninachokipenda kwenye blog ni kuwa, kila mwandishi ana mfumo wake. Hivyo unaweza kuchagua mfumo wowote wa kiuandishi katika blog yako. Kwa mfano : unaweza kuwa unaandika makala katika mfumo wa kitaalamu au unaweza ukawa unaandika makala za kawaida.

3. Chagua vitu vya kuandika kwenye blog yako.

Baada ya kuchagua Mada ya kuandika kwenye blog yako, hatua inayofuata ya kuanzisha blog ni kuchagua mambo ambayo utaandika na yale ambayo hutaandika.

4. Andika makala nzuri na zenye mvuto.

Ili uweze kuwa na wasomaji endelevu kwenye blog yako, unapaswa kuandika makala zenye mvuto na zinazotatua matatizo ya jamii.

5. Tambua aina za makala utakazoandika.

Hatua nyingine ya kuanzisha blog ni kuchagua mtindo wa makala zako. Kuna aina nyingi za mitindo ya uandishi wa makala baadhi yake ni hii ifuatayo :

Mtindo wa kuorodhesha (List) .

Kwa mfano :Mambo sita ya kufanya ili uweze kufanikiwa katika maisha.

Mtindo wa kuandika dondoo (Tips)

Kwa mfano :Ukitaka kufauru mtihani, zingatia mambo yafuatayo.

Mtindo wa kuelezea (review) huduma au bidhaa .

Mfano :Maelezo kuhusu simu ya IPhone 6.

Mtindo wa kupendekezea (recommendation) bidhaa au huduma.

Mfano :Ukitaka kupiga picha zenye ubora camera ya cannon itakufaa.

Mtindo wa ‘jinsi ya ‘(how to)

Mfano :Jinsi ya kuanzisha blog.

Mtindo wa mahojiano (interview)

Mfano :Kutana na Bilionea Maganga aliyeanza biashara yake kwa kuuza ubuyu.

Mtindo wa kutumia video

Mtindo wa kurekodi sauti (podcast)

Mtindo wa kualika wataalam wa mambo mbalimbali (guest post) kuandika makala kwenye blog yako.

6. Weka ratiba nzuri ya kuweka makala zako.

Weka ratiba nzuri ya kuweka makala zako. Ninakupendekezea uwe unaweka makala kila siku, kila baada ya siku mbili, mara mbili kwa juma n.k. Jambo la msingi la kuzingatia hapa ni kuwa na ratiba maalumu ya kuweka makala zako ili uweze kuwa na wasomaji wengi watakaofuatilia blog yako.

Nimatumaini yangu kuwa umejifunza kitu katika makala hii ya hatua za kuanzisha blog. Kwa maoni au swali au ushauri, usisite kuwasiliana nami kwa whatsap 0752081669. Au unaweza kuweka maoni yako hapa chini.

Karibu katika makala ijayo

Jinsi Ya Kuongeza Wasomaji Kwenye Blog Yako.

Jinsi Ya Kuongeza Wasomaji Kwenye Blog Yako.

Mpendwa, nikukaribishe tena katika makala hii. Katika makala ya leo nitazungumzia jinsi unavyoweza kuongeza wasomaji kwenye blog yako. Njia nitakazoeleza hapa zitakusaidia kuongeza maradufu wasomaji wa blog yako na hivyo kupata mafanikio kwenye blog yako.

Soma:Kuanzisha blog: Sababu 10 za kuanzisha Blog yako.

Jinsi ya kuongeza wasomaji kwenye blog yako.

1. Andika makala mara kwa mara kwenye blog yako.

Weka makala mpya mara kwa mara kwenye blog yako. Unaweza kuandika makala, ukaposti picha au ukaweka makala za sauti (Podcasting).

Weka ratiba maalumu kwa ajili ya kuweka makala mpya kwenye blog yako.Ratiba husaidia kuwafanya wasomaji wako wajue ni wakati gani wategemee makala mpya.

2. Wasikilize wasomaji wako na ujibu maoni au maswali yao.

Miongoni mwa vitu vizuri sana ambavyo unaweza kuvifanya kwa wasomaji wako ni kuhakikisha kuwa kila msomaji wako anafurahia kuwa kwenye blog yako. Weka kwenye blog yako ukurasa wa mawasiliano ili kama kuna swali uweze kulijibu haraka iwezekanavyo. Kama kuna maoni yoyote kwenye makala zako, jitahidi kuyajibu haraka. Kwa kufanya hivyo, utaweza kuongeza wasomaji kwenye blog yako.

3. Tembelea Blog zingine na majukwaa mbalimbali na uchangie mada zinazotolewa.

Ili uweze kuwa na wasomaji wengi kwenye blog yako, unatakiwa kushiriki kwenye blog za watu wengine kwa kuchangia maoni yako. Tafuta blog zinazoandika makala kama zako na uwe unatoa maoni yako. Unapokuwa unatoa maoni usisahau kutaja blog yako. Kwa kufanya hivyo utafanya blog yako kutambulika na hivyo kupata wasomaji wengi.

4. Alika miongoni mwa wasomaji wako kuandika makala.

Pia, ili uweze kuongeza wasomaji, unaweza kualika miongoni mwa wasomaji wako kuandika makala. Hii itasaidia kuifanya blog yako kuwa na makala zenye ladha tofauti.

5. Wasiliana na wasomaji wako kwa njia ya email.

Waalike wasomaji kujisajiri (subscribe) ili waweze kupata taarifa kila unapoweka makala mpya. Kuna namna nyingi ya kufanya wasomaji wajisajiri ili kupata taarifa kila unapoweka makala. Mojawapo ya njia hizo ni kuweka kifaa cha kukusanyia taarifa za wasomaji wako kama vile jina na baruapepe (email). Hivyo msomaji anapokuwa amependezwa na makala zako atajisajiri ili aweze kupata taarifa kila unapoweka makala mpya. Mfano wa kifaa hicho ni MailChimp

6. Unganisha blog yako na mitandao ya kijamii.

Miongoni mwa njia bora kabisa za kuongeza wasomaji wa blog yako ni kuiunganisha na mitandao ya kijamii kama vile facebook, twitter, Pinterest na LinkedIn .Mitandao hii ina watu mamilioni. Hivyo unapokuwa na kurasa kwenye mitandao hii na ukawa unashea makala zako, utapata wasomaji wengi.

7. Shirikisha wasomaji wako kutoa maoni yao kwa kuwauliza maswali.

Shirikisha wasomaji wako kwa kuwauliza maswali mbalimbali kuhusiana na makala unazotoa ili watoe maoni yao. Unaweza kukusanya maoni ya wasomaji kwa kuweka kifaa kinachoitwa Survey Monkey kwenye blog yako.

8. Zingatia blog yako kuonekana vizuri kwenye simujanja (smartphone).

Hakikisha kuwa blog yako inaonekana vizuri kwenye smartphone ili uweze kupata wasomaji wengi kwani kwa sasa watu wengi wanatumia simu za mkononi.

9. Andika mada tofauti tofauti kwenye blog yako.

Ili uweze kuongeza wasomaji wengi, unaweza kuchanganya mada tofauti tofauti kwenye blog yako. Lakini zingatia mada hizo ziwe zinaendana na malengo ya blog yako. Kwa mfano blog yako inahusu biashara, unaweza kuandika makala ya namna ya kuanzisha biashara, lakini pia unaweza kuchanganya makala kama vile namna ya kutangaza biashara kwenye mitandao ya kijamii n.k

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ambayo yatakusaidia kuboresha blog yako. Kwa maoni au ushauri usisite kuweka maoni yako hapa chini. Lakini pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa njia ya whatsap 0752081669.

Asante na karibu katika makala ijayo.

Jinsi Ya Kukuza Blog Yako: Mambo 10 Ya Kuzingatia.

Jinsi Ya Kukuza Blog Yako: Mambo 10 Ya Kuzingatia.

Mpendwa, karibu sana katika makala hii. Katika makala hii nitaelezea Jinsi ya kukuza blog yako. Nitazungumzia mambo kumi ya msingi unayotakiwa kuyafanya ili uweze kuwa na blog bora ambayo itakuwa ni chanzo cha kukuletea pesa (kipato) .

Jinsi ya kukuza blog yako: Mambo kumi ya kuzingatia.

1. Tambua sauti yako.

Blog yako inakuwakilisha wewe mtandaoni. Hivyo, kila unachoandika kinawakilisha mawazo yako na hivyo kukutofautisha wewe na watu wengine. Hivyo unatakiwa kuchagua mtindo wa uandishi wa makala zako. Unapokuwa unafikiria mtindo wako wa uandishi, jiulize mwenyewe maswali yafuatayo :

unataka wasomaji wa makala zako wawe ni watu wa aina gani?

Unahitaji kuwa na blog ya kufundisha ujuzi gani?

2. Weka blog yako kuwa ni miongoni mwa majukumu yako ya kila siku.

Maisha yanabadilika. Unaweza kupata kazi mpya au kubadilishiwa majukumu, unaweza kupata watoto na hivyo majukumu yako kuongezeka. Ili uweze kukuza blog yako, hakikisha kuwa, hata kama utakuwa na majukumu mengi, weka pia blog kuwa miongoni mwa majukumu yako ya msingi. Kwa kufanya hivyo utaifanya blog yako kuwa ni sehemu ya kazi kama kazi zingine na hivyo blog yako itakuwa bora na yenye watembeleaji .

3. Uliza wasomaji wako kutoa maoni kuhusiana na makala zako.

Kila mwisho wa makala zako, wahamasishe wasomaji wako kutoa maoni kuhusiana na mada uliyoandika. Hii itakusaidia kujenga mahusiano mazuri na wasomaji wako na pia kujua mahitaji yao. Kila maoni au maswali yanapotolewa, hakikisha unayajibu kwa wakati.

 4. Tambua blog zingine zinazoandika makala zinazofanana na zako

Angalia blog zilizofanikiwa zinazoandika makala kama za kwako na ujifunze kutoka kwao, pia jiunge na majukwaa mbalimbali yanayojadili mada unazotoa. Hii itakuongezea ujuzi katika mada unazoandika.

5. Chunguza Takwimu na vyanzo vya watembeleaji wa blog yako.

Kuna faida nyingi za kujua vyanzo vya watembeleaji wa blog yako. Utajua watembeleaji wako wengi wanatoka sehemu gani, makala zipi zilizotembelewa zaidi na mambo mengine. Hii itakusaidia kujua ni mada zipi zinazopendwa zaidi na hivyo kukusaidia kujua ni mada zipi uendelee kuziandikia katika makala zako zijazo.

6. Weka malengo ya blog yako

Ili uweze kukuza blog yako, unatakiwa kuweka malengo ya blog yako yanayopimika ili uweze kujua kama blog yako inakua au la. Weka malengo mepesi kupimika kama vile

Kuongeza wasomaji: Kwa mfano : Ninahitaji kupata wasomaji wapya 50 kila mwezi kwenye blog yangu.

Ratiba ya kuweka makala kwenye blog: Kwa mfano : Nitakuwa nikiweka makala mpya moja kila siku kwenye blog yangu.

Kufungua na kutumia mitandao ya kijamii: Kwa mfano : Nitafungua kurasa kwenye facebook, twitter, na instagram. Pia nitakuwa nikishea makala mpya za blog yangu kwenye mitandao hiyo ya kijamii.

Kujipatia kipato: kujipatia kipato kwenye blog yako ni lengo la muhimu ambalo unatakiwa kuliweka. Kwa mfano : Baada ya mwaka mmoja blog yangu ianze kuniingizia kipato cha shilingi million moja kila mwezi kutokana na matangazo pamoja na kuuza bidhaa mbalimbali pamoja na huduma.

7. Weka viashiria vya mafanikio ya malengo yako.

Weka viashiria vya mafanikio ya malengo ya blog yako ili uweze kujua wapi umefikia. Kwa mfano : Uliweka malengo ya kuongeza wasomaji wapya 50 kila mwezi. Pima mafanikio kwa kuangalia takwimu za watembeleaji wa blog yako.

8.Weka malengo ya namna ambavyo blog yako itakuingizia kipato.

Kila mmiliki wa blog ni hitaji lake kuona blog yake ikimuingizia kipato cha kujikimu kimaisha. Hivyo ili uweze kukuza blog yako, unapaswa kuweka malengo ya namna gani blog yako itakuingizia kipato.Kwa mfano :

Je una malengo ya kutumia mfumo wa matangazo (ads) kukuingizia kipato? Je ni aina gani ya matangazo utaweka?

Je una mpango wa kuingia ubia na watu binafsi au makampuni kuweka matangazo yao?

Je una mpango wa kuuza bidhaa zako wewe mwenyewe kwenye blog yako kama vile vitabu au kozi mbalimbali kutokana na ujuzi wako?

Je una mpango wa kutumia blog kama jukwaa la kujitangaza kuwa wewe ni mtaalam katika jambo fulani ili watu wakutambue na kukupatia tenda za kazi mbalimbali ili uweze kuwafanyia na kujipatia kipato?

9.Anza kidogo na jipe muda kukuza blog yako.

Unaweza kuanza blog yako bila gharama yoyote kwa kutumia blogger halafu kadiri blog yako inavyozidi kukua unaweza kuihamishia kwenye mifumo mingine ya hali ya juu zaidi kama vile wordpress.

10.Kila unapopiga hatua moja, fanya tathmini.

Kwa sababu kazi ya blog ni endelevu, hivyo, ili uweze kukuza blog yako, jenga utamaduni wa kutathimini kila hatua unayopiga kufanikisha malengo uliyojiwekea kisha boresha zaidi.

Kwa leo niishie hapo. Kama una swali lolote au maoni kuhusiana na makala hii, usisite kuandika hapa chini. Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa njia ya whatsap 0752081669.

Asante sana na karibu katika makala ijayo.

Sababu 10 Za Kuanzisha Blog Yako.

Sababu 10 Za Kuanzisha Blog Yako.

Kama unafikiria kuanzisha blog lakini huna uhakika kama uko sahihi na uamuzi wako, usiwe na wasiwasi kwani makala hii inakwenda kukupatia majibu yote ambayo yamekuwa yakikutatiza. Katika makala hii nitakushirikisha sababu 10 za kuanzisha blog. Basi karibu tuendelee .

Je Ninapaswa Kuanzisha Blog? Sababu 9 kwa nini unapaswa kuanzisha na kuwa na Blog yako mwenyewe. (na maswali 7 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog)

  1. Sababu 6 za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe.
  2. Sababu 3 ambazo sio za msingi za wewe kuanzisha blog (Kama una sababu hizi usianzishe blog)
  3. Maswali 7 ya muhimu unayopaswa kujiuliza kabla ya kuamua kuanzisha blog.
  4. Sasa fanya maamuzi.

Katika Makala hii tunaenda kuangalia maswali muhimu na ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha blog. Lakini kabla hatujaendelea na maswali hayo, hebu kwanza tuangalie sababu za msingi za wewe kuwa na blog yako mwnyewe.

Tutaangalia sababu 6 za msingi za wewe kuwa na blog yako mwenyewe. Lakini pia tutaangalia sababu 4 ambazo sio za msingi.

 Sasa hebu tuendelee.

1. Sababu 6 za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe.

Kama una miongoni mwa sababu hizi au nzuri zaidi ya hizi za wewe kuanzisha blog , basi ukianzisha blog utafanikiwa sana.

Sababu ya msingi #1: Unahitaji kuandika na kufundisha watu kuhusiana na mada unayoipenda.

Kama una ujuzi ,au mada unayoipenda na unahitaji kuwashirikisha watu ujuzi wako, ukiamua kuanzisha blog na kufundisha watu ujuzi wako unaoupenda, utafanikiwa sana kwenye kazi yako ya blog.

Sababu ya Msingi #2: Unahitaji kuanzisha na kujenga Biashara kupitia mtandao wa internet.

Inawezekana unahitaji kuanzisha blog ukiwa na sababu ya kuanzisha biashara yako na kuitangaza kuipitia mtandao wa internet. Au inawezekana tayari una biashara na kupitia kuanzisha blog,unahitaji kutangaza biashara yako ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi.

Pia kupitia blog unaweza kujiajiri na kutengeneza kipato.Kwa mfano,unaweza kuuza maarifa yako mtandaoni kwa kuuza kozi mbalimbali, vitabu pepe (ebooks) au kuuza ushauri wako wa kitaalamu kwa watu.

Sababu ya msingi #3: Unahitaji kutengeneza Brand yako.

Blog ni njia nzuri sana ya kukuza jina lako na kulifanya litambulike na kuwa maarufu kwa watu. Hivyo, kama unataka watu na jamii kwa ujumla wakutambue, anzisha blog na uwasaidie watu kutatua matatizo yao kupitia kuandika makala kwenye blog yako.

Sababu ya Msingi #4: Unahitaji kutatua changamoto zinazoikabili jamii na kufanya maisha ya watu yabadilike.

Kama utaanzisha blog ili kutatua matatizo ya watu utafanikiwa sana kwani watu wana changamoto nyingi zinazowakabili na wanahitaji mtu atakayeweza kutatua changamoto zao.Hivyo kama unahitaji kuanzisha blog ili kuweza kubadilisha maisha ya watu,nakutia moyo songa mbele kwani utafanikiwa sana katika kazi yako.

Sababu ya msingi #5: Unahitaji kujiajiri na kujipatia kipato kupitia maarifa,ujuzi au hobby yako.

Pia sababu nyingine unaweza kuanzisha blog ili kujiajiri na kutumia ujuzi ulionao kufundisha watu na kujipatia kipato mtandaoni.

Soma:Njia 9 za kutengeneza kipato kupitia blog.

Sababu ya Msingi#6: Unafurahia Kujifunza Vitu Vipya Kila Siku.

Unapoanzisha blog umeanza safari ndefu ya uandishi. Hivyo utatakiwa ujifunze vitu vipya kila siku ili uweze kubobea kwenye mada unayofundisha.

2. Sababu 3 ambazo sio za msingi za wewe kuanzisha blog(Kama una sababu hizi usianzishe blog)

Pamoja na kuwa sababu nilizozielezea hapo juu ni za msingi za wewe kuanzisha na kuwa na blog yako mwenyewe, Sababu zifuatazo sio za msingi. Hivyo, kama una sababu hizi ninazoenda kuzielezea sasa au zinazofanana na hizi, usianzishe blog kwani itakuwa vigumu sana kwako kufanikiwa.

Sababu isiyokuwa ya msingi #1: Unahitaji kutengeneza Pesa Haraka.

Kama unahitaji kuwa n blog kwa lengo la kutengeneza pesa haraka ,basi unaweza kushindwa kufikia malengo yako. Hii ni kwa sababu ili uweze kutengeneza pesa kupitia blog unapaswa kujipa muda kuijenga blog yako kwa kuweka makala mara kwa mara ili ujenge mahusiano na wasomaji wako. Hivyo, kama utaweka nguvu katika kuandika makala za kuelimisha jamii, watu watakupenda na hivyo watakuwa tayari utakapoamua kuwauzia bidhaa au huduma unayotoa.

Sababu isiyokuwa ya msingi #2: Huna kitu cha kuelimisha bali unahitaji kuwa unaweka mambo maisha yako binafsi mtandaoni.

Kama unahitaji kutengeneza kipato kupitia blog kuandika maisha yako binafsi haitakusaidia kukuza blog yako. Kumbuka kuwa watu huwa wanaingia mtandaoni kujifunza maarifa ambayo yatatatua changamoto zao.Hivyo ukianzisha blog ili kuweka mambo yako binafsi hutaweza kukuza blog yako.

Hata hivyo, unaweza kuanzisha blog kutokana na hobby yako ambayo unahisi itakuwa msaada kwa watu kutatua changamoto zao.

Sababu isiyokuwa ya msingi  #3: Huwa unasoma blog nyingi na unaona ni fahari na wewe kumiliki blog.

Inawezekana ukaona kuwa kwa kuwa unapenda kusoma Makala kwenye blog mbalimbali na wewe ukafikiria kuwa na blog yako mwenyewe. Japokuwa sababu hii sio mbaya ,lakini sio sababu ya kutosha kwa wewe kuanzisha blog. Wazo hili ni sawa na la mtu anayependa kuangalia movie halafu akatamani na yeye awe muigizaji. Kuanzisha blog kunahitaji kujitoa kiasi cha kutosha kusoma na kuandika Makala mara kwa mara kama unataka kufanikiwa kwenye kazi hii. Hivyo kusema tu kuwa kwa kuwa unapenda kusoma blog mbalimbali na wewe unahitaji kuwa na blog yako mwenyewe haitoshi kukufanya na wewe uanzishe blog. Kama unataka kuanzisha blog  unapaswa kutafakari Zaidi na uwe na sababu za msingi kama nilizoziainisha hapo kabla.

Hatari nyingine ya kuanzisha blog kwa sababu tu unapenda kusoma blog zingine ni kuwa , kwa kuwa utakuwa huna maandalizi na sababu za msingi za wewe kuwa na blog utaishia kunakiri (copy and paste) blog zile unazopenda kuzisoma.

Maswali 7 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog.

Sasa tayari umefikiria kwa kina na umeona kuwa una sababu za msingi za kuanzisha blog. Je uendelee mbele au unaenda kupoteza muda wako bure?

Hapa nimekuwekea Maswali 8 ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla ya kuanzisha Blog.

Swali #1: Je umechagua mada unayoipenda?

Unapokuwa umechagua mada unayoipenda, hiyo ni hatua ya kwanza kuelekea mafanikio. Hii ni kwa sababu unapoanzisha blog, utaendelea kuweka Makala kwa miaka mingi ijayo. Hivyo ukiwa umechagua mada unayoipenda , utakuwa unafurahia kuandika mara kwa mara na kusoma zaidi kujiongezea ujuzi kwenye mada yako.

Swali #2: Je una ujuzi wa kutumia computer na mtandao wa internet?

Hapa sizungumzii kuwa uwe umesoma sana kuhusiana na mambo ya computer,ninachosema ni ule uelewa tu wa msingi wa jinsi ya kutumia internet.

Swali #3: Je utakuwa na muda na nguvu ya kutosha kuandika Makala?

Jambo jingine la msingi unalopaswa kujiuliza ni kuwa ,utakuwa na muda na nguvu kuendesha blog yako? Kumbuka kuwa ili uwe na blog yenye mafanikio, unapaswa uwe unaweka Makala mara kwa mara. Hivyo unapaswa ujiulize na uwe mkweli kwenye nafsi yako kama utaweza kuwa na muda wa kuandika Makala za blog yako.

Swali  #4: Jinsi gani utatengeneza kipato (pesa) kupitia blog yako?

Jambo jingine la msingi unalopaswa kulifikiria ni kuwa , ni jinsi gani utatengeneza kipato kupitia blog yako.Je utakuwa ukiuza kozi mbalimbali ulizoandaa,vitabu pepe au utakuwa ukitoa huduma ya ushauri na watu wakakulipa? Au utatumia blog yako kuuza bidhaa zako mwenyewe au kutangaza bidhaa za makampuni mengine na wewe ukapata gawio (commission)? Kimsingi kuna njia nyingi sana ambazo unaweza kuzitumia kwenye blog yako kupata kipato. Hivyo unapaswa kufikiria jinsi ambavyo blog yako itakuingizia kipato toka siku ya kwanza unapoianzisha.

Swali#5: Utakuwa ukiandaa Makala za aina gani?

Kwa kuwa Makala ndio msingi wa blog, hivyo unapaswa kufikiria Makala zako zitakuwa za aina gani. Je ni kurekodi video au kuandika Makala? Na Je utakuwa ukiandika Makala zenye urefu gani?

Hivyo, unapaswa kujiuliza jambo hili mapema kabla ya kuanzisha blog yako.

Swali #6: Utapimaje maendeleo ya blog yako?

Kuna njia nyingi za kupima maendeleo ya blog yako.

Kama lengo lako si kutengeneza pesa bali ni kuelimisha jamii, unaweza kupima maendeleo ya blog yako kwa kuangalia ongezeko la idadi ya watembeleaji kwenye blog yako na ongezeko la email za watu waliojiunga na blog yako.

Kama lengo lako ni kujiajiri na kutengeneza kipato kupitia blog utapima maendeleo ya blog yako kwa kuangalia ni kiasi gani cha pesa unatakiwa uwe umepata kupitia blog kwa kipindi ulichojiwekea. Inaweza kuwa mwezi au mwaka.

Swali #7: Utakuwa ukiweka Makala mpya kila baada ya muda gani?

Kabla ya kuanzisha blog unatakiwa pia kujua ratiba yako ambayo utaitumia kuweka Makala kwenye blog yako. Inaweza kuwa mara moja kila siku au mara moja kwa juma n.k . Hii itawafanya wasomaji wako kujua wakati maalumu ambao wakiingia kwenye blog yako watapata maarifa mapya.

Sasa ni wakati wako wa kuamua,Je unahitaji kuanzisha blog?

Katika Makala hii nimejitahidi kuelezea faida za kuanzisha blog na kumiliki blog yako mwenyewe. Pia nimezungumzia maswali ya msingi unayopaswa kujiuliza kabla hujaingia kwenye kazi hii.

Kumbuka kuwa , kama unaweza kupata masaa machache tu kwa juma na ukawa na mada unayopenda kufundisha, hakuna kitakachokuzuia wewe kuanzisha na kujipatia kipato kupitia blog. Songa mbele!

Nimatumaini yangu kuwa umepata maarifa ya kukusaidia kuanzisha blog .Kama una maoni yoyote, usisite kudondosha maoni yako hapa chini! Pia unaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kama unahitaji ushauri, kuhusiana na jinsi ya kujiajiri na kutengeneza pesa mtandaoni kwa simu namba 0752081669.

Asante na karibu katika makala ijayo.

Njia 9 Za Kutengeneza Kipato Kupitia Blog.

Njia 9 Za Kutengeneza Kipato Kupitia Blog.

Kama unasoma Makala hii kwa sababu unahitaji kujua jinsi ya kutengeneza pesa(kipato) kupitia Blog, basi nikuhakikishie kuwa upo mahali sahihi.

Soma: Njia 10 za kutengeneza pesa mtandaoni bila kuathiri muda wako wa kazi

 Katika Makala hii nimekuandikia njia 9 ambazo unaweza kuzitumia kujipatia kipato kupitia blog yako.

Jinsi ya kutengeneza pesa (kipato) kupitia Blog:Njia 9 unazoweza kuzitumia.

  1. Makala za kulipia(sponsored Blog Content)
  2. Kutangaza na kuuza Bidhaa za makampuni kwa lengo la kupata gawio(commisions)(Affiliate Programs)
  3. Kuweka matangazo ya Biashara kwenye Blog(Blog Advertisements)
  4. Kuuza kozi mbalimbali mtandaoni
  5. Kuuza bidhaa mbalimbali(Physical Products)
  6. Kuuza software mtandaoni
  7. Kuuza huduma zako mtandaoni
  8. Kuandika na kuuza Vitabu pepe (ebooks)
  9. Kuwa mshirika wa kibiashara na Makampuni mbalimbali.

Kama wewe ni mgeni kabisa kuhusiana na Blog, kabla ya kuendelea na Makala hii, unaweza kupitia Makala ya Jinsi ya kuanzisha Blog na kutengeneza pesa mtandaoni: Mwongozo rahisi wa jinsi ya kuanzisha Blog.

Kimsingi ,kuwa na blog yako mtandaoni ambayo tayari imekwishaanza kupata watembeleaji ni hatua ya kwanza kuelekea kuanza kujipatia kipato. Japokuwa ni jambo jema kufikiria njia ambazo unaweza kuzitumia kujipatia kipato kwenye blog yako hata kama ndio kwanza umeianzisha,Makala hii inawafaa zaidi wale ambao tayari wana blog zao na wameshaanza kupata watembeleaji na hivyo wanahitaji kuzipeleka blog zao katika hatua nyingine ambayo watakuwa wakijipatia kipato. Hivyo, kama bado hujaanzisha blog, unaweza kupitia Makala yangu ya Jinsi ya kuanzisha Blog na kutengeneza pesa : Mwongozo rahisi wa jinsi ya kuanzisha Blog.

Jenga msingi imara wa Blog yako kabla ya kufikiria namna ya kutengeneza kipato.

Kabla ya kwenda moja kwa moja kwenye njia za kuingiza kipato kupitia blog,hebu tujikumbushe kwa ufupi ni nini kinatakiwa ili uweze kuwa na blog yenye mafanikio.

Ili uweze kuwa na blog yenye mafanikio tuliona kuwa unapaswa kuchagua kwa uangalifu mada (niche),kuandika Makala zenye mvuto na kuitangaza blog yako ili uweze kupata wasomaji wengi. Hivyo baada ya kuwa umefanya mambo hayo yote ndio unaanza kufikiria jinsi ambavyo utajipatia kipato kupitia blog yako.

Sasa hebu tuangalie njia ambazo uanweza kuzitumia kutengeneza kipato kupitia Blog yako.

Jinsi ya kutengeneza pesa (kipato) kupitia Blog:Njia 9 unazoweza kuzitumia.

1. Makala za kulipia (Sponsored Blog Content)

Nini maana ya Makala za kulipia (sponsored content)? Hizi ni Makala ambazo Kampuni au mtu binafsi anakulipa ili uweze kuandika kwenye blog yako Makala ambayo itakuwa inaelezea Bidhaa au biashara ya kampuni yake. Kwa sababu blog yako itakuwa na wasomaji wengi, hivyo makampuni yanaweza kufanya makubaliano na wewe ili uandike Makala zinazotangaza biashara zao.

Hivyo baada ya blog yako kuwa na wasomaji wengi,unaweza kufanya makubaliano na makampuni mbalimbali au watu binafsi kuwatangazia biashara zao kupitia kuandika Makala kwa malipo.

Unapokuwa umepata kampuni au mtu binafsi ambaye ana bidhaa na anataka uandike Makala kuelezea bidhaa yake,hakikisha kuwa unakuwa mkweli kulingana na ubora wa bidhaa hiyo kwa wasomaji wako. Hii ni kwa sababu wasomaji wako watakuwa wanakuamini na hivyo chochote unachokiandika kwenye blog yako hakikisha kuwa kina ukweli ili kuendelea kujenga Imani ya wasomaji wako. Jambo la msingi ni kuwa hakikisha bidhaa au biashara ambayo utaamua kutangaza inaendana na mada za blog yako.

2. Kutangaza na kuuza Bidhaa za makampuni kwa lengo la kupata gawio(Affiliate Programs)

Hii ni njia nyingine ya kutengeneza kipato kupitia blog yako. Katika njia hii ya affiliate Program unajiunga na makampuni yanayouza bidhaa kwa lengo la kutangaza bidhaa zao.Baada ya kujiunga utapewa matangazo yenye link ambayo utayaweka kwenye blog yako.Kila mtu anayebofya link hiyo atapelekwa kwenye tovuti ya kampuni linalouza bidhaa hiyo. Kila mtu anayenunua bidhaa kupitia link yako wewe unalipwa kamisheni kutokana na mauzo ya bidhaa hiyo.Miongoni mwa makampuni yanayotoa huduma hii ni Amazon,Aliexpress na mengine mengi yaliyoko nje ya nchi. Kwa Tanzania kuna Dudumizi n.k

3.Kuweka matangazo ya Biashara kwenye Blog(Blog Advertisements)

Kuweka matangazo kwenye blog ni njia rahisi ambayo unaweza kuitumia kujitengenezea kipato.Hata hivyo njia hii kwa kuwa ni rahisi kipato utakachoingiza ni kidogo sana kama blog yako ina watembeleaji wachache. Miongoni mwa platform ambazo unaweza kujiunga na kuweka matangazo yao ni hizi zifuatazo:PropellerAds ,Google AdSense na mengine mengi. 

4. Kuuza kozi mbalimbali mtandaoni.

Je una ujuzi au maarifa yoyote ambayo unaweza kufundisha watu wengine? Je wasomaji wako wanakuona kuwa wewe ni mtaalam katika ujuzi fulani?

Tengeneza kipato kupitia ujuzi wako kwa kuandaa kozi na kuiuza mtandaoni (creating an online course ) na hapo utakuwa umetengeneza mfereji wa kukuingizia kipato kwa muda mrefu .

Kuandaa na kuuza kozi mtandaoni ni njia rahisi kwani unaweza kurekodi video fupifupi zinazofundisha ujuzi ulionao kulingana na mada unayofundisha kwenye blog yako na ukazipangilia vizuri na kutengeneza kozi ambayo utaiuza mtandaoni kupitia blog yako.Kumbuka kuwa, kama una ujuzi fulani,watu wanahitaji ujuzi wako uweze kuwasaidia katika maisha yao na hivyo wako tayari kununua ujuzi huo. Kazi kwako!

Ushauri wangu unapokuwa unahitaji kutengeneza kipato kupitia kuandaa kozi mtandaoni, ni kwa kuanza kuandaa kozi fupifupi.

Jinsi gani unaweza kuandaa kozi yako ya kwanza mtandaoni?

Jambo la kwanza kabisa,utatakiwa kujua ni ujuzi au maarifa gani unayotaka kufundisha( na itachukua muda gani kwa mtu kujifunza ujuzi huo).

Baada ya hapo,fanya utafiti upate kujua kama ujuzi au maarifa hayo unayotaka kufundisha watu wanayahitaji.

Baada ya hapo,gawanya ujuzi unaotaka kuuandalia kozi katika masomo mbalimbali. Kwa mfano, una blog inayofundisha ujasiriamali na unahitaji kuaandaa kozi ya Jinsi ya kuanzisha Biashara. Hapa utatakiwa kugawa maarifa haya katika video fupifupi zizoelezea somo mojamoja kwa mfano:

  • Nini maana ya Biashara
  • Jinsi ya kupata wazo la Biashara
  • Jinsi ya kuandika mchanganuo wa Biashara
  • Hatua za kufuata ili kuanzisha Biashara
  •  Jinsi ya Kusajiri Jina la Biashara BLERA n.k

Video hizi utazipangilia kwa lengo la kufikisha ujuzi uliokamilika kwa msomaji wako na hivyo kumuwezesha kutatua changamoto aliyonayo na hivyo kubadili maisha yake.

Kwa kweli fursa ni nyingi sana kutengeneza kipato kupitia kuandaa kozi kwenye blog yako.Jambo la kuzingatia ni kuwa,hakikisha kozi unazoandaa ziendane na mada(niche) unayofundisha kwenye Blog yako.

Ifanye kozi yako ya kwanza kuwa rahisi na utaendelea kuboresha zaidi unavyoendelea kupata uzoefu unapoendelea kuandaa kozi zinazofuata.

5.Kuuza bidhaa mbalimbali(Physical Products)

Pia njia nyingine ambayo unaweza kuitumia kuingiza kipato ni kuuza Bidhaa zako mwenyewe. Unaweza kufungua duka la mtandaoni kwenye ukurasa mmojawapo wa blog yako na ukauza na watu wakanunua moja kwa moja kwenye blog yako.

Unaweza kutafuta supplier kutoka kwenye soko la mtandaoni la Alibaba na ukaagiza bidhaa kwa lebo yako na ukauzia watu kwenye blog yako.

6.Kuuza software mtandaoni.

Je wewe ni mtaalamu wa computer (developer)? Au kama sio wewe je una rafiki yako ambaye ana ujuzi huo? Kama una ujuzi huo,unaweza ukaanzisha blog inayohusiana na ujuzi ulio nao na kisha ukaandaa software ambayo utaiuza kupitia blog yako kwa wasomaji wako. Hii ni njia nzuri sana ambayo itakuletea kipato kikubwa na endelevu.

7.Kuuza huduma zako mtandaoni

Kuuza ujuzi ulionao kama huduma inakaribia kufanana na kuuza kozi mtandaoni.Tofauti inakuja kuwa unapouza ujuzi wako mtandaoni unakuwa ukitoa huduma kwa mtu mmoja mmoja au vikundi vya watu kwa kuongea nao na kutoa ushauri au huduma yako.Hivyo wanakulipa kwa kutoa huduma yako.

8.Kuandika na kuuza Vitabu pepe (ebooks)

 Kuandika na kuuza vitabu pepe(ebooks)  ni njia nzuri sana ya kutengeneza kipato kupitia blog yako.Uzuri wa hii njia ni kuwa ukiwa tayari umemaliza kuandika kitabu chako na kukiweka mtandaoni,huhitaji gharama zingine za ziada bali kitabu chako kitaendelea kukuletea kipato kwa muda mrefu wa miezi na miaka!

9. Kipato kupitia washirika wa kibiashara(Business Partnerships)

Pale unapokuwa na blog iliyofanikiwa na kuwa na wasomaji wengi,hapo utavutia washirika wengi wa kibiashara kuungana na wewe ili waweze kutangaza biashara zao kupitia blog yako. Hii ni kwa sababu utakuwa una mtaji mkubwa wa watu.Wanaweza kutumia blog yako kuuza bidhaa au kutangaza huduma zao na wewe wakakulipa.

Kama nilivyosema hapo mwanzoni mwa Makala hii,unatakiwa kwanza kukuza blog yako ndio uweze kufikiria jinsi ya kutengeneza kipato.

Je una swali au komenti yoyote? Usisite kudondosha komenti yako hapa chini! Pia kama una hitaji ushauri wowote, usisite kuwasiliana nami kwa simu namba 0752081669. Karibu katika makala ijayo.

Jinsi Ya Kuchagua Mada (Niche) Kwa Ajili Ya Blog Yako.

Jinsi Ya Kuchagua Mada (Niche) Kwa Ajili Ya Blog Yako.

Watu wengi wanapotaka kuanzisha blog, hupata shida waanzishe blog kuhusiana na mada ipi. Kama na wewe ni miongoni mwao,nitakupatia hatua rahisi ambazo ukizitumia utaweza kupata mada bora kwa ajili ya blog yako. Katika makala hii nitazungumzia Jinsi ya kuchagua mada (niche) kwa ajili ya blog yako. hebu tuanze kuangalia hatua hizo.

Soma: Njia 9 za kutengeneza kipato kupitia blog

Jinsi ya kuchagua mada(niche) kwa ajili ya blog yako.

1. Chukua karatasi na Orodhesha vitu vyote unavyovipenda.

Nini unapenda kufanya au kuzungumzia?

Orodhesha vitu vyote unavyovipenda kuvifanya au kuvizungumzia kwenye maongezi yako. Haijalishi ni vikubwa au ni vidogo,we viandike tu.

Inawezekana kwenye orodha yako baadhi ya vitu vikawa kwa mfano:

  • Biashara ndogondogo
  • Soka
  • mazoezi
  • Kuchati facebook na Instagram.
  • Kuogelea
  • Kusoma vitabu n.k

Sasa baada ya kuwa umeorodhesha, unapoangalia orodha yako utashangaa kuona kuwa kuna baadhi ya vitu ulivyoorodhesha vinaweza kuwa mada nzuri kwa ajili ya wewe kuanzishia blog yako. Hivyo weka alama ya nyota kwenye vitu unavyoona kwenye orodha yako vinakupendeza zaidi na vinaweza kuwa ni mada za kuanzishia blog ili uje uvirudie baadaye.

2. Fikiria juu ya Blog,magazeti na vitabu unavyopenda kusoma.

Jinsi Ya Kuchagua Mada (Niche) Kwa Ajili Ya Blog Yako.

Sasa hebu weka pia orodha ya blog,magazeti na vitabu unavyopenda kusoma. Kisha orodhesha mada ambazo huwa unapenda kusoma kwenye vitabu, magazeti au blog hizo. Utashangaa baadhi ya mada ulizoorodhesha zinaweza kuwa ni mada bora za wewe kuanzisha blog yako. Weka alama ya nyota kwenye mada ambazo unaona zinakuvutia ili baadaye uje uzirudie kuziangalia upya.

3. Orodhesha kazi zote ulizowahi kufanya na zile unazoendelea kufanya na uzoefu wako.

Njia nyingine ya kuchagua mada (niche) ni kwa kuangalia ni kazi gani ulizowahi kuzifanya au unaendelea kuzifanya? Ziorodheshe hata kama ni ndogo kiasi gani.Lakini unapendelea vitu gani (hobbies)? Viorodheshe. Inawezekana ukaanzisha blog kuhusiana na ujuzi wako wa kazini au ukachagua kipengele kimoja kati ya majukumu au ujuzi ambao unautumia kazini. Pia unaweza kuanzisha blog kutokana na hobby yako. Hivyo vyote viorodheshe. Baada ya hapo angalia kwenye orodha yako vitu ulivyovipenda zaidi na uviwekee alama ya nyota ili uje kuviangalia zaidi baadae.

4. Orodhesha vitu ulivyowahi kuvikamilisha.

Andika orodha ya vitu ulivyowahi kuvikamilisha katika maisha yako. Kwa mfano;

  • Semina ulizowahi kuhudhuria
  • Kozi ulizowahi kusoma n.k

Vyote hivi vinaweza kuwa ni vyanzo vya wewe kupata mada ambayo utaitumia kwenye blog yako. Orodhesha ujuzi ulioupata na kwenye hiyo orodha ,weka alama ya nyota kwenye ujuzi ulioupenda zaidi ili baadaye uje kuuangalia zaidi.

5. Angalia mada zenye umaarufu ambazo zitaendelea kuwa maarufu kwa miaka mingi ijayo.

Pia kama bado unapata kikwazo, orodhesha mada ambazo kwa kweli zitaendelea kuwa na uhitaji kwa miaka mingi ijayo na uangalie kipengele kitakachokufaa kwenye blog yako. Mfano wa mada hizo ni:

  • Biashara: Hii inajumuisha vipengele kama jinsi ya kuongeza kipato,jinsi ya kuanzisha biashara, jinsi ya kuwekeza,jinsi ya kupunguza matumizi,jinsi ya kuepuka madeni n.k
  • Afya:Hii inachukua eneo kubwa sana.Baadhi ya mada zake ni Jinsi ya kupunguza uzito,Afya ya akili,tiba mbadala n.k
  • Malezi: Hii inajumuisha malezi ya watoto.
  • Ujasiriamali: Hii inajumuisha jinsi ya kujiajiri n.k
  • Utengenezaji wa Tovuti: Hii inajumuisha jinsi ya kutumia WordPress n.k

Sasa mada zote ulizozipenda na kuziwekea alama ya nyota unaweza sasa kuangalia ni mada ipi itakufaa.Ili uweze kujua kama mada uliyoichagua itakufaa, unaweza kuipima kwa kutumia maswali yafuatayo:

Maswali 9 ya muhimu unayopaswa kujiuliza unapochagua mada(niche) kwa ajili ya blog yako.

Kabla ya kuchagua mada (niche) yoyote kati ya zile ulizoziwekea nyota jiulize maswali yafuatayo.

Swali #1. Je unaipenda kiasi cha kutosha mada uliyoichagua?

Unaweza kushawishika kuchagua mada kutokana na umaarufu wake.Lakini jambo la msingi kujiuliza ni kuwa ,je unaipenda kiasi cha kutosha mada uliyoichagua? Hii ni kwa sababu mada uliyoichagua utakuwa ukiitumia kwenye blog yako kwa miaka mingi ijayo. Hivyo ukichagua mada ambayo huipendi kiasi cha kutosha,kadri muda unavyokwenda utakosa hamu ya kuendelea kuandika na hivyo blog yako kufa.

Swali #2. Je una maarifa ya kutosha kutokana na mada uliyoichagua?

Kama unataka kujenga blog yenye mafanikio unatakiwa  kuandika makala ambazo zitakuwa na msaada mkubwa kwa wasomaji.Ili uweze kuwa unaandika Makala ambazo watu watazipenda na zenye kuelimisha unatakiwa kuwa na maarifa yakutosha kutokana na mada yako. Hii ni kwa sababu wasomaji watakuwa wanakutegemea wewe kuwa ni mtaalamu wa mada husika na hivyo wakati mwingine watahitaji kupata msaada wa ziada. Hivyo hakikisha una uelewa wa kutosha mada uliyoichagua.

Swali #3. Je ukiamua kuuza bidhaa au huduma kutokana na mada uliyoichagua watu watu watakuwa tayari kununua?

Kabla ya kuanzisha blog unatakiwa pia kujiuliza je kuna bidhaa au huduma yoyote ambayo utakuwa unauza kutokana mada uliyoichagua? Kwa mfano: Unahitaji kuanzisha blog kuhusiana na Biashara ndogondogo,

 Je ukiuza vitabu,kozi ,bidhaa au huduma inayohusiana na mada yako watu watakuwa tayari kununua?

Hilo pia ni swali unalopaswa kujiuliza kabla ya kuchagua mada hiyo.

Swali #5. Je mada uliyoichagua itaendelea kuhitajiwa na watu kwa miaka mingi ijayo?

Swali jingine la msingi ni kuwa, mada uliyoichagua itaendelea kuhitajiwa na watu kwa miaka mingi ijayo? Kama utachagua mada ambayo itakuwepo kwa muda mfupi halafu ikapitwa na wakati utajikuta kuwa blog yako itakuwa haihitajiki tena.

Swali #6. Je kuna ushindani kiasi kwenye mada uliyoichagua?

Unaweza ukafikiria kuwa mada nzuri ni ile ambayo haina ushindani yaani  hakuna blog nyingine zinazotoa mada hiyo. Lakini ukweli ni kuwa ukiona mada uliyoichagua haina ushindani kabisa tafsiri yake ni kuwa inawezekana mada hiyo haihitajiki sana na ndio maana hakuna blog zinazofundisha mada hiyo. Hivyo, chagua mada yenye ushindani wa wastani.

Swali #7. Je unafurahia watu wanapokutambua kuwa wewe ni mtaalam wa mada uliyoichagua?

Ili uweze kufanikiwa kwenye kazi ya blog, ni lazima kuchagua mada (Niche) unayoipenda. Ingawa hutamtangazia kila mtu kuwa wewe ni mwandishi wa blog inayoelezea mada kwa mfano ya malezi ya watoto, lakini ni jambo jema kufurahia mada uliyoichagua na pia kuona fahari watu wanapokutambua kuwa wewe ni mtaalamu wa elimu ya malezi ya watoto. Usichague mada ambayo utaona aibu kujitambulisha kwa watu kuwa wewe ni mtaalamu wa mada hiyo.

Swali#9. Je mada uliyoichagua itakuwa na Makala ambazo zitadumu kwa muda mrefu bila kupoteza thamani yake?

Hapa ninazungumzia Makala ambazo zikisomwa leo,kesho zinakuwa zimepitwa na wakati kwa mfano Makala zinazozungumzia matukio ya siku(News). Siku inapopita Makala uliyoiandika inakuwa haina thamani tena.Hivyo unapochagua mada kwenye blog yako usichague mada ambayo itakuwa na Makala ambazo thamani ya Makala zake zitadumu kwa muda mfupi.Chagua mada ambayo Makala zake zitakuwa na ubora uleule kwa miaka mingi ijayo (evergreen content). Hebu nitoe mfano wa mada ya Ujasiriamali: katika mada hiyo ukawa umeandika Makala ya “JINSI YA KUANZISHA BIASHARA BILA KUWA NA MTAJI WA PESA”. Makala hii hata ikipita miaka 10 itaendelea kuwa na ubora uleule japo kadri muda unavyoenda utakuwa ukiiboresha tu kulingana na mabadiliko ya jamii na teknolojia.

Faida ya kuwa na Makala zenye ubora unaodumu kwa muda mrefu(evergreen content) ni kuwa:

Badala ya kuandika makala mpya mara kwa mara kuvuta wasomaji wa Blog yako, Makala hizi zitakuwezesha kuvuta wasomaji kuja mara  kwa mara kwenye blog yako hata kama hujaweka Makala zingine mpya. Hii ni kwa sababu maudhui ya Makala zako yatabaki kuwa na ubora uleule.

Njia 4 ambazo unaweza kuzitumia kujihakikishia kuwa utafanikiwa kwenye mada uliyoichagua kabla ya kuanzisha Blog.  

Sasa tayari umeamua kuchagua mada ambayo utaitumia kwenye blog yako. Tutaenda kuangalia majaribio au njia ambazo utazitumia kujihakikishia kuwa utafanikiwa kwenye mada uliyoichagua.

Jaribio #1. Jaribu kufikiria na kuandika vichwa vya habari vya Makala angalau 50 vinavyohusiana na mada uliyoichagua.

Tenga muda wa kama saa moja hivi ukiwa peke yako sehemu tulivu. Chukua kalamu na daftari na jaribu kufikiria vichwa vya habari vya Makala zinazohusiana na mada yako.

Andika vichwa vya habari vingi kadiri unavyoweza . Lengo ni kuandika vichwa vya habari angalau 50.

Kwa mfano: Hebu tuchukulie kuwa umechagua mada ya MALEZI:

Hebu tuanze kufikiria vichwa vya habari vinavyoendana na mada yetu:

  1. Jinsi ya kulea mtoto akiwa bado tumboni
  2. Sababu 6 zinazoathiri ukuaji wa mtoto baada ya kuzaliwa
  3. Jinsi ugomvi kati ya baba na mama unavyoathiri malezi ya watoto
  4. Jinsi ya kuwafundisha watoto kusoma wakiwa nyumbani.
  5. ………….
  6. …………..
  7. ………….

Kama ukiishiwa vichwa vya habari kwenye hili zoezi kabla ya kufikia vichwa vya habari 50, basi hii ni dalili kuwa inawezekana mada uliyoichagua haitakuwa chaguo sahihi kwako. Hii ni kwa sababu ili blog yako ianze kupata umaarufu na kupata muitikio kutoka kwa wasomaji,unatakiwa uwe umeandike Makala nyingi Zaidi ya 50.

Jaribio #2. Fungua Ukurasa wa Facebook au Group la Facebook linalohusu Mada uliyoichagua.

Njia nyingine na ya moja kwa moja ya kuangalia mada uliyoichagua kama itakufaa ni kuanzisha ukurasa wa Facebook au Group.

Unaweza kuupa ukurasa wako au group lako jina ambalo utalitumia kwenye blog yako.

Anza kuandika Makala na kuziweka kwenye ukurasa wako au group lako. Kama utafurahia kuposti na kuanza kupata wafuasi ambao watakuwa wakikomenti na kulike basi hiyo ni dalili nzuri kuwa utafurahia kuendesha blog kwa mada uliyoichagua.

Jaribio #3. Jaribu kuandika Makala tano zinazoendana na mada yako.

Mwisho, jaribu kuandika Makala tano zinazoendana na mada yako.

Kama utaona kuandika Makala tano ni nyingi au kama utachoka (bored) baada tu ya kuandika Makala moja, basi unapaswa kufikiria upya uchaguzi wako wa mada inawezekana umechagua mada ambayo sio sahihi kwako.

Kwa ufupi: Jinsi gani unaweza kuchagua mada bora kwa ajili ya blog yako?

Hapa ninakupatia vitu vitatu vya kufuata (checklist):

 Fikiria mada nyingi iwezekanavyo kabla ya kuchagua mada moja. Kwa kuwa na mada nyingi ulizozifikiria unaweza kupata mada bora Zaidi kutokana na mada ulizozifikiria.

 Zifanyie mada zako majaribio kama nilivyokuelekeza katika Makala hii ili kupata mada moja ambayo itakuwa bora kuliko mada zingine.

 Kwa kutumia majaribio niliyokuelekeza katika Makala hii utaweza kuchagua mada (niche) bora sana kwa ajili ya blog yako.

Kwa leo niishie hapo. Kama una maoni yoyote kuhusiana na makala hii ya Jinsi ya kuchagua mada(niche) kwa ajili ya blog yako, usisite kudondosha maoni yako hapa chini. Pia kama unahitaji ushauri wowote, wasiliana nami kwa simu/whatsap 0752081669.

Asante na karibu katika makala zijazo.

Jinsi Ya Kuandika Makala Zenye Mvuto Mtandaoni.

Jinsi Ya Kuandika Makala Zenye Mvuto Mtandaoni.

Kujifunza  jinsi ya kuandika Makala zenye mvuto ambazo watu watapenda kuzisoma na hivyo kuwa na wasomaji wengi kwenye blog yako si jambo gumu.Ni kweli, inachukua muda mrefu,nguvu pamoja na mazoezi ya kutosha ili uwe mwandishi uliyebobea.Lakini kama unahitaji kujifunza jinsi ya kuandika Makala ambazo zitapendwa na watu na kukuongezea wasomaji kwenye blog yako unaweza kuanza baada ya kuwa umesoma mpaka mwisho Makala hii.

Katika Makala hii ya jinsi ya kuandika Makala zenye mvuto tutazungumzia kila kitu kuanzia jinsi ya kuwatambua wasomaji wako,mpaka kwenye kanuni  ya jinsi ya kupata mawazo ya Makala zitakazopendwa na wasomaji wako,Jinsi ya kuandika vichwa vya habari vitakavyovuta usikivu wa wasomaji wako na kuwafanya wahamasike kusoma Makala zako,Jinsi ya kupangilia Makala zako ili ziweze kusomeka na kueleweka kwa urahisi na mambo mengine mengi..

Jinsi ya kuandika Makala zenye  mvuto zitakazopendwa na wasomaji na kukuletea pesa mtandaoni.

Jinsi Ya Kuandika Makala Zenye Mvuto Mtandaoni.
  1. Wafahamu wasomaji wako
  2. Andika kichwa cha habari kinachovutia kwenye kila makala yako
  3. Vuta usikivu wa wasomaji wako toka mwanzo wa makala yako
  4. Fanya makala zako zisomeke na kueleweka kwa urahisi.
  5. Tumia picha na vielelezo kwenye makala zako
  6. Andika makala zinazolenga kutatua changamoto ya msomaji.
  7. Hakikisha makala zako zinaonekana vyema hata kwenye simu za mkononi.
  8. Lenga zaidi katika ubora kuliko wingi wa makala.

1. Wafahamu vyema wasomaji wako.

Kabla ya kujifunza jinsi ya kuandika Makala, unatakiwa tayari uwe umechagua mada ambayo utakuwa ukiitumia kwenye blog yako,kwa kiingereza inaitwa niche. Kwa mfano inawezekana ukawa umeanzisha blog yenye mada(niche) ya Ujasiriamali. Hivyo unatakiwa uchague mada ambayo utaitumia kwenye blog yako.Mada ndio itakayoitambulisha blog yako kuwa inaelezea kuhusiana na mambo gani. Katika mada yako,chambua ni aina gani ya maarifa au Makala ambazo ukiandika zitatatua changamoto za wasomaji wako na hivyo kuwafanya wavute usikivu katika kusoma Makala zako. Andika vitu ambavyo wasomaji wako wanahitaji kujua na sio vile ambavyo wewe unataka kuwaambia.

Chambua kwa umakini changamoto zinazowakabili wasomaji wako na hivyo uweze kuandika maarifa ambayo kwa kweli ni hitaji lao.

2. Andika kichwa cha Habari kinachovutia kwenye kila Makala yako na kinacholenga kutatua changamoto zao.

Kichwa cha habari kinapokuwa kizuri na kinachovutia na kutatua changamoto kitaifanya Makala yako ipate wasomaji wengi.Hata unapoishare Makala yako kwenye mitandao ya kijamii, watu huanza kwanza kusoma kichwa cha habari kabla ya kusoma Makala yote. Hivyo ni muhimu kutatua changamoto ya msomaji kuanzia kwenye kichwa chako cha habari ili aone umuhimu na sababu yakusoma Makala yako.

Kabla hata watu hawajaanza kusoma Makala yako, kwa kusoma tu kichwa cha habari, wanakuwa tayari wamekwishaanza kuelewa unachoenda kuzungumzia.

Utafiti unaonyesha kuwa  watu 6 kati ya  10  hushare Makala kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook,Twitter na LinkedIn kwa kusoma na kuvutiwa tu na kichwa cha habari.

Sasa unawezaje kuandika kichwa cha habari ambacho kitawavutia watu na kuwafanya wasome Makala yako na kuishare?

Sasa hebu tuangalie vitu vichache ambavyo unatakiwa kuvizingatia ili uweze kuandika kichwa cha habari kinachovutia

  • Tumia namba: Watu huwa wanatafuta mtandaoni njia rahisi ya kutatua changamoto zao.Hivyo ukiandika Makala ambayo ni mwongozo unaoonesha hatua kwa hatua jinsi ya kutatua jambo Fulani, watu watahitaji kusoma Makala hiyo.

Kwa mfano:Njia 10 za kutengeneza pesa mtandaoni

Pia unaweza kutumia mwaka kuonesha kuwa Makala yako ni ya muda huu na kuwa wasomaji wanapata maarifa ambayo hayajapitwa na wakati.

Kwa mfano:Sababu 8 za wewe kuanzisha na kuwa na Blog yako mwenyewe kwa mwaka huu wa 2021.

Angalizo: Usisubiri mpaka uwe umepata kichwa cha habari ambacho kimekamilika ndio uandike Makala,andika kichwa cha habari kadiri unavyoweza na utaendelea kuboresha kichwa chako cha habari .

Endelea kuandika Makala yako na mawazo ya vichwa mbalimbali vya habari yatakuwa yanakuja kwenye akili yako na baadaye utapata kichwa cha habari ambacho kitakufaa.

3. Vuta usikivu wa wasomaji toka mwanzo wa Makala yako.

Una sentensi moja mpaka mbili kuwafanya wasomaji wasome Makala yako au la. Hivyo kama unahitaji watu wasome Makala kwenye blog yako lazima uanze kwa sentensi ambayo itawavuta wawe na sababu ya kuendelea kusoma Makala yako.

Njia rahisi ya kuandika utangulizi mzuri ambao utawavuta wasomaji kuendelea kusoma Makala yako ni kuanza kwa kujibu Nani,Nini,wapi, lini haraka iwezekanavyo.

Katika kizazi hiki cha watu waliochoka kusoma unatakiwa kuweka pointi zako ziwe wazi badala ya kuzificha na msomaji aanze kuzitafuta.

Unapoweka pointi zako wazi mwanzoni unatoa sababu kwa msomaji kuendelea kusoma Makala yako.

4.Fanya makala zako zisomeke na kueleweka kwa urahisi.

Ni mara chache sana watu husoma neno kwa neno mtandaoni labda mpaka pale wawe wamevutiwa na Makala.

Utafiti unaonyesha kuwa ni 20% tu ya watu husoma maelezo mwanzo mwisho mtandaoni.Hivyo ili Makala zako zipate wasomaji unatakiwa kuandika katika mfumo wa kuorodhesha point(list).

Mambo mengine ya kuzingatia ni haya:

  • Aya za Makala yako ziwe fupi
  • Tumia maneno rahisi kueleweka na wasomaji.
  • Tumia mfumo wa kuorodhesha (list) kwenye makala zako.
  • Weka vichwa vidogo vya habari kwenye Makala zako
  • Unaposisitiza pointi tumia bolditalics, au saizi tofauti ya maneno.
  • Mara kwa mara tumia picha,chati na vielelezo kwenye Makala zako.

5.Tumia picha na vielelezo kwenye makala zako.

Watu wanapenda kuona picha.Hilo ni lazima ulifahamu linapokuja suala la kuandika Makala ambazo zitawavutia wasomaji wako.

Zaidi ya 50% ya ubongo wetu hupokea,kutunza na kufanyia kazi taarifa ambazo zipo katika mfumo wa picha , ukilinganisha na 8% kwa kugusa na 3% kwa kusikia.

Ili kuweza kuwa na Makala zenye mvuto kulingana na utafiti huo,ukiongeza picha kwenye Makala zako utakuwa umeongeza thamani,kuheshimika na kuaminika .

Wakati huo huo unapokuwa unaandika makala yenye makosa mengi unapoteza heshima na uaminifu ambao wasomaji wako watakuwa wameujenga kwako.

6.Hakikisha makala zako zinaonekana vyema hata kwenye simu za mkononi.

Kila mmoja anafahamu kuwa ili Makala iweze kufikia watu wengi Zaidi ni lazima iweze kusomeka kwenye vifaa mbalimbali zikiwemo simu za mkononi. Hivyo hakikisha Makala zako zinaweza kuonekana vizuri kwenye aina mbalimbali za vifaa zikiwemo simu za mkononi.

7.Lenga zaidi katika ubora kuliko wingi wa makala.

Ni kweli kuwa kuandika Makala nyingi na mara kwa mara kunaifanya blog yako ipate wasomaji wengi.Lakini kama Makala unazoandika hazilengi kutatua changamoto za watu muda sio mrefu watu wataikimbia blog yako.Hivyo wekeza katika kuandika Makala zenye ubora hata kama ni mara chache kuliko kuandika Makala nyingi zisizokuwa na ubora. Jambo la kuzingatia tu ni kuwa hata unaandika mara chache ,lazima uwe na ratiba maalumu ya kuweka Makala zako.

Asante kwa kuwa nami katika Makala hii.Je una komenti yoyote? Usisite kudondosha komenti yako hapa chini.Pia kama unahitaji ushauri, usisite kuwasiliana nami kwa simu au whatsap 0752081669.

Asante na karibu katika makala ijayo.

error

Enjoy this blog? Please spread the word :)

Follow by Email
WhatsApp